Saturday, March 31, 2012

Mtaji ni kama mbegu

Ukifa hautokuwa, mtaji inavyokua,
Kitu hakitobakia, kufilisika ni njia,
Na ukishakuishiwa, mengi yatakusumbua,
Mtaji ni kama mbegu, ukiula haukui!

Talanta ukijaliwa, budi kuziangalia,
Tofauti ukajua, na hela iliyokuwa,
Kuguswa kutoridhia, salama mkabakia,
Jina mchoyo ukipewa, kubali na kuridhia,
Mtaji ni kama mbegu, ukiula haukui!

Mtaji mizizi hutoa, ndipo panapoanzia,
Hapo ukishikilia, chini hutotumbukia,
Ila ukja legea, pabaya utaingia,
Mtaji ni kama mbegu, ukiula haukui!

Mtaji wataka kulea, na maji kuumwagia,
Na hesabu kuzijua, unavyotakiwa kukua,
Usije ukapungua, nakisi ukaingia,
Mtaji ni kama mbegu, ukiula haukui!

Mtaji wataka mbolea, na samadi kuitia,
Na udongo kubambua, k isha ukadadavua,
Na dawa kuumwagiwa, wadudu kutokaribia,
Mtaji ni kama mbegu, ukiula haukui!

Kitu ukishagundua, mwenyewe kujifanyia,
Ndugu kutowaachia, na rafiki na jamaa,
Wengi waharibikiwa, watu kutumainia,
Mtaji ni kama mbegu, ukiula haukui!

Mtaji umeumbua, tajiri walodhania,
Wakajikuta nazaa, imekwishawachezea,
Hakuna wa kulmlilia, yazidi sepa dunia,
Mtaji ni kama mbegu, ukiula haukui!

Kila wakifikiria, uzembe wawashtakia,
Laiti wangelijua, mtaji wasingetoa,
Mchomgoma umekua,kushuka ukikataa,
Mtaji ni kama mbegu, ukiula haukui!

Kidogo ukidokoa, huwezi kurudishia,
Huwa kama ni balaa, ukianza nyong'onyea,
Dhiki hukukimbilia, wengine kuwakimbia,
Mtaji ni kama mbegu, ukiula haukui!

Kila muabudu pesa

MWISHO huja kuikosa, kila muabudu pesa,
Kila kitu humsusa, akabaki hana hisa,
Muflisi kutonesa, liporomoke darasa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Huzitamani anasa, aanze naye kutesa,
Akaziacha fursa, vyenye pato kuvinusa,
Akahama kudodosa, ahamie kutomasa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Huwa ni kisa na mkasa, tena visivyo msasa,
Abakie kipukusa, ndizi isiyo hasusa,
Mwilini akipapasa, akute hanayo hisa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Hisia haiwi hisa, wala halipi posa,
Mchumba utamkosa, ambebe bwana Issa,
Na mwishowe ukasusa, ndoa uache kabisa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Kosa halijawa kosa, hadi kurudia kosa,
Baraka ikikigusa, nusura huwa mkasa,
Ya jana yakawa sasa, mtu uzidi kutesa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Pamoja kujipapasa, shilingi nimeikosa,
Koti nimeshalinusa, bado siioni pesa,
Na chini nimetikisa, naona yote mkasa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Watu huja kuwatesa, kila muabudu pesa,
Akakopa na kususa, madeni yakawa h isa,
Na kokote mkunusa, harufu mtaikosa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Mtaenda kwenye misa, na masjidi kugusa,
Dua mtie vitasa, bado huwa ni makosa,
Nyusi akishapepesa, yote huwa yake hisa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Ukitaka kumgusa, hupasuka kama kasa,
Akalia na kususa, eti nyie mwamtesa,
Keshalishindwa darasa, kumsomesha si ruksa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Na pesa itamtosa, milele ikamsusa,
Abaki kula mikasa, na vingine vyenye tasa,
Rehema kutomgusa, h adi tawba kunusa,
Kila muabudu pesa, mwisho huja kuikosa!

Tumezoea majembe

Nawasema kuurumbembe, waliokubuhu vijembe,
Vichwa vyao wasivimbe, kuwasifu nisiambe,
Ninawaona ni ng'ombe, kuchinjwa wao ujumbe,
Tumezoea majembe, havitushindi vijembe!

Niacheni niwachambe, wanaokifu wajumbe,
Hata kitu wasirambe, kwenye hizo zao tembe,
Na popote wasitambe, bado ni wala maembe,
Tumezoea majembe, havitushindi vijembe!

Ajira yao waimbe, ili watu wasigombe,
Hutaka vichwa wavimbe, wavipate na vikombe,
Kwa kuzing'oa pembe, na kumwaga nyingi pombe,
Tumezoea majembe, havitushindi vijembe!

Wanataka uwalambe, na ya kwao uyaimbe,
Kama sivyo wakukumbe, wakuchanje kwa uwembe,
Macho yako wakufumbe, ya ovyo usiwachambe,
Tumezoea majembe, havitushindi vijembe!

Nendeni mkawabambe, huku wamevaa pembe,
Ni majini msiombe, mkutane na wazembe,
Bilauri na vikombe, huvitumia wachambe,
Tumezoea majembe, havitushindi vijembe!

Nalipika langu sembe, na mchuziwe wa shombe,
Vinginevyo usiambe, riziki yangu si chembe,
Pawa tila ni uvimbe, kwanini mguu usivimbe ?
Tumezoea majembe, havitushindi vijembe!

Nanywa hili langgu kombe, majirani msisambe,
Nitazikomesha ngebe, vya kwangu wasiviibe,
Niwafungie mikebe, wasikike wasitambe,
Tumezoea majembe, havitushindi vijembe!

Hatuogopi vijembe, tumezoea majembe,
Vinginevyo msitambe, wimbo wenu tuuimbe,
Na siku ya siku tugombe, mchawi wetu tumzombe,
Tumezoea majembe, havitushindi vijembe!

Kuna harufu ya hongo

HUJIFANYA watawala, wananchi wakazuga,
Wao wakipata kula, makombo watagawa-ga,
Maua katika yala, ni sehemu ya maboga,
Kuna harufu ya hongo, kauli za viongozi!

Ila lazuka suala, lisilotaka uoga,
Kileo pia kimila, udhia tukaubwaga,
Watu wasio fadhila, nao tupate waaga,
Kuna harufu ya hongo, kauli za viongozi!

Wanaotumia hela, haki zetu kuvuruga,
Kukataa yao hila, pembeni tukawaswaga,
Wabakie wenye ala, akili wanaotumia,
Kuna harufu ya hongo, kauli za viongozi!

Zinakwama zetu hali, kwa kuyabeba maboga,
Ni wachache wa fadhili, kwayo wakishakuroga,
Hukufanza ni anzali. wakazidi kujikoga,
Kuna harufu ya hongo, kauli za viongozi!

Ya kwao sio kamili, ndio kisa wanahonga,
Na wengine majahili, hujuma wanazitunga,
Budi mustakabali, hawa tukawavuruga,
Kuna harufu ya hongo, kauli za viongozi!

Ili tupate jamali, wa kale tuwapa bega,
Tuiwashe na kandili, yaliyo bora kuiga,
Tusiwe tena mithili, viumbe wanaofugwa,
Kuna harufu ya hongo, kauli za viongozi!

Hali zetu kubadili, budi tuache kuhongwa,
Tukamhofu Adili, kiboko kutotupiga,
Tukazijenga amali, na wengine kutuiga,
Kuna harufu ya hongo, kauli za viongozi!

Tumuombeni Jalali, mabaya tukayabwaga,
Uondoke mushkeli, neema tupate oga,
Zinawiri zetu hali, utu tupate kujenga,
Kuna harufu ya hongo, kauli za viongozi!

Unavuta blanketi

Kiasi ungelijua, yako ungeliyapima,
Yasipate kupungua, au kuzidi kasima,
Katikati ukatua, ungali bado wahema,
Unavuta blanketi, jua lakuamkua?

Muda unapoachia, yaweza zuka nakama,
Hili ukatangulia, na yale yakasimama,
Subira wasiokuwa, ndipo hapo hulalama,
Unavuta blanketi, jua lakuamkua?

Usingizi kuugua, ukizidi unauma,
Hali ikawa ni mbaya, pasiwe tena uzima,
Na haSa pakuzingatia, palipo na ndarahima,
Unavuta blanketi, jua lakuamkua?

Muda wataka tambua, umuhimu kuupema,
Na kila linalokuwa, nafasi ukaisoma,
Na somo ukalitoa, bila kuvunja kalmima,
Unavuta blanketi, jua lakuamkua?

Na usipojitambua, hili kwako si lazima,
Ila yatakayotokea, ujumbe zitautuma,
Na haki ukaridhia, bila vingine kusema,
Unavuta blanketi, jua lakuamkua?

Huwezi ukaelwa, muda wake mahakama,
Haukufuli rufaa, na masmaha kuchuma,
Hutoka ukaishia, hakuna kurudi nyuma,
Unavuta blanketi, jua lakuamkua?

Muumba wa zetu sanaa, namshukuru Adhama,
Nami nililopangiwa, kwa wakati kutazama,
Chumo nikajichumia, pahala pema kusimama,
Unavuta blanketi, jua lakuamkua?

Ukililia kiatu

KIATU ukililia, unapaswa kutambua,
Wapo waliozaliwa, miguu hawakupewa,
Hapungukiwi Jalia, ila hilo karidhia,
Ukililia kiatu, mwenzio miguu hana!

Mzazi hupungukiwa, unapaswa kulijua,
Ndiye anayezitoa, pindi anapojaliwa,
Kama asipogaiwa, ni kipi atakigawa?
Ukililia kiatu, mwenzio miguu hana!

Siwezi kujisifia, riziki ninaigawa,
Yapo juu alokuwa, nami ninamgonjea,
Hushukuru nikipewa, na kukosa naridhia,
Ukililia kiatu, mwenzio miguu hana!

Maisha yana hatua, kupata na kupotea,
Kama somo ukijua, sahihi na kukosea,
Na mengine majaliwa, hauwezi kuyajua,
Ukililia kiatu, mwenzio miguu hana!

Yako wewe angalia, na tosheka ukijua,
Wako juu watakuwa, nawe kati kubakia,
Na chini wakafatia, kama wewe wasojaliwa,
Ukililia kiatu, mwenzio miguu hana!

Mwana ninakuusia, jenga kinaya na dunia,
Na hautopungukiwa, utatosheka radhia,
Yao ukaangalia, na yako ukatumia,
Ukililia kiatu, mwenzio miguu hana!

Tosheka nayo dunia, nayo itakuachia,
Nje wanaoangalia, na husuda kuwajaa,
Husumbuka na dunia, kufa bado wana njaa,
Ukililia kiatu, mwenzio miguu hana!

Huwa watu wa kulia, kucheka wakakohoa,
Maji hawawezi tia, kinywani wametulia,
Shinikizo huingia, mapema kuteketea,
Ukililia kiatu, mwenzio miguu hana!

Akili ukijaliwa, wapaswa kuzitumia,
Fakiri ukijijua, juu zitakunyanyua,
Na subira ukilea, inshallah utajaliwa,
Ukililia kiatu, mwenzio miguu hana!

Chemchemi ikikauka

Mnagombea kitu gani, kisima hakina maji,
Nikifanya tathmini, hakuna mnachohitaji,
Na ujio siuoni, ila kuhama kijiji,
Chemchemi bila maji, mnagombea kitu gani ?

Nawaona Kisauni, bado mwatafuta m aji,
Walio kaskazini, sasa wawapeni uji,
Kiu hakiuamini, bado chalilia maji,
Chemchemi bila maji, mnagombea kitu gani ?

Na nyie Mchikichini, yako wapi mahitaji,
Mnauchoma ubani, wageuka kuwa mboji,
Bado yako ughaibuni, kwenu yasita hayaji,
Chemchemi bila maji, mnagombea kitu gani ?

Nimeuliza yamini, kama kuna ufujaji,
Yakawa bila thamani, tokea kwenye thaluji,
Wanasema yumkini, kwa hili si wasomaji,
Chemchemi bila maji, mnagombea kitu gani ?

Chemchemi bila maji, mnagombea kitu gani ?

Nimefika na Uzini, nilipotoka Kimbiji,
Utafiti kubaini, kisa chake ukosaji,
Na majibu si yakini, ila kuna uhitaji,
Chemchemi bila maji, mnagombea kitu gani ?

Nauliza Mkoani, na Chake kwenye mji,
Wao wayaficha ndani, mvua wakitaraji,
Watakuwamo shakani, ikiwa nayo haiji,
Chemchemi bila maji, mnagombea kitu gani ?

Malindi nikasaini, na Lamu nimewahoji,
Nauliza kuna nini, maji yakwama Buruji,
Au wapuuza dini, kakasirika wao Jaji?
Chemchemi bila maji, mnagombea kitu gani ?

Wanateta hadharani, bandari wanaitaraji,
Kama si leo mwakani, na nasara waundaji,
Kisiwa kiko shakani, Maajid kumsujudi,
Chemchemi bila maji, mnagombea kitu gani ?

Tuesday, March 27, 2012

AACHE JIJENGA YEYE, AKUJENGE WWE ?

Maisha yake mafupi, mja katika dunia,
Na akili zake fupi, katika kufikiria,
Hajui katoka wapi, atang'ang'ania bua,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Hatari haiogopi, huogopa manufaa,
Akakamata makapi, na punje kuziachia,
Kwa udhia fotokopi, ibilisi amekua,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Kwa neema hanenepi, zaidi hukimbilia,
Augua yanguyapi, bidhaa hajaijua,
Na kwa ukweli haapi, shetani keshamwingia,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Nusura muda haipi, yake kuyapalilia,
Hali siku zake ngapi, hilo hajaling'amua,
Nahodha hamuogopi, ni yeye ajidhania,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Uwe ni ndugu wangapi, hali hawataijua,
Huhesabu mali ngapi, sikuhiyo zaingia,
Ukikopa hakukopi, haukopesheki baa,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Hawaniulizi vipi, twaweza kukusaidia,
Wangoja tangazo fupi, msibani kunijia,
Mauti huwa ni papi, nyumba zao hujengea,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Nimeandika kifupi, kwani nachanganyikiwa,
Nje hauvai chupi, ila ndani yavaliwa,
Na mengi kama makapi, huwezi kuongelea,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Ndugu zangu siwatupi, ila sintowategemea,
Yamenishinda mangapi, nao wanaangalia,
Na wengine wako 'hepi', dhiki zikinifumua,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Uoza unachosifu....

Ni makao yake nzi, uozo ukisifiwa,
Usafi kwake ajizi, na manukato kinyaa,
Kwenye zama za ushenzi, hata mtu naye huwa,
Uoza unachosifu, ni ikulu yake nzi!

Wanaizaya wapuzi, nzi nawalingania,
Wengine kwao viazi, na wao wanaojua,
Hawaijui miezi, na inavyopanguliwa,
Uoza unachosifu, ni ikulu yake nzi!

Nyakati hawamaizi, za kupwa na kujajaa,
Hawayajengi makazi, pale palipotulia,
Ila ni yao hifadhi, pale panapotitia,
Uoza unachosifu, ni ikulu yake nzi!

Hudhani yao hijazi, ngazi walizopandia,
Kushuka chini hawezi, wa juu kachagulia,
Na mazao na mizizi, kati yake bora huwa,
Uoza unachosifu, ni ikulu yake nzi!

Huyaogopa maradhi, akawa kiguu na njia,
Mauti ikawa kazi,aliko kumkimbilia,
Lakini hana ujuzi, hutua panapotakiwa,
Uoza unachosifu, ni ikulu yake nzi!

Hushikwa kigugumizi, Ziraili akitua,
Akawa aomba radhi, hata kwa asiyoyajua,
Ulimi ukawa ndizi, mzito kuunyanyua,
Uoza unachosifu, ni ikulu yake nzi!

Anachoona azizi, ndicho kinachomuua,
Na aipandayo ngazi, juu hujamuengua,
Dunia hii malazi, makazi haikujaliwa,
Uoza unachosifu, ni ikulu yake nzi!

Na ukimuona nzi, kwenye mvi ametua,
Ndani nywele za nyuzi, vidonda vinachipua,
Na ubongo mfinyanzi, maji yeshakuingia,
Uoza unachosifu, ni ikulu yake nzi!

Nihifadhi ya Azizi, njia kunichagulia,
Hakunaye kiongozi, anayekutangulia,
Na wewe ni muokozi, ingawa wakukataa,
Uoza unachosifu, ni ikulu yake nzi!

Twafa mara mbilimbili

Haiwezi kuwa hoja, ila kwa walio dhalili,
Katika kufunga mkaja, mitihani hukabili,
Akili bure hufuja, panapohitaji musuli,
Twafa mara mbilimbili, nini kufa mara moja?

Watu hufa kwa kungoja, pamwe na ya leo hali,
Majuja na Maajija, nao hawatayahimili,
Vilemba nayo makoja, ya uongo si halali,
Twafa mara mbilimbili, nini kufa mara moja?

Watu hufa kwa kufuja, na wengine ubahili,
Mbinafsi wetu mja, na yake si ya wawili,
Anaikosa daraja, kwa kuwa ndumilakuwili,
Twafa mara mbilimbili, nini kufa mara moja?

Watu hufa kwa useja, na wengine wanawali,
Walafi wana mirija, tena miwili miwili,
Hufanza lisilo haja, wakaacha bilkuli,
Twafa mara mbilimbili, nini kufa mara moja?

Watu hufa kwa magonjwa, na wengine mankuli,
Wapo wapendao ganja, lakini hutupa wali,
Wanywao chupa moja, wengine kumi na mbili,
Twafa mara mbilimbili, nini kufa mara moja?

Wapo wasio faraja, misaada ni aghali,
Na wanaopiga mbinja, kwenye bohari ya mali,
Bahari yao kuvuja, huwa ni kitu muhali,
Twafa mara mbilimbili, nini kufa mara moja?

Haweshi wanaokuja, na kuondoka shughuli,
Kitamu anayeonja, huiogopa shubili,
Na kinyume cha mjanja, huwa mtu anzali,
Twafa mara mbilimbili, nini kufa mara moja?

Akujenge nani wewe

Maisha yake mafupi, mja katika dunia,
Na akili zake fupi, katika kufikiria,
Hajui katoka wapi, atang'ang'ania bua,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Hatari haiogopi, huogopa manufaa,
Akakamata makapi, na punje kuziachia,
Kwa udhia fotokopi, ibilisi amekua,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Kwa neema hanenepi, zaidi hukimbilia,
Augua yanguyapi, bidhaa hajaijua,
Na kwa ukweli haapi, shetani keshamwingia,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Nusura muda haipi, yake kuyapalilia,
Hali siku zake ngapi, hilo hajaling'amua,
Nahodha hamuogopi, ni yeye ajidhania,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Uwe ni ndugu wangapi, hali hawataijua,
Huhesabu mali ngapi, sikuhiyo zaingia,
Ukikopa hakukopi, haukopesheki baa,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Hawaniulizi vipi, twaweza kukusaidia,
Wangoja tangazo fupi, msibani kunijia,
Mauti huwa ni papi, nyumba zao hujengea,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Nimeandika kifupi, kwani nachanganyikiwa,
Nje hauvai chupi, ila ndani yavaliwa,
Na mengi kama makapi, huwezi kuongelea,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

Ndugu zangu siwatupi, ila sintowategemea,
Yamenishinda mangapi, nao wanaangalia,
Na wengine wako 'hepi', dhiki zikinifumua,
Akujenge nani wewe, aache jijenga yeye?

MALI

Ukombozi kuchelewa, bado hatujajikomboa,
Miaka ikiyoyomea, subira nayo hupaa,
Na juu wanaokua, kuamsha watakiwa,
Mali wanatuambia, a lutta continua!

Huwezi juu kukaa, na kisha ukashangaa,
Na akili kulemaa, ni lipi la kuamua,
Watu wanakungojea, si wewe kuwangojea,
Mali wanatuambia, a lutta continua!

Vinatakiwa vifaa, raia kuwapatia,
Kazi wakazitambua, na nchi kuendlea,
Zana zinapopunguwa, majungu mwajitakia,
Mali wanatuambia, a lutta continua!

Na wale wenye tamaa, nafasi waingojea,
Kwa klila anayesinzia, sharti kuchomolewa,
Ukiamka ukalia, watu hukupuuzia,
Mali wanatuambia, a lutta continua!

Kizingiti ukishakua, watu budi kukung'oa,
Ndivyo ilivyo dunia, hili huwezi kimbia,
Inafaa kuchukua, hatua zinazofaa,
Mali wanatuambia, a lutta continua!

Kila aliye na njaa, katu hawezi tulia,
Hadi tumbo likajaa, na kiu kujinasua,
Haya usipoyatambua, wengi watakusumbua,
Mali wanatuambia, a lutta continua!

Na viziwi wahofiwa, haya kutoyasikia,
Na vipofu nao pia, wenda hawatajionea,
Ila waliochaguliwa, katika siku radhia,
Mali wanatuambia, a lutta continua!

Mambo si kuyangojea, ila kuyafuatilia,
Na kisha kuyachungua, ukweli ukaujua,
Halafu kuazimia, hatua ukachukua,
Mali wanatuambia, a lutta continua!

Afrika inalia, njie tumeshapotea,
Wengi twaigilizia, asili twaiachia,
Nako tunakoelekea, siko tunakotakiwa,
Mali wanatuambia, a lutta continua!

Tabaka la watawala

Hujua wanayojua, ujinga wakaulea,
Mwana asiyejijua, mbeleko hatoachia,
Hubwebwa akanyamaa, taahira keshakua,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Mtawala hunyakua, kisicho chake kutwaa,
Kisha akagugumia, na mengine kuchukua,
Ikawa hajawaachia, akili ila udhia,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Na mchana huibiwa, jua linaangazia,
Kasumba wameshatiwa, sio wanaojijua,
Ikawa wanasifia, kikaango kilichokuwa,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Mafuta yanayotumiwa, wao kuwakaangia,
Ni yao yakamuliwa, kikaangoni kutiwa,
Na kisha huja kuliwa, kama wa bure dagaa,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Chini wanapoambiwa, kukaa wanatakiwa,
Hushindwa kuligundua, sio wa kuamriwa,
Ila wao watakiwa, amri kuja zitoa,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Wakubali kung'olewa, na wao ndio wa kung'oa,
Nafasi waiachia, wawezayo kutumia,
Usafi ukaingia, kila pembe, kila njia,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Rasilimali majuha, wadhani zimeumbiwa,
Wa juu waliokuwa, na sio wao raia,
Wakubwa wakawaachia, vipande kuvimegua,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Kura wanawaachia, wao wakasimamia,
Wakashindwa kutambua, ni wao wanaotakiwa,
Haki kuisimamia, na kuzuia kuibiwa,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Hukimbizwa kwa hatua, sungura ukadhania,
Kwa kuwa mbaya sheria, ukubwa haijaujua,
Na muda umeingia, hili kuliangalia,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Hupigwa kisha walia, kazi waliowapatia,
Wakashindwa kuelewa, kufukuza watakiwa,
Juu wao watakiwa, kila kitu kwangalia,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Wamelala wanaliwa, wasimama wavuliwa,
Watembea wategewa, wanyanyuka, wazuiwa,
Uchumi wamekalia, wajanja wawaachia,
Tabaka la watawala, lazidi kete watwana!

Mbona vyanzo viko vingi ?

SUBIRA huvuta kheri, nami ninangojea,
Nitakuwa ni msiri, ndarahima kunuia,
Vyombo kuvishauri, uchumi wapate jua,
Mbona vyanzo viko vingi, mwang'ang'ania vichache ?

Nangoja halmashauri, hodi kunipigia,
Niwape yangu khabari, nipate kuwastua,
Wakazigundua siri, uchumi wameketia,
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?

Haki kwavyo ving'amuzi

Wakubwa naulizia, vigezo walivyotumia,
Haki ya kutuuzia, ving'amuzi Tanzania,
Umma mmechukua, na walokole walokuwa?
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?

Madhehebu naulizia, zingine zilizokuwa,
Mbona hamkuchagua, au kweli wameishiwa,
RC na Islamiya, wameshindwa kulipia?
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?

Nao kina Ahmmadiya, na ina Ismailia?
Nako mashambani pia, vipi mtakufikia?
Za simu natarajia, kampuni zingefaa,
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?

Mitaji tukipatia, vijana wa Tanzania,
Tivii kujiundia, hivi hawataridhia?
Twendelee kununua, mapinduzi yeshaingia?
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?

Ajira twazililia, nyie mnaziachia?
Ipo teknolojia, Tivii kujiundia,
Mbona mnachelewa, au mmekusuidia?
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?

Masafa kutuchia, mikoa huru ikawa,
Hilo mmeshaamua, au amri mwangojea?
Karne imeshaingia, Tivii kukosa karaha,
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?

Na uhuru mwatakiwa, watu mkatuachia,
Nyie ni kusimamia, na si kutuingilia,
Ushauri nautoa, mwapaswa kufikiria,
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?

Wakimbia ushindani

Mbona mnavuta kamba, hamtaki ushindani,
Hivi sasa mnagomba, kwa kukosa ukinzani,
Nchi nzito kama mimba, hamtaki afueni?
Wakimbia ushindani, wataka ukiritimba ?

Mzigo mmeusomba, tena mwatia kichwani,
Njiani mwatoka shamba, letni niwabebeeni,
Kibaka mnanichamba, ni mwizi na mhuni?
Wakimbia ushindani, wataka ukiritimba ?

Ugonjwa umewakumba, kutokea viwandani,
Na sokoni mwauimba, na feri na mnadani,
Mmeshindwa kuimba, nyimbo ziko mkononi?
Wakimbia ushindani, wataka ukiritimba ?

Mnajipaka mavumba, samaki mwatupa chini ?
Heri mnayoikumba, mwasema si yenu thamani?
Mashavu yanawavimba, ibilisi mtadhani,
Wakimbia ushindani, wataka ukiritimba ?

Kicheko usichocheka

Hukuumiza moyoni, kicheko usichocheka,
Kichomi kiwe mbavuni, kifua kikateseka,
Raha uwe huioni, uzidi kukasirika,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Watu huwa mashakani, na shaka haijafika,
Sikuzote taabani, watakuja kudhurika,
Na wenye mali ndani, kuhofu wafilisika,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Wenye uzuri mwilini, wagwaya watachujuka,
Uzuri wakathamini,kuliko kilichowaweka,
Wakaishiwa imani,kwa sumu wakapambika,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Na wanaojiamini, akili zimepevuka,
Wakajiweka kundini, kwa akili kuhesabika,
Hawaishi tathmini, ya kama wanawehuka,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Wazima huwa shakani, maradhi yatawashika,
Ikawa zao mizani, riziki zinapimika,
Na mengine abadani, hawataki kuyashika,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Mtaji wanaoghani, miradi kukamilika,
Huyatafuta madeni, kichwani yakabebeka,
Hofu yao duniani, wasije kuanguka,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Mimi nimebaki ndani, shauri ninaliweka,
Namuachia Manani, hali yangu kutunzika,
Nangojea hisani, kulishwa na kunivika,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Nami naishika dini, nisome na kupambika,
Nipate kuwa kundini, wasomi wasioridhika,
Katika yake Qurani, kuijua na hakika,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Nataka ijenga dini, kwa ridhaa ya mhusika,
Ya Allah, biidhini, ninaiomba hakika,
Na Maashallah mwakani, nimalize robo njia,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Nautafuta utani, utakaostahika,
Nimchekeshe Mughni, na wengine kadhalika,
Maisha yawe laini, tena pasi kusumbuka,
Kicheko usichocheka, hukuumiza moyoni!

Umfaaye hakufai

FAA unaowafaa, usingoje shukrani,
Hilo halitatotkea, sembuse wakuthamini?
Watu wapenda pokea, kutoa kwao mtihani,
Umfaaye hakufai, kwenye dhiki hukimbia !

Unapowasaidia, tia uko hasarani,
Kwa kipimo kutumia, chake hapa duniani,
Ila kwako hii njia, kuelekea maskani,
Umfaaye hakufai, kwenye dhiki hukimbia !

Tenda kama hujajua, tena halina thamani,
Na mtu kutoangalia, alivyokuwa usoni,
Shukrani akitoa, mwambie ampe Manani,
Umfaaye hakufai, kwenye dhiki hukimbia !

Watu ni kuwavumilia, ili usiwe shakani,
Wakwambiacho sikia, kufanya kitu imani,
Uwape nacho ukiwa, sio chako cha rehani,
Umfaaye hakufai, kwenye dhiki hukimbia !

Usije ukawatia, katika hiyo mizani,
Wa kweli waliokuwa, na waongo nukstani,
Mola ungemwachia, huwa ni kubwa hisani,
Umfaaye hakufai, kwenye dhiki hukimbia !

Usinune kujikwaa, pasiwe mwenye imani,
Juu akakunyanyua, akakuweka kitini,
Shukuru unachopewa, mengineyo ni ihsani,
Umfaaye hakufai, kwenye dhiki hukimbia !

Mbele ukiangalia, usije fika mwakani,
Kwanza toa inshallah, na hedaya ithamini,
Kinachowahi hutua, kabla kufika chini,
Umfaaye hakufai, kwenye dhiki hukimbia !

Moyo wako achilia, mshukuru na Bathini,
Hatua uliyofikia, hakika sio thakini,
Zaidi unachopewa, ungemuachia Manani,
Umfaaye hakufai, kwenye dhiki hukimbia !

Wanaonunuliwa

Vibarakala si jana, ndipo walipoanzia,
Hawa ni yetu amana, huifuata dunia,
Kazi yao ni utwana, mabwana kutumikia:
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Kwenye redio wajaa, huru na zinazotumiwa,
Kazi yao kutumiwa, uongo waupakua,
Matunda yake twajua, Rwanda tulijionea,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Magazeti nayo pia, wengi wananunuliwa,
Huajiri changudoa, ili mradi kuwafaa,
Malengo yakatimia, bei rahisi ikawa,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Huandika yasokuwa, wakaacha yalokuwa,
Vigumu kununuliwa, ila ruzuku huvua,
Samaki uozo hua, kutupwa wakiamkia,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Televisheni kwingia, haraka wazikimbilia,
Kinyaa waliokuwa, marashi kujipakaa,
Na udi kujitia,ubani kuvukizia,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Uoza ukishakuwa, vigumu ukarejaea,
Freshi haijakuwa, na wala haitakuwa,
Uoza ukishakua, hivyohivyo hubakia,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Labda ukishakaukia, harufu kutoitoa,
Kunuka kukapungua, vumbi ukishakuwa,
Watu kuvumilia, japo asili wajua,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Haramu ilokuwa, halali haitokuwa,
Na wanaonunuliwa, watakiwa kujijua,
Si kwa yangu manufaa, ila moto kukimbia,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Roho wanapokutoa, haya utajionea,
Ziraili hukujia, usoni ana ghasia,
Ulikuwa ni udhia, naye anakuchukia,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Kuumbwa akujutia, ewe mwanaizaya,
Mwingine angezaliwa, watu angeliwafaa,
Busati umetumiwa, viatu kuvifutia?
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!


Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Kwa hasira hukutoa, hiyo roho yako mbaya,
Na hata ukijutia, motoni unaingia,
Naye huchekelea, sawasawa imekua,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Hili sijashabikia, wanangu ninawambia,
Mwataklwa kujikomboa, muache kuwa malaya,
Itawaghasi dunia, na akhera kuumia,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

Usia nimeshatoa, babu sasa nimekua,
Vipofu wasiokua, haya watajionea,
Na viziwi watapewa, ishara wakalijua,
Kila anayetumiwa, kwa hiari yake mwenyewe,
Moto anauchochea
Hawezi kusamehewa
Nadra ataombewa
Hata na anayemtumia
Jehanamu huingia!

SI NCHI YA KUFANIKIWA!

Nje wanakimbilia, kwa hao wenye ulaji,
Huku wajititimua, wenda kusaka mitaji,
Kumbe wanang'ang'ania, kuujenga uhitaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Uongo waliojaa, viongozi na walaji,
Kiburi wakajitia, wajione wajuaji,
Raia huwaumbua, mithili wakeketaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Wanaokosa ulua, wakajaa ufujaji,
Fedha wakazitumia, ukata uwe wahiji,
Mola hatowaridhia, hata ikiwa Miraji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Wajuao kutumia, ila sio upataji,
Nchi huwa wanaua, nao ni wauaji,
Polepole inakuwa, lakini ni mauaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Na chama kilichojaa, watu wababaihsaji,
Kazi kwake ni kulea, taifa la wahitaji,
Ombaomba walokuwa, kwa njaa na upataji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Viongozi wenye njaa, hufata wanunuaji,
Wakauza visokuwa, hata pia na mitaji,
Muda wote hulaaniwa, hawawi wafufuaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Uongo ukienea, hakuna usahihishaji,
Kila pembe huingia, panya kwenye mifereji,
Mchana huko hukaa, na usiku watokaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Hata paka wakitua, hushindwa ukamataji,
Maana hununuliwa, wakawa si wa kuchaji,
Kulamba wakaishia, wanaopewa ulaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Kisa demokrasia, bado tunaihitaji,
Mbali iliyoenea, katika uchaguaji,
Uoza kuundoa, kwa kuwa wasafishaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Nguvu kinapoachiwa, chama kimoja ulaji,
Wananchi wataumia, hakuna wa kuwafariji,
Nguvu sawia zikiwa, hapo kuna uponaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Bunge linatakiwa, bila wachakachuaji,
Na idadi sawa kuwa, kwa wote wagombeaji,
Ikilazimu ikawa, mseto kwa uundaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Ushindani maridhia, jambo la uiokoaji,
Mabaya hufichua, hakuna cha uzikaji,
Watu wawe kidedea, kuwafuta wajuaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Watu wawe kidedea, kuwafuta wajuaji,
Kwa chama kisichotakiwa, kukataliwa ulaji,
Nje wakaondolewa, wabakie watakiwaji,
Watu wawe kidedea, kuwafuta wajuaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Katiba inatakiwa, wananchi wawe majaji,
UUoza kuuondoa, kila wanapohitaji,
Na wala si kuzuiwa, na sheria za wafujaji,
Watu wawe kidedea, kuwafuta wajuaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Raia wanatakiwa, wasiwe wasindikizaji,
Kila kitu kufuatia, na maamuzi kuhoji,
Kikiwa kisichokuwa, pawe na uwajibikaji,
Ndani isoangalia, si nchi ya kufanikiwa!

Kiongozi bandia

Kiongozi wa sumaku, anaweza kutulia,
Huvutwa huku na huku, nani wa kumshikilia,
Huwa kama vile kuku, mtama anayemwagiwa,
Na kiongozi bandia, hujaliwa itihari ?

Husikiza mamluku, uongo akavamia,
Akaifanya shauku, isivyo akaamua,
Na akangalia huku, mkuku wakatokea,
Na kiongozi bandia, hujaliwa itihari ?

Huwa achezeshwa zuku, sindima wakachagua,
Huja nyuma zake siku, kila leo kuchelewa,
Hana analolishuku, kila kitu hufanziwa,
Na kiongozi bandia, hujaliwa itihari ?

Hawezi kutabaruku, diniye anaigwaya,
Watu humpiga chuku, adhani wamshangilia,
Ukija mtafaruku, mwenyewe huja bakia,
Na kiongozi bandia, hujaliwa itihari ?

Huwa mwingi wa shauku, na machache hutimia,
Ahadi zake ni buku, mfukoni ana mia,
Yanavyozidi masiku, utapeli uhofiwa,
Na kiongozi bandia, hujaliwa itihari ?

Haishi bila ruzuku, inayotoka kubaya,
Na barua za udaku, nyuma huwa zafatia,
Japo anakula kuku, tembele hufurahia,
Na kiongozi bandia, hujaliwa itihari ?

Na akiwa na kasuku. upuuzi ataongea,
Hata yalo marufuku, watu atawaachia,
Haya huja kumpiku, hatimaye huzidiwa,
Na kiongozi bandia, hujaliwa itihari ?

Maisha si sikukuu, ila kwa waliopagawa,
Yako kama yako huku, mkenge umashaingia,
Na kisha siku ya siku, hatia ni kutumiwa,
Na kiongozi bandia, hujaliwa itihari ?

Uongozi kudhibiti

Uongozi kizingiti, ndani unajifukia,
Hahujui wakati, wala yanayotokea,
Husiikiliza pointi, ovyo zilizonukuliwa,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Hupewa kisicho nati, na kisha kikaachia,
Haufanywi utafiti, kwenye giza hubakia,
Na kusaoma magazeti, ni wavivu walokuwa,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Tivii nazo wavuti, husakura kwa kinyaa,
Wataka kitu smati, ndani kipate tulia,
Hakuna tena wakati, ya zamani kurudia,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Redio hawazifati, wajinga huwaachia,
Huwasoma Muqsiti, akayafanza sawia,
Baina kati kwa kati, huja wakatumbukia,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Huwajaza Muqliti, hekima watarajiwa,
Na siku yao umati, juu huja wanyanyua,
Tena bila masharti, mtu aliyeyatoa,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Nchi yatakiwa chati, na miundo kutumia,
Ikawa jambo hukuti, mtu lisilopangiwa,
Kila kitu kwa wakati, kikawa chahudumiwa,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Taifa lataka dhati, kila kitu kufuatia,
IKawa hakuna kiti,kisichokupekuliwa,
Na zikatoka ripoti, yafaa au kutofaa,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Nchi haifurukuti, bila ya kusimamiwa,
wako watu kama nati, lazima kufunguliwa,
Kisha kubanwa kwa kati, hapo hapo kutulia,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Wapo wasio nishati, vigumu kwenda sogea,
Wataka pigwa mabuti, watoke walipokaa,
Na wengine kama sleti, kazi ni kuandikiwa,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Upo wa gari na wa jeti, mnapaswa kuchagua,
Upo ujuzi na cheti, na vyote haviwi sawa,
Na uhai na mauti, mwaweza hayo chagua,
Uongozi kudhibiti, na sio kudhibitiwa!

Watu unawakosea, ukiwafanya wajinga !

Akili kweli ni nywele, kila mtu ana zake,
Hata awe mwenye ndwele, yeye pia ana yake,
Huwezi mfanza mchele, akili usojaliwa,
Ukiwafanya wajinga, watu unawakosea!

Wengine kama mshale, na mkuki ueleke,
Yao mbele kwa mbele, kusaka chao wateke,
Hawataki misukule, na yao yaje yazikwe,
Ukiwafanya wajinga, watu unawakosea!

Si ya leo ni ya kale, na taji lao wavike,
Niliona ya Kaole, wala mbali msifike,
Mtu kuchanjwa chale, sio tu asilogeke,
Ukiwafanya wajinga, watu unawakosea!

Mtu kuchanjwa chale, sio tu asilogeke,
Wengine hufanya vile, washika wasimshike,
Na wengine mkalole, hupanga mbali wafike,
Ukiwafanya wajinga, watu unawakosea!

Ila kuishi milele, vigumu likubalike,
Sio leo toka kale, kila jambo na miko yake,
Na chunusi si upele, japo zote zikunike,
Ukiwafanya wajinga, watu unawakosea!

Si mtu wa makelele, ya kwangu yaimbike,
Napenda vigelegele, ila si vyenye makeke,
Inanibana tungule, kwenye chakula usiweke,
Ukiwafanya wajinga, watu unawakosea!

Uzee hauwi dawa

Kama sio majaliwa, uzee hauwi dawa,
Kila unavyojongea, huzidi uoza kuwa,
Tabia ikawa mbaya, na kwa wengine kinaya,
Uzee hauwi dawa, ikesha tabia mbaya!

Huongezeka tamaa, dhambi ukanyemelea,
Dhuluma ukachagua, na vitoto kuvizia,
Mvi japo zakujaa, huna aibu wala haya,
Uzee hauwi dawa, tamaa kuja pungua?

Uongo utauzua, mkeo ukamwambia,
Na watoto kudoea, chumo likikulemea,
Ukweli huukimbia, motoni kukimbilia,
Uzee hauwi dawa, uongo kuukataa !

Dini wasioijua, mikongojo watumia,
Hushindwa kumrejea, Mola anayewangojea,
Wakawa wanakimbilia, bado ya kwenye dunia,
Uzee hauwi dawa, Rabana kumrejea !

Na wenye tabia mbaya, kama wameshalaaniwa,
Hulka huendelea, h ata uzee kwingia,
Huwezi kumuongoa, silo alilopangiwa,
Uzee hauwi dawa, ikesha tabia mbaya!

Wapo wanaojitia, ujana waendelea,
Mambo wakajifanyia, ya kuchukiza raia,
Nishai wakawatoa, na heshima kupungua,
Uzee hauwi dawa, tamaa kuja pungua?

Waliokuwa wambeya, humazah huchimbua,
Ukubwani kuugua, na hasa ugonjwa ukawa,
Kila wataloongea, si lingine ni umbeya,
Uzee hauwi dawa, umbeyakuukataa !

Watu wakubwa wakiwa, huangamia dunia,
Kama wale wa Ulaya, nako Amerika pia,
Vizazi vyaumbuliwa, kwa umbeya kuzagaa,
Uzee hauwi dawa, Rabana kumrejea !

Wakubwa si malaika

ZAMANI kuna hadaa, sinema iliyokuwa,
Wakubwa tulidhania, watu wema wanakua,
Watukufu tukajua, hata kuwasujudia,
Wakubwa si malaika, uongo usikubali!

Hasa wanaotumiwa, watu kuwanyanyapaa,
Uroho waliojaa, ukubwa kujilimbikia,
Na uchu kuupakua, mlo wote kujilia,
Wakubwa si malaika, uongo usikubali!

Kuna wakubwa balaa, wizi wamejisomea,
Huwaibia raia, fukara wazidi kuwa,
Wakadhani mashujaa, kumbe ni tupu fedheha,
Wakubwa si malaika, uongo usikubali!

Kura zikihesabiwa, mabingwa wa kuhadaa,
Yao kwao hujipangia, hadi washindi wakawa,
Mate anawatemea, Mola akiangalia,
Wakubwa si malaika, uongo usikubali!

Waongo pia wajaa, Afrika nawambia,
Na dhambi huwarudia, kwa wengine kusingizia,
Mola hawajamjua, hatoweza kusinzia,
Wakubwa si malaika, uongo usikubali!

Katiba huwaibia, wamiliki walokuwa,
Ujivuni kujitia, na ujibari kuvaa,
Shahidi ashuhudia, kiyama chawangojea,
Wakubwa si malaika, uongo usikubali!

Wapo wanaong'aa, mchana unapokuwa,
Usiku ukiingia, mashetani wanakuwa,
Free Masons mwajua, jina wameshagaiwa,
Wakubwa si malaika, wengine ngono tabia!

Ziara zinatumiwa, uchafu kujifanyia,
Huzungukwa na zinaa, kila njia ya hatua,
Malaika humkimbia, baharini kwenda kaa,
Wakubwa si malaika, wengine mashoga pia!

Hawana la kuhofia, kaumu Lutu ikiwa,
Wachache waliokuwa, yao hujizawadia,
Ila nchi hulaaniwa, ikaja kuadhibiwa,
Wakubwa si malaika, wengine ni wasagaji!

Kalakhi twakuangukia, inusuru Tanzania,
Cha kufanya wakijua, hatuna tunalojua,
Salama tunaililia, wakiwa tuliokuwa,
Wakubwa si malaika, wengine kumbe waovu!

Jenereta

MRADI uliobakia, kuuza majeneereata,
Rahisi kuyanunua, na kuongeza ukata,
Watu wakiwa na njaa, lazima watatufuata:
Mradi wa jenereta, unakua Tanzania:
Hao waliouleta,
Wanaongeza ukata,
Laana zetu wapata,
Yajewachoma mafuta,
Ambayo wayatumia!

Hatuogopwi kusutwa, hadaa kwetu tabia,
Pindi tunapotafuta, ncha butu kwetu huwa,
Usiku twameremeta, hata nyota kuzidia,
Mradi wa jenereta, unakua Tanzania:
Hao waliouleta,
Wanaongeza ukata,
Laana zetu wapata,
Yajewachoma mafuta,
Ambayo wayatumia!

Unapozidi ukata, hata ngebe huibua,
Chuma ulete twateta, budi kuiganga njaa,
Ushindi tusipopata, riziki itapotea,
Mradi wa jenereta, unakua Tanzania:
Hao waliouleta,
Wanaongeza ukata,
Laana zetu wapata,
Yajewachoma mafuta,
Ambayo wayatumia!

Hununua jenereta, wenyewe kujiuzia,
Haiwi kwetu sakata, mipango twajisukia,
Huwaondoa vimeta, pindi wakiingia,
Mradi wa jenereta, unakua Tanzania:
Hao waliouleta,
Wanaongeza ukata,
Laana zetu wapata,
Yajewachoma mafuta,
Ambayo wayatumia!

Sisi nani kujaleta, ustawi Tanzania,
Wakati kwetu ukuta, nasi twajitafutia,
Kukosa sio kupata, hatutaki nyeng'enyea,
Mradi wa jenereta, unakua Tanzania:
Hao waliouleta,
Wanaongeza ukata,
Laana zetu wapata,
Yajewachoma mafuta,
Ambayo wayatumia!

Hebu lete kalkuleta, hesabu kukokotoa,
Hadi mwaka ukipita, bilionea nimekua,
Huwezi nyuma nivuta, ufukura nakimbia,
Mradi wa jenereta, unakua Tanzania:
Hao waliouleta,
Wanaongeza ukata,
Laana zetu wapata,
Yajewachoma mafuta,
Ambayo wayatumia!

Nchi nitaikokota, ipate kuendelea?
Nache wengine kupata, mimi nife kwa njaa?
Utu huo nakeketa, siwezi ukubalia,
Mradi wa jenereta, unakua Tanzania:
Hao waliouleta,
Wanaongeza ukata,
Laana zetu wapata,
Yajewachoma mafuta,
Ambayo wayatumia!

Zachanua jenereta, hapa kwetu Tanzania,
Kelele zinazoleta, na hewa kuichafua,
Mradi sisi twapata, haya tunavumilia,
Mradi wa jenereta, unakua Tanzania:
Hao waliouleta,
Wanaongeza ukata,
Laana zetu wapata,
Yajewachoma mafuta,
Ambayo wayatumia!

Jenereta, jenereta, huree Watanzania,
Ukikosa utaokota, nafuu bei ikiwa,
Usiyahofu mafuta, karibu tutajichimbia,
Mradi wa jenereta, unakua Tanzania:
Hao waliouleta,
Wanaongeza ukata,
Laana zetu wapata,
Yajewachoma mafuta,
Ambayo wayatumia!

Monday, March 26, 2012

Kushangaa si vibaya

Binadamu yake hulka, mapya kuyashangaa,
Likisha kufahamika, kawaida linakuwa,
Kisha hudharaulika, likaacha kujaliwa,
Kushangaa si vibaya, ubaya kuyaharibu!

Ubaya wenye hakika, kupuuza yalokuwa,
Yakaacha kujengeka, uzee yakaingia,
Yawe yasahaulka, na kaburi kuchimbiwa,
Kushangaa si vibaya, ubaya kuyaharibu!

Reli zilishajengeka, wakati tunashangaa,
Uhuru tukaushika, wa bendera kupepea,
Na leo zinameguka, uzee zimeshaingia,
Kushangaa si vibaya, ubaya kuyaharibu!

Vipi zilisahaulika, kosa letu kushangaa,
Hazikukarabatika, ovyo tukaziachia,
Na sasa twashtukia, zapaswa kujengwa upya,
Kushangaa si vibaya, ubaya kuyaharibu!

Barabara zajengeka, nadra kuangalia,
Akili zimeteguka, hatujui fatilia,
Kila kitu chafanyika, kama vile hai chawa,
Kushangaa si vibaya, ubaya kuyaharibu!

Nani wa kuangalia, waziri hajamjua,
Kama ameshamjua, hajui fuatilia,
Mikenge tunaingia, nchi yazidi lemaa,
Kushangaa si vibaya, ubaya kuyaharibu!

Visima vinachimbika, hakuna kuangalia,
Hadi vaja kubomoka, hakuna anayejua,
Na shule zinajengeka, udhaifu ziliizojaa,
Kushangaa si vibaya, ubaya kuyaharibu!

Na shule zinajengeka, udhaifu ziliizojaa,
Wajenzi wanaumbuka, mabomu zikizinduliwa,
Wenyewe wastahika, na wakubwa wahamiwa,
Kushangaa si vibaya, ubaya kuyaharibu!

Radhi asiyekuomba

MUNGWANA akikosea, mwepesi kujikosoa,
Kitu anajidhania, na ubora kajitia,
Vyema kumuangalia, mwalimu wake dunia,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Yeye anakukosea, ujeuri ajitia,
Kisha akunyanyapaa, mithili una hatia,
Kwa dharau ashupaa, na vijembe kuvitia,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Shetani keshamwingia, moto kamzawadia,
Damu inamchochea, na hasira kumjaa,
Ubaya afrikira, anapokuangalia,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Unafiki amejaa, nje awachangamkia,
Na umbeya augawa, kusema ameonewa,
Ukweli wanaojua, haweshi kumshangaa,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Ukweli huukimbia, uongo kushikilia,
La ajabu hurudia, kama anakutania,
Kimya budi kukaa, iko siku atavia,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Mjinga hukudhania, unavyomvumilia,
Siri hajaitang'amua, bado anakuchezea,
Mwenye imani hujua, na subira huwania,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Naye huzidi mwombea, amnusuru Jalia,
Hisani humfanyia, japa hayawani kawa,
Nafsi huililia, shetani kumuingia,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Mengi huyafikiria, mazuri yaliyokuwa,
Wana kutowasumbua, ambao hawajakuwa,
Muda akajiwekea, wana wapate kukua,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Ahali huzingatia, yao wote majaliwa,
Ukweli akiujua, hupuuza yalokuwa,
Moja akaliangalia, la wote linalowafaa,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Mhanga hujitolea, au kafara akawa,
Bora apare kuzua, nusura ikawafaa,
Na wanaojitambua, ukweli wakaujua,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Mwisho nimeshafikia, kalamu naiachia,
Heri wanaosikia, uzima watajaliwa,
Ole wao wasojua, mauti yawavizia,
Radhi asiyekuomba, dharau huyo kajaa.

Nchi inao wenyewe

Nasi tumewasikia, kwa siri wayasemayo,
Nchi waishikilia, hakunao wengineo,
Hawawezi iachia, mbwa watawale wao,
Nchi inao wenyewe, sisi tukae pembeni:
Ndivyo wasemavyo wao!

Haraka waliamua, lao kuwa ni chaguo,
Macho walipofungua, walopewa ufunuo,
Ukweli wameujua, kwa Mola ni marejeo,
Nchi inao wenyewe, sisi tukae pembeni:
Ndivyo wasemavyo wao!

Dhambi ukiitumia, matunda yake ni hayo,
Uoza ukiingia, samaki wote si zao,
Na uongo ukishakua, baraka si tena yao,
Nchi inao wenyewe, sisi tukae pembeni:
Ndivyo wasemavyo wao!

Ujanja watatumia, ila ovyo mwendo wao,
Hakuna lakuchanua, hunywea maua yao,
Rangi waweza jipakaa, chakavu majengo yao,
Nchi inao wenyewe, sisi tukae pembeni:
Ndivyo wasemavyo wao!

Afu keshawakimbia, kwa hivyo vituko vyao,
Na wakiziomba dua, madogo mapato yao,
Jalia huwajalia, ukweli wauuchao,
Nchi inao wenyewe, sisi tukae pembeni:
Ndivyo wasemavyo wao!

Walizojilundikia, huliwa na mchwa wao,
Mikosi nayo balaa, ikaribu na wao,
Marashi wakijipakaa, bado uvundo wanao,
Nchi inao wenyewe, sisi tukae pembeni:
Ndivyo wasemavyo wao!

Dhuluma yawaumbua, kwa kuwatenga wenzao,
Vyote wanagugumia, hakuna libakiayo,
Usoro wapalilia, heshima si tena yao,
Nchi inao wenyewe, sisi tukae pembeni:
Ndivyo wasemavyo wao!

Ndiye unayechagua, viongozi wetu hao,
Dhambi tumekufanyia, ni zawadi tupewayo,
Ghali sana imekua, sasa budi marejeo,
Nchi inao wenyewe, sisi tukae pembeni:
Ndivyo wasemavyo wao!

Mwiba ng'ombe au yai

Taarifa zaingia, uwizi umefanyika,
Kituoni naingia, zamu yangu kuishika,
Faili nimeletewa, notisi imeandikwa,
Mwiba ng'ombe au yai, nani ni jambazi wa kweli ?

Mkubwa kashikwa wizi, ng'ombe wa mtu kateka,
Walofanya fumanizi, kwao sasa ni mateka,
Wanangoja maamuzi, polisi twende mdaka,
Mwiba ng'ombe au yai, nani ni jambazi wa kweli ?

Kisha eti kuna mwizi, yai moja kalipoka,
Tena kaiba majuzi, mwibiwa hana hakika,
Hana habari dokozi, kama alikwishapoka,
Mwiba ng'ombe au yai, nani ni jambazi wa kweli ?

Duni vifaa vya kazi, kituo chafilisika,
Natakiwa maamuzi, mara moja kufanyika,
Bodaboda ya makzi, ipate kwenda tumika,
Mwiba ng'ombe au yai, nani ni jambazi wa kweli ?

Nikaamua upuuzi, kesi ya yai yafutika,
Koplo kumpa kazi, mkubwa kwend a kumshika,
Mara simu fululizi, zasema siwezi mshika,
Mwiba ng'ombe au yai, nani ni jambazi wa kweli ?

Nikafanya ugunduzi, koplo kumbe atumika,
Mkubwa kampa kazi, nami kushughulika,
Amri kaweka wazi, bosiwe kaelimika,
Mwiba ng'ombe au yai, nani ni jambazi wa kweli ?


Kuuliza siliwezi, neno limegundulika,
Kumbe kuna wengine wezi, kamwe huwezi washika,
Hawa ni wa ndani wezi, daima wanalindika,
Mwiba ng'ombe au yai, nani ni jambazi wa kweli ?

Iko aiku mtaingia

Kidela kasimulia, simulizi kazishika,
Kichwa anaugulia, kawachokoza mzuka,
Sasa wanahadithia, ibura zinazozuka,
Iko aiku mtaingia, kutoka sintowaachia!

Ajua wanaojua, hata kwao keshafika,
Ni watu wa kutangulia, japo sio wa kufika,
Mwendo wao kutembea, kitako hakijakalika,
Iko aiku mtaingia, kutoka sintowaachia!

Msongo umeshapaa, mhemuko wa mzuka,
Juu mtu ahemea, ataka kupumzika,
Kivuli kakusudia, wanakataa mzuka,
Iko aiku mtaingia, kutoka sintowaachia!

Miye hubaki kucheka, ni wasioelekeka,
Mbuyu wauparamia, ujuha unaofanyika,
Hali walishatakiwa, mbuyu kuuzunguka,
Iko aiku mtaingia, kutoka sintowaachia!

Acha kuyafikiria, ya karibu kufanyika,
Macho ukifungua, mbali utatahadharika,
Kujenga asiyepewa, utamlaumu kubomoka?

Ngazi inayotitia, walaumu kuporomoka?
Na juu wanaokuwa, wajua chini watafika?
Kaa juu shikilia, mimi na yangu naondoka,
Iko aiku mtaingia, kutoka sintowaachia!

Upambe naukataa, fikra nitazitoa,
Mtu ukimtumia, wengine kudhulumika,
Hakika mwenye hatia, hubaki ni mhusika,
Iko aiku mtaingia, kutoka sintowaachia!

Kigingi kimebakia, kisiki hutoepuka,
Mbona ningeshachukua, ningehitaji miliki,
Kunyonya sikuzoea, wala sinayo ashiki,
Iko aiku mtaingia, kutoka sintowaachia!

Hapahapa nabakia, fikra kugawanyika,
Chema nikatumikia, na bora kujazalika,
Hadithi kusimulia, kizazi kisicho shaka,
Iko aiku mtaingia, kutoka sintowaachia!

Mguu mmekosea

Wenzangu nawausia, marafiki kuchagua,
Wapo tunaowajua, utumwa walitutia,
Na ubaguzi wajaa, kwao bado ni kadhia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Historia twaijua, milango twawaachia,
Na bado twajionea, waipondavyo dunia,
Askari wamekuwa, ukubwa wameukwaa,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Yao yanadidimia, nini watatupatia,
Ila kondomu kupewa, tena zilizochakaa,
Na za bure chandalau, eti dawa ya malaria,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Unafiki twajitia, hawa kuwavumilia,
Mugabe namchukia, ila kwa hili radhia,
Mashariki inafaa, sote tuanze elekea,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Nchi wanaigawa, ubaguzi warejea,
Elimu yao yapwaya, uhuni umeingia,
Na fedha zimepungua, raha zao ni karaha,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Wameacha mhofia, mmiliki wa dunia,
Ya watu yawazuzua, Usodoma waridhia,
Rafiki nao tukiwa, dhambi tunajibebea,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Watu ovyo wanaua, na sisi wao wabia?
Mola kumuhofia, wenzangu nawaambia,
Dhulumati hana njia, akhera nayo dunia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Najua mwanichukia, ukweli ninapotoa,
Manjumati mmepewa, na makombo mwatumia,
Hayo yenu yawafaa, na sio sisi raia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Utumwa mnatutia, kulekule mwarejea,
Ardhi mwagaiwa, bure vito kuchukua,
Pipi mkishazipewa, hayo yote mwaridhia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Shahidi historia, itakavyowaumbua,
Dhalimu tutawajua, rahisi wanunuliwa,
Laana kuwaachia, wao na kizazi pia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Yarabi twakuangukia, zahama kuiondoa,
Mapema itavyokuwa, kadri ukikadiria,
Nchi isije ungua, na watu kuteketea,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Mzungu akikujua

Hiy9 ni yake tabia, toka alipozaliwa,
Watumwa huwatumia, ya kwake wakamfaa,
Kaigeuza dunia, tambaa kujifutia,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Nasaba walozaliwa, watumwa waliokuwa,
Kasumba inakolea, vigumu kuwaondoa,
Bado wanyenyekea, mweupe kumtegemea,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Huwapuuza wazawa, na tena wakawagawa,
Nchi wakaachia, wazungu wasiojua,
Na tenda wakazitoa, kwa zuzu nao majuha,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Wanachofuatilia, pasenti wanayopewa,
Mengine kwao udhia, nchi hii yawapwaya,
Benki wakizichukua, Ulaya wanahamia,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Wana huwagharamia, elimu ya kujijua,
Waende kutojijua, na kurudi wasiojua,
Na urithi huachiwa, na wafalme walokuwa,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Sinema za Kinigeria, hili zinalitambua,
Ona shere kuchezewa, mweusi anavyotanua,
HJku njaa wajifia, ndugu zao walokuwa,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Ni Urussi iliyokuwa, na sasa yamerudia,
Wafalme watumia, raia wararuliwa,
Ufaransa nako pia, hadi mapinduzi kuwa,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Afrika yalemaa, kwa mbeleko ya Ulaya,
Na kila mwenye kujua, hili atalikataa,
Vijana ninawaambia, msije mkachelewa,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Sanaa watuulia, sasa nyani tumekua,
Twaiga yasiyokuwa, na tena yasiyofaa,
Weusi hautakuwa, weupe ninawaambia:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Lugha wanatuulia, na elimu kudidimia,
Watoto twawaonea, Kiingereza kutumia,
Kusoma sio kujua, lugha ya mama si bia,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Lugha ni kujisomea, nyingi tu ukazijua,
Maabara zatumiwa, sayansi na teknolojia,
Miezi haba yafaa, hata mbili ukajua:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Mashariki twatakiwa, tuanze kueleka,
Kichina tukakijua, nacho pia Kimalaysia,
Kadhalika na India, Gujarati kuongea:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!


Ila kwa kufundishia, ni ya mama kutumia,
Rohoni inaingia, na vitu vingi kujua,
Moyoni hukubaliwa, kama mbegu vikakua:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Ninamuomba Jalia, nusura kutupatia,
Kutoa wanaosinzia, tupate wanaozua,
Bure tunayoyaua, na wenyewe kujifia:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Kinyesi njiani.....

UTUSANI natumia, tena kwa kukusudia,
Vipofu waliokuwa, pengine watajizomea,
Uvivu wakiachia, matatizo wakajua,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Kipato mwakusudia, kua au kupungua?
Wasafi msipokuwa, ndoto yenu itakuwa,
Maneno mwajivunia, vitendo vimepotea?
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Hoteli zanyanyuliwa, ni uyoga zimekua,
Pembeni ukisogea, kinyesi kinaelea,
Mzungu katumbukia, na laana kaitoa,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Hamkioni kinyaa, wakubwa mlokuwa,
Ulaya mnaingia, ya kwao mwajionea,
Hivi ndivyo inavyokua, au mmepungukiwa?
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Njia kunao udhia, nao pia wa kinyaa,
Huwezi ijua njia, kila pembe yatumiwa,
Pikipiki zashtua, hujui zinakotokea,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Kama kinyesi balaa, na bajaji nazo pia,
Popote hujipitia, hata za miguu njia,
Hatuioni sheria, mitaa yetu nazaa,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Madiwani watumbua, enzi wameshaipewa,
Kazi yao kupokea na si haki kutoa,
Wepesi wa kuchukua, sio wa kuangalia,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Ukubwa ukililia,jua ni kutumikia,
Wakubwa walokuwa, wataka kutumikia,
Sultani wamekua, chini hawatatembea,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Ya kwao si ya raia, wanao wa kutumiwa,
Watu wa kuagiziwa, utumwa walojitia,
Hawajengi, wabomoa, sasa tunajionea,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Ingekuwa uranium ?

Watu chini huanzia, sio juu hutokea,
Msingi usipokuwa, jengo halitobakia,
Tsunami ikiingia, hakuna cha kubakia,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Kuzuri kulikokuwa, wa juu wankokaa,
Makwetu huku udhia, wa kawaida raia,
Uwekezaji wavia, heshima imepungua,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Watalii twalilia, twakosa hata maua ?
Bustani zapotea, ya ikulu yabakia,
Muhimu kujishangaa, udhia tulivyokuwa,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Watu viguu na njia, nini kitaangaliwa?
Muda wazidi potea, viraka tumebakia,
Mahandaki yamekuwa, njia katika mitaa,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Mlo juu mwatakiwa, haya kuja jionea,
Kwa miguu kutembea, mpate wetu udhia,
Labda mtafikiria, makwenu mkirejea,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Mabasi yetu balaa, TB yatutishia,
Abiria wanavyojaa, kwambukizana si nia,
Ila nchi yatuachia, wenyewe kuteketea,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Muhimbili wasifiwa, mbu wamezawadiwa,
Ni wakubwa walokuwa, utandawazi waingia,
Kimataifa wadaiwa, hadhi waweza chukua,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Vipofu tumeshakuwa, hatuuoni udhia,
Viziwi wa kusikia, ukweli twaukataa,
Husema tusiyojua, twaacha tunayojua,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Bila ya kutengemaa, ya chini yalokuwa,
Usia nawaachia, wana mwaja kuwaua,
Na hukumu zatakiwa, toka sasa kwandaliwa,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Mashahidi mashairi

Mashahidi ushairi, Yarabi ndiyo dhamiri,
Inshallah kujiri, kwa yako hiyo kadiri,
Sitaki umashuhuri, nataka yako akheri,
Mashahidi mashairi, kwa vizazi vya akheri!

Mengine ninaghairi, ila yako wewe kheri,
Ni hadhari, ni khabiri, siwezi fanya jeuri,
Ni mchache wa kiburi, wala sina ujibari,
Mashahidi mashairi, kwa vizazi vya akheri!

Ushahidi nahadhiri, kwa yako kubwa fahari,
Yajaze yangu kwa heri, kaumu itasawari,
Ni elimu naabiri, kufata yako amrii,
Mashahidi mashairi, kwa vizazi vya akheri!

Hakuna ninalokariri, bila ya kwako Barrii,
Ni mtumwa sighairi, kazi yako idhihiri,
Nisiwe nami kuffari, kwangu uovu ujiri,
Mashahidi mashairi, kwa vizazi vya akheri!

Naishika bilauri, kunywa ni yako hiari,
Ya watu nisihasiri, na taifa taksiri,
Ila kama yako siri, waiondosha ghururi,
Mashahidi mashairi, kwa vizazi vya akheri!

Sina siri ni dhahiri, za wazi zangu habari,
Ninamuomba Ghaffuri, mengine yasije jiri,
Anayabuni mushawari, mazuri na yenye kheri,
Mashahidi mashairi, kwa vizazi vya akheri!

Giza zito likitanda

Kichwani limeniganda, kutokea utotoni,
Kadiri ninaipenda, naitaka maishani,
Kwalo siachi kukonda, dhoofu yangu imani,
Giza zito likitanda, lailati kadri yaja!

Giza kote linatanda, nuru hamna upenuni,
Nafsi zimejisunda, mamumunye ukubwani,
Nani wa kukupenda, kama haupo machoni,
Giza zito likitanda, lailati kadri yaja!

Nafsi imenishinda, ninaugua moyoni,
Kila nilichokilinda, hivi leo mashakani,
Sasa wanazuka nunda, waingia akilini,
Giza zito likitanda, lailati kadri yaja!

Ninajifunga mkanda, kwendelea taabuni,
Aijambo akipenda, ataniafu Manani,
Mitihani kuishinda, nikaona afueni,
Giza zito likitanda, lailati kadri yaja!

Mwana mpotevu

Wasojua biblia, mpotevu humwambaa,
Hali kitabu chajua, hadithi kimesimulia,
Kondoo aliyepotea, bora kuliko ya mia,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Ni wale wenye nizaa, hiyana na kuchukia,
Mwana watamuachia, imuadhibu dunia,
Na motoni huingia, kwakushindwa kumlea,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Nusura haitakuwa, mwana akishapotea,
Imelani biblia, nasisi twaisikia,
Ila kwa wenye tamaa, yao yakatengenea,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Mwana aliyelelewa, wazazi awasikia,
Ukubwani huja via, akawa sana mbaya,
Au taahira kuwa, kimya ajinyamazia,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Wazazi humfanyia, kila hali kila njia,
Naye si wa kupigania, bali wa kupiganiwa,
Hupewalo huchukua, akosacho huachia,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Vijana wanatakiwa, watundu waliokuwa,
Wazee wamepotea, dhambi wameziachia,
Wengi wajisaidia, na si wa kusaidiwa,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Mali wajilimbikia, kushoto pia kulia,
Vyeo wavigombea, hata kwa wasiyoyajua,
Nchi watuharibia, kwa rushwa kuzipokea,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Watoto wa kufikia, kazi wanagawiwa,
Madudu watufanyia, wawalinda kwa hatia,
Kizungumkuti ubia, walokwisha wawafaa,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Taahira walokuwa, wengine waheshimiwa,
Huku wakijabomoa, kule wanahamishiwa,
Nasi tumeyang'amua, ulizo twawaachia,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Ni nje kiteknolojia, akili wanachezewa,
Wabaki kung'amg'ania, kumbe wanaporomoa,
Waiza demokrasia,kumbe ndio wajiua,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Fakiri tulokuwa, haramu twageuziwa,
Kidogo chanyakuliwa, watoto wao kupewa,
Huwa kama vile kawa, patupu ukifunua,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Karima twamlilia, wajawe kutuhurumia,
Na wanaotunyanyapaa, riziki yao kuvia,
Ulinzi ukautoa, uchi wapate bakia,
Mwana akiwa jeuri, akaja kuwa mzuri,
Akesha wake ubishi
Wazazi kuwasikia,
Wazee hujivunia
Na radhi kumuachia!

Historia twaijua?

Wenzangu nawausia, marafiki kuchagua,
Wapo tunaowajua, utumwa walitutia,
Na ubaguzi wajaa, kwao bado ni kadhia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Historia twaijua, milango twawaachia,
Na bado twajionea, waipondavyo dunia,
Askari wamekuwa, ukubwa wameukwaa,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Yao yanadidimia, nini watatupatia,
Ila kondomu kupewa, tena zilizochakaa,
Na za bure chandalau, eti dawa ya malaria,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Unafiki twajitia, hawa kuwavumilia,
Mugabe namchukia, ila kwa hili radhia,
Mashariki inafaa, sote tuanze elekea,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Nchi wanaigawa, ubaguzi warejea,
Elimu yao yapwaya, uhuni umeingia,
Na fedha zimepungua, raha zao ni karaha,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Wameacha mhofia, mmiliki wa dunia,
Ya watu yawazuzua, Usodoma waridhia,
Rafiki nao tukiwa, dhambi tunajibebea,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Watu ovyo wanaua, na sisi wao wabia?
Mola kumuhofia, wenzangu nawaambia,
Dhulumati hana njia, akhera nayo dunia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Najua mwanichukia, ukweli ninapotoa,
Manjumati mmepewa, na makombo mwatumia,
Hayo yenu yawafaa, na sio sisi raia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Utumwa mnatutia, kulekule mwarejea,
Ardhi mwagaiwa, bure vito kuchukua,
Pipi mkishazipewa, hayo yote mwaridhia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Shahidi historia, itakavyowaumbua,
Dhalimu tutawajua, rahisi wanunuliwa,
Laana kuwaachia, wao na kizazi pia,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Yarabi twakuangukia, zahama kuiondoa,
Mapema itavyokuwa, kadri ukikadiria,
Nchi isije ungua, na watu kuteketea,
Historia yatwambia, mguu umeshakosea!

Mzungu akikujua

Hiy9 ni yake tabia, toka alipozaliwa,
Watumwa huwatumia, ya kwake wakamfaa,
Kaigeuza dunia, tambaa kujifutia,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Nasaba walozaliwa, watumwa waliokuwa,
Kasumba inakolea, vigumu kuwaondoa,
Bado wanyenyekea, mweupe kumtegemea,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Huwapuuza wazawa, na tena wakawagawa,
Nchi wakaachia, wazungu wasiojua,
Na tenda wakazitoa, kwa zuzu nao majuha,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Wanachofuatilia, pasenti wanayopewa,
Mengine kwao udhia, nchi hii yawapwaya,
Benki wakizichukua, Ulaya wanahamia,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Wana huwagharamia, elimu ya kujijua,
Waende kutojijua, na kurudi wasiojua,
Na urithi huachiwa, na wafalme walokuwa,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Sinema za Kinigeria, hili zinalitambua,
Ona shere kuchezewa, mweusi anavyotanua,
HJku njaa wajifia, ndugu zao walokuwa,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Ni Urussi iliyokuwa, na sasa yamerudia,
Wafalme watumia, raia wararuliwa,
Ufaransa nako pia, hadi mapinduzi kuwa,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Afrika yalemaa, kwa mbeleko ya Ulaya,
Na kila mwenye kujua, hili atalikataa,
Vijana ninawaambia, msije mkachelewa,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Sanaa watuulia, sasa nyani tumekua,
Twaiga yasiyokuwa, na tena yasiyofaa,
Weusi hautakuwa, weupe ninawaambia:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Lugha wanatuulia, na elimu kudidimia,
Watoto twawaonea, Kiingereza kutumia,
Kusoma sio kujua, lugha ya mama si bia,
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Lugha ni kujisomea, nyingi tu ukazijua,
Maabara zatumiwa, sayansi na teknolojia,
Miezi haba yafaa, hata mbili ukajua:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Mashariki twatakiwa, tuanze kueleka,
Kichina tukakijua, nacho pia Kimalaysia,
Kadhalika na India, Gujarati kuongea:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!


Ila kwa kufundishia, ni ya mama kutumia,
Rohoni inaingia, na vitu vingi kujua,
Moyoni hukubaliwa, kama mbegu vikakua:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Ninamuomba Jalia, nusura kutupatia,
Kutoa wanaosinzia, tupate wanaozua,
Bure tunayoyaua, na wenyewe kujifia:
Mzungu akikujua, wapenda utegemezi:
Haachi kukutumia
Mtumwa kwake ukawa
Na kisha hukudharau!

Chakula, pembeni......

UTUSANI natumia, tena kwa kukusudia,
Vipofu waliokuwa, pengine watajizomea,
Uvivu wakiachia, matatizo wakajua,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Kipato mwakusudia, kua au kupungua?
Wasafi msipokuwa, ndoto yenu itakuwa,
Maneno mwajivunia, vitendo vimepotea?
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Hoteli zanyanyuliwa, ni uyoga zimekua,
Pembeni ukisogea, kinyesi kinaelea,
Mzungu katumbukia, na laana kaitoa,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Hamkioni kinyaa, wakubwa mlokuwa,
Ulaya mnaingia, ya kwao mwajionea,
Hivi ndivyo inavyokua, au mmepungukiwa?
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Njia kunao udhia, nao pia wa kinyaa,
Huwezi ijua njia, kila pembe yatumiwa,
Pikipiki zashtua, hujui zinakotokea,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Kama kinyesi balaa, na bajaji nazo pia,
Popote hujipitia, hata za miguu njia,
Hatuioni sheria, mitaa yetu nazaa,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Madiwani watumbua, enzi wameshaipewa,
Kazi yao kupokea na si haki kutoa,
Wepesi wa kuchukua, sio wa kuangalia,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Ukubwa ukililia,jua ni kutumikia,
Wakubwa walokuwa, wataka kutumikia,
Sultani wamekua, chini hawatatembea,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Ya kwao si ya raia, wanao wa kutumiwa,
Watu wa kuagiziwa, utumwa walojitia,
Hawajengi, wabomoa, sasa tunajionea,
Chakula, pembeni mavi, hivi utaweza kula ?

Ingekuwa uranium ?

Watu chini huanzia, sio juu hutokea,
Msingi usipokuwa, jengo halitobakia,
Tsunami ikiingia, hakuna cha kubakia,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Kuzuri kulikokuwa, wa juu wankokaa,
Makwetu huku udhia, wa kawaida raia,
Uwekezaji wavia, heshima imepungua,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Watalii twalilia, twakosa hata maua ?
Bustani zapotea, ya ikulu yabakia,
Muhimu kujishangaa, udhia tulivyokuwa,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Watu viguu na njia, nini kitaangaliwa?
Muda wazidi potea, viraka tumebakia,
Mahandaki yamekuwa, njia katika mitaa,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Mlo juu mwatakiwa, haya kuja jionea,
Kwa miguu kutembea, mpate wetu udhia,
Labda mtafikiria, makwenu mkirejea,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Mabasi yetu balaa, TB yatutishia,
Abiria wanavyojaa, kwambukizana si nia,
Ila nchi yatuachia, wenyewe kuteketea,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Muhimbili wasifiwa, mbu wamezawadiwa,
Ni wakubwa walokuwa, utandawazi waingia,
Kimataifa wadaiwa, hadhi waweza chukua,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Vipofu tumeshakuwa, hatuuoni udhia,
Viziwi wa kusikia, ukweli twaukataa,
Husema tusiyojua, twaacha tunayojua,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Bila ya kutengemaa, ya chini yalokuwa,
Usia nawaachia, wana mwaja kuwaua,
Na hukumu zatakiwa, toka sasa kwandaliwa,
Vinyesi barabarani, sasa twafungulia,
Zimesinzia sheria, hazichukui hatua,
Uranium ingekuwa, inavuja kwenye njia:
Nini kingelitokea ?

Mechi nimeiandaa

Wabunge tu kwa wabunge

Kiingereza kwa Kiingereza

Wabunge wanatakiwa, wajifanyo kujua,
Kiingereza kikawa, katikati chaelea,
Na sasa nimeamua, bungeni kwenda ingia,
Mechi nimeiandaa, kuzungumza ung'eng'e!

Kenya nimetembelea, na sababu kuzijua,
Na Uganda nako pia, majilisi nimetua,
Kiingereza wakijua, siwezi wakatalia,
Mechi nimeiandaa, kuzungumza ung'eng'e!

Tanzania tunajua, Kiswahili yatumia,
Tisini na tisa kwa mia, wote wankisikia,
Ila sasa mazoea, yameanza kuchipua,
Mechi nimeiandaa, kuzungumza ung'eng'e!

Wapo wanaojidhania, king'eng'e wanakijua,
Nami sitaki kataa, lao nawakubalia,
Spika nitamwingia, mechi apate niachia,
Mechi nimeiandaa, kuzungumza ung'eng'e!

Awamu kuichukua, king'eng'e tu kutumiwa,
Marufuku itakuwa, Kiswahili kukitia,
Hata neno moja kuwa, budi utaadhibiwa,
Mechi nimeiandaa, kuzungumza ung'eng'e!

Kusema watatakiwa, kwa ghibu kutumia,
Hakuna kuangalia, maandishi yalokuwa,
Fasaha mia kwa mia, lazima upate kuwa,
Mechi nimeiandaa, kuzungumza ung'eng'e!

Tivii nazitumia, rasmi yangu barua,
Zote zinakubaliwa, bungeni kwenda ingia,
Shindano kujionea, mambo yatakavyokua,
Mechi nimeiandaa, kuzungumza ung'eng'e!

Umbeya naukataa, eti komedi itakuwa,
Au Futuhi ikawa, mbavu watu kuumia,
Maana ninavyojua, Kiingereza mwakijua,
Mechi nimeiandaa, kuzungumza ung'eng'e!

Nahofu kuwasemea, wakubwa waheshimiwa,
Msininyime ridhaa, shindano kutofanikiwa,
Nami nawanyenyekea, hili mkalikubalia,
Mechi nimeiandaa, kuzungumza ung'eng'e!

Achia rasilimali

Siasa mnatumia, makapi mtabakiwa,
Sanaa nimesomea, na ukweli naujua,
Vingine haitakuwa, ila kujiharibia,
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Bora ukiwachukia, kwa akili kutumia,
Waoga ukachukua, upate kuwatumia,
Naapa utafulia, na mbali hautafikia,
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Taylor hutomjua, na Fayol ni ruia,
Demming nikikwambia, nokiauti nakutoa,
Sembuse gwiji radhia, Drucker aliyekuwa?
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Rasilimali ni njia, kila pembe kuingia,
Siasa, uchumi pia, kingine hakitafaa,
Na hasa kama ikiwa,ni watu wa kuamua,
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Hawa waonyesha njia, taasisi ikakua,
Si kila mtu afaa, nafasi kushikilia,
Wapo waliozaliwa, maalum walokuwa,
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Wengine wamejaliwa, wa kula na kutumia,
Hawawezi angalia, chochote kipate kua,
Ila wao kujilia, hilo kweli wanajua,
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Wakubwa nawashangaa, kamba walioshilia,
Sasa wanaiachia, farasi ajiendea,
Na kitakachotokea, sote tunatarajia,
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Fedha ukiwamwagia, shimoni zinaingia,
Chini kwenda didimia, ndio itakuwa tabia,
Hakuna wa kuzuia, 'freefall' inakuwa,
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Hakuna wa kuzuia, 'freefall' inakuwa,
Wang'eng;e nawaachia, bungeni waliojaa,
Hili kuwatasiria, raia msiyoyajua,
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Razaki namtambua, kwake hili nimejua,
Wala sitaki umbeya, kwingine kusingizia,
Nami namkubalia, mwanga wake natumia,
Achia rasilimali, watu bora ilokuwa:
Na taasisi huvia!

Hutowahadaa wote

Uongo waliozoea, wataka jirahisishia,
Vyombo kwa kuvitumia, wadhani watafanikiwa,
Gizani tungelikuwa, hili ningelihofia,
Sikuzote, pande zote, watu wote ni vigumu:
Wote kuwadanganya!

Simu sasa zaoangea, ukweli utaujua,
Kwa masafa huchanua, vijijini kuingia,
Wazee wanayajua, hata na watoto pia,
Sikuzote, pande zote, watu wote ni vigumu:
Wote kuwadanganya!

Picha zinasimulia, kwingine yanayotokea,
Senegal nilijua, kifaransa kuwaambia,
Babu wakamchezea, na wakamtosa pia,
Sikuzote, pande zote, watu wote ni vigumu:
Wote kuwadanganya!

Mnachokipuuzia, ndicho kitawaumbua,
Akili zimechanua, Tanzania ni maua,
Vijana rangi wazua, kwa fani na tasnia,
Sikuzote, pande zote, watu wote ni vigumu:
Wote kuwadanganya!

Nyota wanachipukia, kuuliza wanaojua,
Uongo kuuukataa, na wakubwa kutumiwa,
Kwao demokrasia, azizi imeshakua,
Sikuzote, pande zote, watu wote ni vigumu:
Wote kuwadanganya!


Vizee vilivyokuwa, ndivyo mmeachiwa,
Njaa inavovisumbua, na fani wasiozijua,
Kama walivyolemaa, ndivyo mtavyolemaa,
Sikuzote, pande zote, watu wote ni vigumu:
Wote kuwadanganya!

Mhando mmemwachia, dungayembe mwachukua,
Mtavuna msiyojua, na chenfga kuambulia,
Sana nawasikitikia, njia mnavyopotea,
Sikuzote, pande zote, watu wote ni vigumu:
Wote kuwadanganya!

Samaki waanza kuoza, pakachani wabakia?

Kwa mamia wanaoza, samaki kwenye pakacha,
Uoza wafululiza, kama vile wapikicha,
Juu utajitokeza, asubuhi kumekucha,
Kwenye pakacha samaki, nusuye wameshaoza:
Wewe umejituliza,
Hivi utaacha kuoza?

Samaki nawauliza, mbona bado mwajificha ?
Mngemuomba muweza, mngeacha Ualinacha,
Wenyewe kujigeuza, kabla hamjachacha,
Kwenye pakacha samaki, nusuye wameshaoza:
Wewe umejituliza,
Hivi utaacha kuoza?

Mazoea yawakwaza, kuchoropoka mwakacha,
Wenyewe mwajimaliza, pakacha msipoacha,
Maana budi kuoza, hili hatwezi waficha,
Kwenye pakacha samaki, nusuye wameshaoza:
Wewe umejituliza,
Hivi utaacha kuoza?

Hunuka wanaooza, tena huwezi kuficha,
Thamani mtajikwaza, uoga kuwachekecha,
Hadhi mkailemaza, mkabakia machicha,
Kwenye pakacha samaki, nusuye wameshaoza:
Wewe umejituliza,
Hivi utaacha kuoza?

Watu watawapuuza, toka mguu hadi kichwa,
Wengine kuwaeleza, mmeshakuwa ndondocha,
Au sokoni mwauza, kama vile ni mchicha,
Kwenye pakacha samaki, nusuye wameshaoza:
Wewe umejituliza,
Hivi utaacha kuoza?

Mwanunuliwa ni viza, mayai kwenda pikicha,
Kutupa kwenye jeneza, ndani mlilolificha,
Na shaibu na ajuza, msukule kuwaficha,
Kwenye pakacha samaki, nusuye wameshaoza:
Wewe umejituliza,
Hivi utaacha kuoza?

Sina nililobakiza, na samaki sio pacha,
Ila nimewajuliza, wacheze lao chakacha,
Au wasipoliweza, basi iwe hiyo chachacha,
Kwenye pakacha samaki, nusuye wameshaoza:
Wewe umejituliza,
Hivi utaacha kuoza?

Taifa lenye uongo

KABLA hatujasogea, jambo nimeazimia,
Kongamano latakiwa, ukweli kuzungumzia,
Adili tukaanzia, na mengine kufuatia,
Taifa lenye uongo, halimpendezi Mola!

Wakubwa wazungumzia, kama yangu kurudia,
Waongo tumeshakuwa, Taifa linahujumiwa,
Juu ulishaanzia, na chini unafikia,
Taifa lenye uongo, humchukiza Mola!

Mkuu aandikiwa, uongo ajisomea,
Kisha aukubalia, taifa kutangazia,
Wacheka hata majuha, nazaa kuuparamia,
Taifa lenye uongo, halimpendezi Mola!

Wabunge waongopewa, ridhaa wanaitoa,
Labda posho watetea, isije kupungua,
Ndivyo tulivyokua, na hapo tumefikia,
Taifa lenye uongo, humchukiza Mola!

Waziri akishajua, uongo wakubaliwa,
Na chama kilichokuwa, na makada wake pia,
Na yeye atajizoa, ukumbini kuingia,
Taifa lenye uongo, halimpendezi Mola!

Na yeye atajizoa, ukumbini kuingia,
Hoja zilizotafitiwa, akazipinga kwa riha,
Naona ni ukichaa, hapa tulipofikia,
Taifa lenye uongo, humchukiza Mola!

Heshima imepungua, mzee ninawaambia,
Kioja mmeshakua, wapi mguu mtatia?
Matope mwajipakaa, mwadhani poda imekua?
Taifa lenye uongo, halimpendezi Mola!

Ni haya kufuatia, kongamano nanuia,
Adili waliojaa, mkono naungojea,
Hatua kuzichukua, likafana kila njia,
Taifa lenye uongo, halimpendezi Mola!

Huko tutazungumzia, maadili Tanzania,
Kwa ukweli kuanzia, serikalini ukawa,
Iwe kuvunja sheria, uongo wakiutoa,
Taifa lenye uongo, humchukiza Mola!

Wangapi utawahonga?

HAMSINI milioni, hesabu Watanzania,
Mna ngapi milioni, wote kuwagawia,
Ukubwa mkauwini, na vinono kuopoa?
Wangapi utawahonga, milioni hamsini?

Hili naona utani, na litawageukia,
Wakaikosa thamani, nyani wanaotumiwa,
Moto uwe duniani, pamwe na akhera pia,
Wangapi utawahonga, milioni hamsini?

Hii kubwa nuksani, haki kwenda kununua,
Yamchukiza Manani, motoni huandikiwa,
Utapeta duniani, ila kesho utalia?
Wangapi utawahonga, milioni hamsini?

Nawaona majinuni, wanaifanya hadaa,
Kama vile ni utani, ya muda kuitikia,
Kumbe wako hatarini, milele watapotea,
Wangapi utawahonga, milioni hamsini?

Uwaonye Shukrani, bwana wa kuhurumia,
Hawa kama mumiani, si watu wa kujijua,
Wanatakiwa imani, kwao kuipalilia,
Wangapi utawahonga, milioni hamsini?

Wataishia motoni, macho wasipofumbua,
Ni ujinga wake nyani, hayawani alokuwa,
Kwanini na kisa gani, wakaja kuangamia?
Wangapi utawahonga, milioni hamsini?

Vyoo vya Chuo Kikuu

Mtihani nautoa, wote ni watahiniwa,
Utafiti kuandaa, Chuo Kikuu ukawa,
Tupate sote kujua, kama kiwango twafaa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Kufunga wameamua, afya wanaohofia,
Vyoo sasa ni balaa, harufu yaweza kuua,
Vinyesi vyatapakaa, ni maua yamekuwa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Wengine wameamua, ratiba kujiwekea,
Safari kujifungia, nyumbani kwenda jifaa,
Mara tatu watimua, vyoo kwao kutumia,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Mbali wanaotokea, msiba kwao imekuwa,
Hawanalo la kugwaya, vijijini wamezoea,
Kuchimba dawa tabia, si ajabu Tanzania!
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Holi faivu twatua, vyooni tunaingia,
Mlango ukifungua, na ndani ukaingia,
Ukiweza jisaidia, maksi wazawadia,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Chooni atakayekaa, digrii atapewa,
Kafaulu kwa kinyaa, kiumbe kuvumilia,
Kutoka kikikataa, huna cha kuambulia,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Wasomi tungedhania, viongozi walokuwa,
Na nje wameshakaa, vyoo wamejionea,
Haya wasingevumilia, kwao ingekuwa balaa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Migomo waichukia, si vyoo vyenye kinyaa,
Ukubwa wafurahia, nyuma ni harufu mbaya,
Hekalu wajijengea, wao na zao jamaa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Wahindwa kuangalia, ya walio wengi afya,
CIA wamekuwa, migomo kuizuia,
Na chama wakitumia, kinyesi wakipakaa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Tivii yao najua, chooni haijaingia,
Laiti ingelijua, hali bora ingekuwa,
Labda waambiwa, hawawezi kuingia,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Au juu waliokuwa, uganga wanatumia,
Kila anayeingia, usafi ajionea,
Ibilisi kubwa dawa, hasa wenye roho mbaya,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Au wanaogopewa, mabaya kutoambiwa,
Na mazuri wasifiwa, na wapambe walokua,
VC lini kuingia, chooo chao raia?
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Au wameteuliwa, shemeji waliokuwa,
Na ndugu zao kujaa, rafiki nao jamaa,
Na wanachokiangalia, safari zao Ulaya?
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Zuri ninalingojea, si watu kuhujumiwa,
Sadaka nimeitoa, chuo kiweze jaliwa,
Daraja juu kupaa, cha kimataifa kuwa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Usafi ukishaingia, chuo kikuu kikawa,
Mpaka msingi pia, sekondari kufikia,
Na taasisi mamia, hali bora ikishakuwa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Na taasisi mamia, kimataifa zikawa,
Ruhusa nitaitoa, uranium kuchimbua,
Usalama nitajua, kweli sasa wazingatiwa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Kabla hamjachimbua, madini mnayotuibia,
Chuo kikuu kutua, vyoo kukarabatiwa,
Kwa hilo tutaelewa, mema mwaanza tutakia,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Wiki ninawaachia, kwa vyoo kutengemaa,
Au picha nachukua, kutangazia dunia,
Hadhi mkaondolwa, na madoa mkatiwa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Vya msingi vyatakiwa, wengi vinawaofaa,
Ubinafsi kinyaa, kama kinyesi na njia,
Kiumbe hawezi kua, unafsi alojaa,
Kipimo cha Uranium, vyoo vya Chuo Kikuu:
Tukachimbue au la!

Mazishi si kampeni

HAPA kwangu kupitia, Kisasi utamjua,
Jina kati yake mia, Qudusi aliyopewa,
Kila ukizingatia, maana yamechukua,
Mazishi si kampeni, Kisasi muogopeni!

Maqilla pia kapewa, srarehe azijua,
Si utani nakwambia, na wala sintakutania,
Na yeye ananijua, napenda kumlilia,
Mazishi si kampeni, Kisasi muogopeni!

Ajua namhofia, hasira akiingia,
Ila akifurahia, nataka mkaribia,
Nani wa kumchezea, kama baba alokuwa?
Mazishi si kampeni, Kisasi muogopeni!

Lakini si kwa udhia, kwa usafi kutokuwa,
Na mahala patakiwa, mwenyewe unapokuwa,
Mchezo kwangu ni dua,kila siku huitoa,
Mazishi si kampeni, Kisasi muogopeni!

Wapo wanaotania, hadhira ilipokuwa,
Laiti wangelijua, kisasi watafanyiwa,
Wenyewe wangekimbia, stara kuigombea,
Mazishi si kampeni, Kisasi muogopeni!

Siasa wanaotia, pale isipotakiwa,
Kama simu kutumia, masjidi ukiingia,
wanatembea na kaa, moto linaloungua,
Mazishi si kampeni, Kisasi muogopeni!

Riha yakataliwa, kwangu sintokarirbia,
Dhaifu nimeshakua, nani wa kuniangalia,
Hadi nitaporejea, kwa Mola wangu Jalia,
Mazishi si kampeni, Kisasi muogopeni!

Uhai mwahuzunika

VIUMBE wanafiki, hebu Mola angalia,
Kwenye msiba mikiki, wadhani wafurahia,
Walokuwa hawafiki, wa kwanza wanaingia,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Uko hai hushikiki, wote wankukimbia,
Wala hauaminiki, nani atakuridhia,
Ya kwako hawahusiki, ya kwao hushikilia,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Huwa haueleweki, hawaijui tabia,
Ikiwa mbali hufiki, njia waliochagua,
Husemwa hutabiriki, hasara waweza tia,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

La kwako halijengeki, zaidi hulibomoa,
Kiumbe hakimiliki, hadi awe na madoa,
Roho hazivumiliki, na si ruksa kutoa,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Kila kitu si riziki, SMS hutumiwa,
Mdogo haneemeki, mkubwa akivimbiwa,
Na mnyonge hanyongeki, hubaki kama udhia,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Wengi hawafurahiki, maisha kwao ruia,
Huota hayakamiliki, mengine huchimbuliwa,
Fakiri hatamaniki, kwa wakubwa ni kinyaa,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Wala hana taharuki, utajiri alopewa,
Au kwa cheo kukua, kikubwa kashikilia,
Hajui asiyemjua, na ndugu hunyanyapaa,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Adhimu siwashtaki, hayo yao majaliwa,
Moto haukamiliki, bila mkaa kupewa,
Na ahali na rafiki, wengine kuni wakawa,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Kiumbe hakamiliki, hadi kujiondokea,
Maisha yake hakiki, utakuta ni tanzia,
Ila wasio na dhiki, wachache wachaguliwa,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Maisha hayashikiki, kwa wengi waliokuwa,
Na wasio wamiliki, ndio wajiendeshea,
Kugawa haigawiki, hadi machweo ya jua,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Najua sistahiki, haya kujawambia,
Sikujali tawfiki, ugomvi naununua,
Mseme sieleweki, hadi kizazi kipya,
Uhai mwahuzunika, kifo mwasherehekea ?

Mzike anayekufaa

Issa ibn Mariamu, alikwishatuambia,
Unafiki kaujua, nje akawatolea,
Wote akawaambia, mfu huzikwa na jamaa,
Mzike anayekufaa, wengine wazikwa na mfu!

Haya namkubalia, siwezi kuyakata,
Ni ukweli uliokuwa, vingine haitakuwa,
Ila wasiojitambua, ukale wamekalia,
Mzike anayekufaa, wengine wazikwa na mfu!

Hofu wanaitumia, mauti yakiingia,
Usononi kuwajaa, kwa kile kisichofaa,
Hai alipokuwa, hayati walimwambaa,
Mzike anayekufaa, wengine wazikwa na mfu!

Ya mwisho ikiwadia, watu hujapigania,
Mstari mbele kua, heshima kujiondoa,
Naona kama kinyaa, na kwangu si maridhia,
Mzike anayekufaa, wengine wazikwa na mfu!

Akili watuchezea, wazima waliokuwa,
Ndio ninawaambia, hayunami asokuwa,
Ukishaninyanyapaa, ufu umeshauchukua,
Mzike anayekufaa, wengine wazikwa na mfu!

Mtu asiyekufaa, mfu kwako keshakua,
Usingoje kumchimbia, siku haitofikia,
Ruksa ukamwambaa, na yake kutoyajua,
Mzike anayekufaa, wengine wazikwa na mfu!

Viumbe tunatakiwa, kuibadili tabia,
Twendeni kiteknolojia, na chipsi kuzitumia,
Ili unayemridhia, nd'o anayekupigia,
Mzike anayekufaa, wengine wazikwa na mfu!

Makaburi kuyajua, dijito kuyawekea,
Ukibipu hurejea, ujue lilipokuwa,
Kidogo tu hujengewa, na bado mazuri yakawa,
Mzike anayekufaa, wengine wazikwa na mfu!

Wafu hai walokuwa, nao wakisharejea,
'No access' kuondoa, tena ukawaridhia,
Na wakishakubaliwa, uhai utarejea,
Mzike anayekufaa, wengine wazikwa na mfu!

Nchi eti mwaongoza?

Mwajivuna kuongoza, swali ninawauliza,
Kitu gani mwaongoza, kila kitu twaagfza?
Hdi sindano ni viza, hatuwezi tengeneza?
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa unda sindano?

Nchi eti mwaongoza?

Trekta kutengeneza, hivi ni miujiza,
Wazungu tukiagiza, kazi zinazowaiza,
Hapa kwettu kuwatunza, kazi hii hawataweza?
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa unda trekta?

Nchi eti mwaongoza?

Plau tunaagiza, powertiller mwaeleza,
Kitu msichoeleza, kwanini kutotengeneza,
Usanii mwaagiza, rahisi vitu kuoza?
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa unda plau?

Nchi eti mwaongoza?

Mabasi yatutatiza, nini tunachokiweza,
Mbona China wameweza, na India watengeneza?
Wahandisi twawaponza, hawawezeshwi wakaweza?
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa unda mabasi?

Nchi eti mwaongoza?

Swaziland naeleza, sio inayojiweza,
Leo wanatengeneza, friji zenye kupoza,
Nishati jua hutunza, umeme imepatiliza,
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa unda friji?

Nchi eti mwaongoza?

Majiko tunaaagiza, badala ya kuengeneza,
Na kupika twawajuza, kila siku tunafanza,
Biashara yatokeza, bei ikiwa yasuuza,
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa unda majiko?

Nchi eti mwaongoza?

Umma tukiwafunza, umeme watatengeneza,
Wazawa trunawabeza, yankii twaagiza,
Wenyewe twajimaliza, twazidi kujilemaza,
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa fuma umeme?

Nchi eti mwaongoza?

Roho tunaziuza, baharini Tanzania,
Tumeshindwa kuongoza, meli kutengeneza,
Wahandisi twalemaza, bilioni twapoteza,
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa kuunda meli ?

Nchi eti mwaongoza?

Ndege zitatumaliza, mitumba tulizoagiza,
Wenyewe twajichuuza, wajanja tunajifanza,
Yatakujatupatiliza, angalizo nawatunza,
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa kuunda ndege ?

Nchi eti mwaongoza?

Wachina tusipowaiza, reli tutatengeneza,
Na tena tukaifanza, ya kisasa muujiza,
Umeme ikasambaza, na haraka kufikiza,
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa kujenga reli ?

Nchi eti mwaongoza?

Barabara zatitia, wajenzi wa kuteua,
Zenyewe hujibomoa, wakubwa wakitembelea,
Nao wameshuhudia, ukweli wanaujua,
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa kujenga njia ?

Nchi eti mwaongoza?

Viwanja vya burudani, na pia vya kucheza,
Bado tumasikini, hali hili twaliweza,
Huu kama si uhuni, nini mtanieleza?
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa jenga viwanja ?

Nchi eti mwaongoza?

Bandari zina kinyaa, na sura zake ni mbaya,
Hata nilipowaambia, kidogo tu mmeangalia,
Hali yaweza ikawa, na sura za kuvutia,
Nchi eti mwaongoza, mwashindwa jenga bandari?

Nchi eti mwaongoza?

Kujenga pia twaweza, nia yetu bado mbaya,
Umasikini twaukuza, sera zetu kwendelea,
Hali ukweli najuza, hili si la kuchezea,
Nchi eti mwaongoza,watu wanakosa nyumba?

Nchi eti mwaongoza?

Njia zipo nyingi sasa, nishati kujivunia,
Ila naona twasusa, akili kuzitumia,
Wananchi twawatesa, hali sisi twatanua,
Nchi eti mwaongoza, wanaikosa nishati?

Nchi eti mwaongoza?

Maji tutakuja agiza, kama tusipoangalia,
Ajizi tunaifanza, watu kutaka jifaa,
Wajanja twawaachia, na sasa wanatunyoa,
Nchi eti mwaongoza, watu wanakosa maji ?

Nchi eti mwaongoza?

Nyingine ni za kupuuza, akili zisizokuwa,
Akili zenye kuzoza, ya yale yasiyokuwa,
Nani upate mjuza, ajira zimepotea?
Nchi eti mwaongoza, vijana hawana kazi?

Asalam aleykum

Mwangoja limiwa shamba?

Vibaya mmelelewa, sikuzote kufanyiwa,
Wengi mmeshalemaa, ya kwenu yadidimia,
Kisa eti mwangojea, mtu kuja wafanzia,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Mithali naitumia, shamba kama tungekuwa,
Tungoje kuja limiwa, na mbegu tukagawiwa,
Ni ajabu ingekuwa, njaa kutokujatuua,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Serikali haijawa, hivyo mnavyoidhania,
Tajiri ingelikuwa, kodi isingechukua,
Kwani ingejitegenea, na tena kutusaidia,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Serikali yetu njaa, tulimacho yategemea,
Na kodi inazopewa, na viwanda vilokuwa,
Bishara nazo pia, kwa kodi huzichangia,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Na migodi yatakiwa, kuacha zao sanaa,
Si tu kodi kutoa, bali mapato kugawa,
Ni yetu Watanzania, vingine watuibia,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Huu mtaji ukiwa, zana tukazinunua,
Shambani tukiingia, vitu tutajifanyia,
Miaka haitazubaa, nchi bora itakuwa,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Kila mtu atakiwa, akili kuzitumia,
Kitu ukafikiria, maishani kukufaa,
Sahau ninakwambia, kuja tena ajiriwa,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Kihamba ukishapewa, kulima unatakiwa,
Ardhi jana ilikuwa, leo akili twapewa,
Ubongo kuutumia, maisha yakachanua,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Usingoje kulimiwa, wala kuja hudumiwa,
Anza kuchachamaa, masomoni unapokuwa,
Fikra kuziangua, kwa mayai ya kufaa,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Moja moja kuchagua, huku chuo waingia,
Hadi ukimalizia, ajira umeshafyatua,
Muajiri utakuwa, na wala sio mwajiriwa,
Mwangoja limiwa shamba, mavuno yawe ya nani?

Chakula kimeshakwisha

HIVI ndivyo imekuwa, hapa kwetu Tanzania,
Watoto wote walia, njaa imewazidia,
Na kial wakiulizia, mama anawaambia:
Chakula kimeshakwisha, baba yenu kala chote!

Feri imeshatushinda

Uongo utatuua, ukweli tuambiane,
Ya feri tunayoona, lipi mwataka mjuwe?
Twatakiana mabaya, wala hakuna kingine,
Feri imeshatushinda, uranium tutaiweza?

Mamluki mlokuwa, ni lazima tuwabane,
Taifa bado kukua, tusifanyane wajane,
Kubaleghe twatakiwa, ndio vichwa viumane,
Feri imeshatushinda, uranium tutaiweza?

Wengi tumeshawajua, maneno yenu manene,
Tena sana mwaongea, mkishakosa matone,
Rahisi kwenu kuua, kwa kuzitafuta 'mane',
Feri imeshatushinda, uranium tutaiweza?

Shahidi najichagua, na vizazi niungane,
Hadhari kukusudia, hadharani niinene,
Mhanga ninajitoa, watoto wasiuane,
Feri imeshatushinda, uranium tutaiweza?

Ikifaa kungojea, hata ikiwa karne,
Lipi lichimbwalo latufaa, hebu kwa wazi mnene,
Kumi mwaisifiwa, hakika nyie senene,
Feri imeshatushinda, uranium tutaiweza?

Trilioni zatakiwa, kwa ubia tuungane,
Na kama wajitetea, kwa hizo zao mashine,
Waziwazi nawambia, twendeni kwa wengine,
Feri imeshatushinda, uranium tutaiweza?

Wachina ninawajua, inafaa tuungane,
Mzungu ni haramia, vinginevyo tusimuone,
Anajifanya kujua, kumbe anatupa mavune,
Feri imeshatushinda, uranium tutaiweza?

Majuha waloobakia, nao hawa waungane,
Nchi zao zinaliwa, wao chao wakivune,
Uchungu hawakujaliwa, wataka wao wanone,
Feri imeshatushinda, uranium tutaiweza?

Feri wangeliijua, haya ni budi waone,
Haramu mwazungumzia, kubwa kama hii niione,
Najua haitakuwa, upele wenu mkune,
Feri imeshatushinda, uranium tutaiweza?