Friday, December 30, 2011

Ujanja wenye hasara

Ajuaye kila kitu, ujanja wenye hasara,
Hujifukuzisha watu, mtu kujiona bora,
Na wengine ni kiatu, au bovu matambara,
Ujanja wenye hasara, ajuaye kila kitu!

Beleshi ndilo sepetu, gharama mwana hasara,
Hayendi maisha yetu, wengine wakisowera,
Hakuna kibaya kitu, kama bure masihara,
Ujanja wenye hasara, ajuaye kila kitu!

Usiache vifutu, kukufanyia duara,
Heri akumeze chatu, wasikunyanyase sira,
Maana kisu cha butu, hukuokoa kafara,
Ujanja wenye hasara, ajuaye kila kitu!

Ushauri jadi yetu, udikteta hasara,
Tusikilize wenzetu, haki bila kuwapora,
Tuijenge nchi yetu, kwa heri na takibira,
Ujanja wenye hasara, ajuaye kila kitu!

Swali jibu likifutu, hujitambua majura,
Wakarejea kwa utu, wajijengee mnara,
Usipotumia watu, itakudhuru hadhira,
Ujanja wenye hasara, ajuaye kila kitu!


© 2011 Sammy Makilla

Uoga wenye faida

Uoga nitajitia, na magoti kutitia,
Kila ninapotambua, jambo nimeshakosea,
Udhaifu kuelewa, yakini umechangia,
Uoga wenye faida, kumuogopa Muumba.

Kwangu sikukusudia, shida kunisaidia,
Jambo likishatokea, lazima kulijutia,
Utakwa sijafikia, upungufu umejaa,
Uoga wenye faida, kumuogopa Muumba.

Na toba kuitubia, huruma kuhurumiwa,
Niombe kusamehewa, Muumba kunisikia,
Sio ya kwangu dunia, nini ninachotambia?
Uoga wenye faida, kumuogopa Muumba.

Njiani najipitia, mwisho wangu naujua,
Huko ninakoelekea, ndipo ninazingatia,
Msafara sijajua, kama nyuma wafatia,
Uoga wenye faida, kumuogopa Muumba.

Mwenyewe nilizaliwa, na pekee nitatua,
Watakaonipokea, uwanjani sijajua,
Naweza pekee ingia, njia nikaulizia?
Uoga wenye faida, kumuogopa Muumba.


© 2011 Sammy Makilla

Hutaniwa tasnia

Kazi nyingine yafaa, sio ya kusimulia,
Ukweli inatakiwa, sio uongo kuuzua,
Mambo kujipikia, yasiyokuwa yakawa,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!

Kafiri kutumikia, mwandishi anapotea,
Heshima hujivunjia, akakosa kuaminiwa,
Utu huja kupotea, ovyo kudharauliwa,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!

Uandishi kujijua, na wito kuupokea,
Wanyonge kusaidia, na sio kusaidiwa,
Hapo ukipafikia, mbele hautaendelea,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!

Kiatu lazima kuwa, kafiri wakakuvaa,
Mavi kuyakanyagia, wewe wakakuachia,
Na waliokutegemea, vingine kukuelewa,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!

Wito ungepigania, nyuma wangelibakia,
Kambi ukiikimbia, muasi watakujua,
Usemalo hupotea, masikio kuzibia,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!

Dini budi kurudia, utuwe ukaujua,
Kwako kuyaazimia, watu yatayowafaa,
Hatua ukachukua, kufata adhimu njia,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!

Njia usiyopotea, Muumba akaridhia,
Kwa yakini kukulea, kilicho bora ukawa,
Jina akakujengea, na kizazi kufatia,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!

Mtumwa mwenye hadaa, kingine hawezi zaa,
Hata vipi akikilea, ovyo lazima kikawa,
Uhuru hatoujua, hadi mwisho wa dunia,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!

Enyi mliopotea, ombeni kujitambua,
Pumzi kuhesabia, neema mliyojaliwa,
Si ovyo kuitumia, mkaja kuyajutia,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!

Ibariki tasnia, wenye wito kuingia,
Wanyonge kupigania, haki wakajipatia,
Fukara kuwainua, na sisi kujipatia,
Hutaniwa tasnia, kafiri kutumikia!


© 2011 Sammy Makilla

Mgonjwa umembeba

Hofu inakutambaa, hadi machoni yang'aa.
Sababu sijaijua, au uliyemchukua,
Waogopa kukufia, njiani bado ukiwa?
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Dhamana umechukua, tena umezidishia,
Ni vigumu kutulia, acha mbali kupumua,
Mikono imekujaa, lipi kuachilia?
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Ukubwa mwaulilia, kiasi hamjajua,
Na yanapowaelemewa, sababu ovyo mwatoa,
Na majibu ya kinyaa, utu yasiyojaliwa,
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Mgonjwa mwamchkua, kavukavu imekua,
Machela kugharamia, mmeona ni udhia,
Au mmepungukiwa, michango haikutimia?
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Ambulensi mwaachia, mjini kutembelea,
Kijijini kufikia, ni vigumu haijawa,
Mwasema mmeendelea, njia gani mwatumia?
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Haya mgonjwa alia, spitali kufikia,
Vipi mtakimbilia, yasishe yake masaa,
Au mtaadhiriwa, njiani aje wafia?
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Zaidi mlizubaa, mgonjwa kumchungua,
Saa hizi angekuwa, dokta keshamwangalia,
Ugonjwa umezidia, hatihati imekua,
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Chakula hakupatia, atembea nayo njaa,
Maradhi yanaingia, hadi yasikotakiwa,
Kazi kubwa itakuwa, mgonjwa kumfufua,
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Chakula ulijilia, chote alichopikiwa,
Uzito ulijitia, kujabeba hukujua,
Hakika nawashangaa, juu mlotangulia!
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Wenyewe mwajipalilia, wananchi wateketea,
Kinyume ngetarajia, watu kwanza kuwagea,
Kisha ndiyo ije kuwa, na nyie kujimegea,
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Wa kwanza mmeshakua, kila kitu kupakua,
Unga ulipoishia, mchuzi mkaumwaa,
Hakuna kilichobakia, sufuria zinang'aa,
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?

Iweje mnashangaa, mgonjwa keshazidiwa,
Haya mmemtakia, shari yenu ilokuwa,
Na njiani akiwafia, haki yenu itakua,
Mgonjwa umembeba, waogopa kukufia?


© 2011 Sammy Makilla

Kuchota maji nchini

Amini usiamini, maji sasa ni muhimu,
Watu waenda kazini, maji kazi ya kudumu,
Yakikosekana ndani, amani haitadumu,
Kuchota maji nchini, sasa kazi ya kudumu!

Na walio mashakani, kinamama wahudumu,
Wanatembea gizani, jamaa kuwakirimu,
Asubuhi na jioni, hii ni yao hukumu,
Kuchota maji nchini, sasa kazi ya kudumu!

Posho wanazisaini, walao aisikirimu,
Kinamama vijijini, hakuna wa kuwarehemu,
Hili lazidi karni, laendelea kudumu,
Kuchota maji nchini, sasa kazi ya kudumu!

Maji yenyewe topeni, kukamua ni muhimu,
Hatukiri wa mjini, vijiji wavidhulumu?
Yakiwa ya kisimani, meupe hayatakua?
Kuchota maji nchini, sasa kazi ya kudumu!

Waruzuku vijijini, sisi tusiowafahamu,
Tuache kuwazaini, tufanze ya kugharimu,
Waipate afueni, nchi wawe nayo hamu,
Kuchota maji nchini, sasa kazi ya kudumu!


© 2011 Sammy Makilla

Umeme twausikia

Uhuru tunaujua, tena tumeshaugua,
Vinazidi vitambaa, njiani kuupepea,
Twahofia kupotea, umeme msipotuwashia,
Uhuru tunaujua, umeme twausikia!

Uhuru twautambua, ila giza laingia,
Umeme mngetuwashia, mengi tungejionea,
Kama hivyo haikuwa, tunaenda kuvumbua,
Uhuru tunaujua, umeme twausikia!

Ahadi mmezitoa, au pipi mmezigawa,
Akili mwatuchezea, au shere imekua,
Vipi mwajisikia, mabomba mkimwaia?
Uhuru tunaujua, umeme twausikia!

Mchuchuma naelekea, mkaa kujiokotea,
Nyumbani nitatumia, umeme sawa ikawa,
Nachoka vumilia, miaka yatangulia,
Uhuru tunaujua, umeme twausikia!

Dini mnaoijua, ibada mngefanyia,
Moto kuugharamia, waumini kutumia,
Sio sadaka kutwaa, wenyewe mkajilia,
Uhuru tunaujua, umeme twausikia!

Mwafanya yasiyofaa, uchaMungu mwajitia,
Laiti mngetambua, kile kinachowangojea,
Mbali mngesogea, na wanaowahadaa,
Uhuru tunaujua, umeme twausikia!

Watu mnawakimbia, wakubwa mwawafanyia?
Hivi Mola mtamjua, kwa watumwa nyie kuwa,
Au viongozi kuwa, ukweli mkatetea?
Uhuru tunaujua, umeme twausikia!

Uhuru babu mwajua, wao waliulilia,
Nyie sasa mwaua, hata walichoanzia,
Aibu ingewajaa, ghafla wangetokea,
Uhuru tunaujua, umeme twausikia!

Masikini walokua, chini yenu watembea,
Hivi mwawaangalia au mnawasiginia?
Mola ninamlilia, ya kwenu kuwagaia,
Uhuru tunaujua, umeme twausikia!


© 2011 Sammy Makilla

Uhuru tunaujua

Uhuru tunaujua, tena tumeshaugua,
Vinazidi vitambaa, njiani kuupepea,
Twahofia kuungua, maji yasipotolewa,
Uhuru tunaujua, maji hatujayajua!

Uhuru twautambua, ila kiu twasikia,
Maji mngetupatia, zaidi tungesikia,
Kama hivyo haikuwa, tunaenda kuchimbua,
Uhuru tunaujua, maji hatujayajua!

Ahadi mmezitoa, au pipi mmezigawa,
Akili mwatuchezea, au shere imekua,
Vipi mwajisikia, mabomba mkimwaia?
Uhuru tunaujua, maji hatujayajua!

Kisimani naelekea, maji kwenda jichotea,
Hii leo Ijumaa, suna inashauriwa,
Maji kuyatumia, hadi ya kuyaogea,
Uhuru tunaujua, maji hatujayajua!

Dini mnaoijua, ibada mngefanyia,
Maji kuyagharamia, waumini kutumia,
Sio sadaka kutwaa, wenyewe mkajilia,
Uhuru tunaujua, maji hatujayajua!

Mwafanya yasiyofaa, uchaMungu mwajitia,
Laiti mngetambua, kile kinachowangojea,
Mbali mngesogea, na wanaowahadaa,
Uhuru tunaujua, maji hatujayajua!

Watu mnawakimbia, wakubwa mwawafanyia?
Hivi Mola mtamjua, kwa watumwa nyie kuwa,
Au viongozi kuwa, ukweli mkatetea?
Uhuru tunaujua, maji hatujayajua!

Uhuru babu mwajua, wao waliulilia,
Nyie sasa mwaua, hata walichoanzia,
Aibu ingewajaa, ghafla wangetokea,
Uhuru tunaujua, maji hatujayajua!

Masikini walokua, chini yenu watembea,
Hivi mwawaangalia au mnawasiginia?
Mola ninamlilia, ya kwenu kuwagaia,
Uhuru tunaujua, maji hatujayajua!


© 2011 Sammy Makilla

Hivi kazi nitapata?

Hivi kazi nitapata, mamangu hajulikani,
Barua nikizileta, kitu zitaaidia ?
Kitu gani nitaleta, hakika nayo nikawa,
Mamangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Ubavuni nikijata, kwa mama wa kufikia,
Hawawezi kunisuta, sio walionizaa,
Jina langu wakafuta, mitaani kutupiwa?
Mamangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Ubunge hakuupata, mama alipogombea,
Ufakiri kapakata, siwezi mtegemea,
Budi kazi kutafuta, pengine nitamsaidia,
Mamangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Hakujipaka mafuta, au mkorogo kutia,
Kwa watu hakunatanata, wakaweza mtambua,
Weusi ulimteta, mwangani hawakumjua,
Mamangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Uwaziri kaudata, kabaki kuusikia,
Na wakubwa hakuitwa, sio wa kuchagulia,
Umaskini anata, nani kumuangalia,
Mamangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Utajiri hakupata, ndugu kawasaidia,
Nyumbani tunachachata, mengi twabangaizia,
Walopata watusuta, nini tutawaambia?
Mamangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Najuta shemu Mjata, hali niliyofikia,
Nasaha naitafuta, waniachie na saa,
Twala wali wa mafuta, na nazi nilizoea?
Mamangu hajulikani, kazi naweza kupata?


© 2011 Sammy Makilla

Babangu hajulikani

Hivi kazi nitapata, babangu hajulikani,
Barua nikizileta, kitu zitaaidia ?
Kitu gani nitaleta, hakika nayo nikawa,
Babangu hajulikani, hivi kazi nitapata ?

Ubavuni nikijata, kwa baba wa kufikia,
Hawawezi kunisuta, sio walionizaa,
Jina langu wakafuta, mitaani kutupiwa?
Babangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Ubunge hakuupata, baba alipogombea,
Ufakiri kapakata, siwezi mtegemea,
Budi kazi kutafuta, pengine nitamsaidia,
Babangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Uwaziri kaudata, kabaki kuusikia,
Na wakubwa hakuitwa, sio wa kuchagulia,
Umaskini anata, nani kumuangalia,
Babangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Utajiri hakupata, ndugu kawasaidia,
Nyumbani tunachachata, mengi twabangaizia,
Walopata watusuta, nini tutawaambia?
Babangu hajulikani, kazi naweza kupata?

Najuta shemu Mjata, hali niliyofikia,
Nasaha naitafuta, waniachie na saa,
Twala wali wa mafuta, na nazi nilizoea?
Babangu hajulikani, kazi naweza kupata?


© 2011 Sammy Makilla

Msomi hathaminiwi

Hana kabisa thamani, wengine waogopewa,
Nani anayemwamini, shauri akalipewa,
Wote kwao mashetani, wao malaika wawa,
Msomi hathaminiwi, ndio yetu Tanzania!

Maamuzi yote nchini, wabovu wanatumiwa,
Na kilichokuwa duni, ndicho kinaamuliwa,
Kuuaga umaskini, hii nasema ruia,
Msomi huogopewa, ndio yetu Tanzania!

Ugiriki tazameni, zamani ilivyokua,
Uchina nako Romani, maamuzi wakitoa,
Ya wasomi ni amini, hayaachi kutumiwa,
Msomi hathaminiwi, ndio yetu Tanzania!

Na unayemthamini, haachi bora kuwa,
Mataifa duniani, hili wanalitambua,
Ni matofali auni, nchi kujaijengea,
Msomi huogopewa, ndio yetu Tanzania!

Akili walio dunia, hili hawatalijua,
Vingine hujiamini, hadi wakatumbukia,
Kulikoni mashimoni, vigumu kuokolewa,
Msomi hathaminiwi, ndio yetu Tanzania!

Ila walio makini, hili wanalielewa,
Wasomi huwathamini, na yao wakasikia,
Na kisha hutathmini, yalo bora kuamua,
Msomi huogopewa, ndio yetu Tanzania!

Nchi huwa mashakani, kuwa na wanaojua,
Kila kilicho uzani, maamuzi kuchukua,
Nchi huja walaani, wasiwe wa kukumbukiwa,
Msomi hathaminiwi, ndio yetu Tanzania!

Wape wetu wahisani, akili ziiizokua,
Waweze kuwaamini, washauri wa kufaa,
Nchi ipate thamani,kwa kile inachotumia,
Msomi huogopewa, ndio yetu Tanzania!


© 2011 Sammy Makilla

Thursday, December 29, 2011

Kesi vyombo vya habari, kuunyonga ushairi.

Jaji:

Wasimama mtuhumiwa, mshairi ashtakia,
Unainyonga sanaa, ushairi Tanzania,
Kila unachoamua, ushairi wapungua,
Ni kweli una hatia, au wanakuzulia?

Mshairi shtakia, wote tupate sikia,
Kilio unacholia, na wao wapate jua,
Hukumu kusaidiwa, nitapokuja kutoa,
Ni kweli watuambia, au unamzulia ?


Mshairi:

Asante mheshimiwa, shtaka kulichukua,
Kilio nitakitoa, wote wapate sikia,
Sina sababu kuzua, ukweli mwajionea,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Gazeti ukiangalia, hakuna wanachotoa,
Mengineyo yamejaa, hata yasiyotufaa,
Kila ukiulizia, ujinga unajibiwa,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Nafasi wasingizia, ila huo ni umbeya,
Wengine wajisemea, udini yaliyojaa,
Fani ni Muhamadia, pekee inawafaa,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Kuua wamenuia, ushairi Tanzania,
Kiswahili nacho pia, kukinyonga wapania,
Ili nchi yote kuwa, Kiingereza yatumia,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Redio zinachanua, pembe zote Tanzania,
Karibu kila mkoa, redio utasikia,
Ila wanatukataa, wachache isipokua,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Michezo waparamia, msukule wadhania,
Uhai kisichokua, ndio kinapaliliwa,
Ni mitini wamekaa, juha tawi wakalia,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Televisheni mpya, ndio kwanza zaingia,
Nani anafikiria, ushairi kuulea?
Picha mbaya watatoa, ushairi wataua,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Intaneti yabakia, sasa inasadiaia,
Ila waliojaliwa, ni wachache walokua,
Vijijini wazubaa, wahofu wabaguliwa,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Nchi imeshalemaa, yasota teknolojai,
Rwanda yatutangulia, nyuma sisi twabakia,
Labda tukizinduliwa, zaidi itatutaa,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Mashuleni waduwaa, vitabu vilivyochakaa,
Hakuna kazi mpya, za zamani watumia,
Watoto zawachefua, darasani wajitoa,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Pasipo kuzungumzia, yale wanayoyajua,
Tungo zikasimuliwa, wote zinazosisimua,
Ushairi utapwaya, na mwisho uje jifia,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Walimu wanaojua, hii feruzi sanaa,
Wachache wamebakia, wengi wameshajifia,
Kazi wanaopanvgiwa, bongo fleva watia,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

