Monday, December 26, 2011

Viongozi kulakula

Uongozi nahofia, wivi waweza ukawa,
Kama wanaojipatia, wakubwa waliokuwa,
Wanyonge kudhulumiwa, na kidogo kuchukuliwa,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kiongozi akipewa, milioni kwa mamia,
Na hawa nao raia, kumi hawajaijua,
Huu sio wizi hua, mchna waendelea?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kumi na nane saa, daktari atumia,
Wagonjwa kuhudumia, bila hata kupumua,
Twashindwa kuwaangalia, wenyewe twajiangalia?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Nesi kote huingia, haishi kujichafua,
Matapishi hufadia, na vinyesi kuchukua,
Bungeni unayekaa, chote hicho wachukua?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Mwalimu choki yaja, machoni na kwenye pua,
Elimu anaitoa, kesho watakaomnyonyoa,
Hili twaliangalia, tunashindwa kuamua,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Sahani mbili mwatwaa, tonge hatujalijua,
Na kisha mwagugumia, hakiwatoshi mwaonewa,
Ibilisi mmekua, binadamu twadhania?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kipimo mnachotumia, mimi bado kukijua,
Kiasi gani mwatwaa, na kiasi gani mwatoa?
Nini mnakichukua, na nini mwatupatia?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?


Au mwavuna mamia, hata msikopandia,
Kwingine mwakupua, vya wengine vilokua,
Hakika nawashangaa, watu msiojijua,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kwa haya mtachukia, ukweli nawaambia,
Mungu mkimtambua, mtageuka tabia,
Nafsi kuzizuia, wengine kuwatangulia,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Tazameni Malaysia, zamani walipoamua,
Viongozi kukataa, malipo yaliyozidia,
Wananchi kwanza kupewa, mtaji wakaendelea,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kisha wao kufatia, nchi imeshanyanyuliwa,
Nyie mwanza kutwaa, nchi inadidimia,
Na Mola kawaumbua, mafuriko kutokea,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Sasa tunawashangaa, mwashindwa wajengea,
Hivi mnategemea, muujiza kutokea,
Fisadi walizochukua, kwanini kutotumiwa,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Nyumba ninawaambia, kwa fakiri ndio dawa,
Hili ukishampatia, mengine atajijua,
Ila mkiliachia, dhulumati tatajua,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Uongozi nahofia, wivi waweza ukawa,
Kama wanaojipatia, wakubwa waliokuwa,
Wanyonge kudhulumiwa, na kidogo kuchukuliwa,

Kiongozi akipewa, milioni kwa mamia,
Na hawa nao raia, kumi hawajaijua,
Huu sio wizi hua, mchna waendelea?

Kumi na nane saa, daktari atumia,
Wagonjwa kuhudumia, bila hata kupumua,
Twashindwa kuwaangalia, wenyewe twajiangalia?

Nesi kote huingia, haishi kujichafua,
Matapishi hufadia, na vinyesi kuchukua,
Bungeni unayekaa, chote hicho wachukua?

Mwalimu choki yaja, machoni na kwenye pua,
Elimu anaitoa, kesho watakaomnyonyoa,
Hili twaliangalia, tunashindwa kuamua,

Sahani mbili mwatwaa, tonge hatujalijua,
Na kisha mwagugumia, hakiwatoshi mwaonewa,
Ibilisi mmekua, binadamu twadhania?

Kipimo mnachotumia, mimi bado kukijua,
Kiasi gani mwatwaa, na kiasi gani mwatoa?
Nini mnakichukua, na nini mwatupatia?

Au mwavuna mamia, hata msikopandia,
Kwingine mwakupua, vya wengine vilokua,
Hakika nawashangaa, watu msiojijua,

Kwa haya mtachukia, ukweli nawaambia,
Mungu mkimtambua, mtageuka tabia,
Nafsi kuzizuia, wengine kuwatangulia,

Tazameni Malaysia, zamani walipoamua,
Viongozi kukataa, malipo yaliyozidia,
Wananchi kwanza kupewa, mtaji wakaendelea,

Kisha wao kufatia, nchi imeshanyanyuliwa,
Nyie mwanza kutwaa, nchi inadidimia,
Na Mola kawaumbua, mafuriko kutokea,

Sasa tunawashangaa, mwashindwa wajengea,
Hivi mnategemea, muujiza kutokea,
Fisadi walizochukua, kwanini kutotumiwa,

Nyumba ninawaambia, kwa fakiri ndio dawa,
Hili ukishampatia, mengine atajijua,
Ila mkiliachia, dhulumati tatajua,

No comments: