Wednesday, June 22, 2011

Mswahili mpe ngono

1.
Tumeshasemwa weusi, na dunia yamaizi,
Ngono kwetu sarakasi,kuiacha hatuwezi,
Nyuma hufata mikosi,dhuluma na ugandamizi,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
2.
Mswahili yeye ngono, vinginevyo haviwezi,
Ona wakata viuno,walio nao ujuzi,
Hapanayo mabishano,Afrika huwawezi,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
3.
Ni asilimia tano,ndiyo ina uongozi
Baki tisini na tano,ni ya pombe na mapenzi,
Ni yanini maulizano,nchi hatuendelezi?
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
4.
Mswahili mke, mme, wote watazama chini,
Na sifa ya mwanamme,wangapi anadhamini,
Bora mema wayahame, jinsi wanavyoithamini,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
5.
Mengine hafikirii, kwa muda unaofaa,
Elimu hakimbilii, ila ngono ikitoa,
Na cheo hakichukui, ila ashiki kuvaa,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
6.
Heri wakuu wa kale,hili sana walijua,
Kuhasi wachagulile,ili tija kunyanyua,
Tufanyeje wateule,nchi yetu kuifaa?
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
7.
Mwili ni yetu dunia, nyingine hatuijui,
Mijitu mvi yajaa,bado hawayakinai,
Vitanda vinazagaa,hadi ofisi zadai,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
8.
Akikwaa utajiri, ngono ndiyo namba wani,
Hatendi kwa watu kheri, ila apate hisani,
Wanaponza itihari, nyoyo hazina imani,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
9.
Na cheo akikikwea, ngono ni yake shabaha,
Chupi atakazovua, hesabu hutoijua,
Ofisi alimokua,danguro Selemania,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
10.
Ukweli hawaupendi, sikia wanavyolalama,
Mwaukataa ufundi,hali mwavifua vyuma?
Nenda China na Uhindi,uone walivyo salama,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
11.
Mawaziri wanakaa, vibinti kuvitumia,
Milioni watumia,raha kujinunulia,
Nchi yateketea,hakuna anayejua,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
12.
Mkiwapa misaada, vibaya wanaitumia,
Waanza fuga vimada,ndani yote Tanzania,
Siasa sasa mnada,na ngono yasaidia,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
13.
Kichefuchefu chafua, wataka hutaki chukua,
Rohoni asiyejijua,Uongozi hufulia,
Tamaa wanaojaa,huishi wafu wakiwa,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
14.
Hili nalishuhudia, japo nitajachukiwa,
Mola ninamlilia, denda miye kunivua,
Watu nikawatumikiya, hadi siku ya kujifia,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.
15.
Labda kizazi kipya,kikija kutupindua,
Kiasi wanaojua, wakabadili tabia,
Tukawa nayo staha, maendeleo kwingia,
Mswahili yeye ngono, uongozi hauwezi.