UKUTA wamebomoa, wakubwa waliokuwa,
Miaka yasahauliwa, hakuna wa kusaidia,
Wazeeka waliokuwa, damu mpya yatakiwa,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Baraza lilibuniwa, leo ladharauliwa,
Ofisi zimefubaa, kisirani imekua,
Hata kompyuta pia, hakuna ilobakia,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Ni wote tunachangia, ushairi kuua,
Ilo wanaoshindilia, wahariri walokua,
Watu wangejisomea, mbali wangekumbukia,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Watu wangeusikia, roho ingesisimua,
Mapya kufikira, tukaacha kudumaa,
Kiuweli tukakua, na sio kuongopea,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Jaji umenisikia, japo kwikwi yanivamia,
Ni ukweli nimetoa, mtu sikumsingizia,
Naomba kufikiria, hukumu ya kuamua,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Shahidi:
Hakika mheshimiwa, hivyo ndivyo ilivyokua,
Kweli tupu kaitoa, sinalo la kukataa,
Tafakari kuamua, kitakachotusaidia,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!


Wakili:


Na mimi Mtanzania, uongo ninachelea,
Nini nitakuambia, Jaji unayesimamia,
Kweli mwenzetu katoa, chembe haikupungua,
Wahariri wauaji, ushairi na mshairi!

Jaji:


Ni nini nitaongea, bila ya mimi kulia,
Hata na zetu sheria, bado zimeelemewa,
Kiswahili hazijawa, kila mtu akajua,
Ila ninawaachia, Watanzania kuamua!

Tumelogwa nadhania, bahati kutoijua,
Ya watu twashikilia, yetu tunayaachia,
Uchumi ungelikua, Kiswahili kutumia,
Ila ninawaachia, Watanzania kuamua!

Wednesday, December 28, 2011

Elfu mbili kumi na mbili

Ninanshukuru kwa umri Jalali
Uzima wa roho na kiwiliwili
Nimeona mwaka ningali kamili
Na siishtakii dhoofu hali
Inshanitangulia ya awali
Niliyopata ya kwangu ni kubuli
Niliyokosa si mali ni muhali
Akheri nimeanza kuikabili
Kwa dua kuomba na ibada kusali
Nakusihi Rahmani kutawakali
Kunionyesha ifaayo siratuli,
Uwe bora wangu mustakabali
Dini, uzima, afya, ulimi na hali
Elfu mbili kumi na mbili


© 2011 Sammy Makilla

Ninataka nikumbukwe

Nisikumbukwe vingine, katika hii dunia,
Zaidi watu wanene, ukweli niliulea,
Na kwa adha na mavune, daima sikuachia,
Ninataka nikumbukwe, nilikuwa ni mkweli.

Moja haikuwa nane, kwa nilivyoshuhudia,
Nane haikuwa nne, watu nilipowaambia,
Na mwembamba si mnene, katu sikumsifia,
Ninataka nikumbukwe, nilikuwa ni mkweli!

Naomba nisiubane, upana uliokua,
Na ukweli niuone, hata gizani ukiwa,
Wazaini niachane, hata nisipoambua,
Ninataka nikumbukwe, nilikuwa ni mkweli.

Nijaliwe tu kichane, mavuno ninayopewa,
La msanii nisisane, niwaachie vichaa,
Niukubali ujane, siku unaponijia,
Ninataka nikumbukwe, nilikuwa ni mkweli.

Nifanyanyo kifane, watu kikawasaidia,
Wanaokonda wanone, kwa siha pia afya,
Wasioona waone, na viziwi kusikia,
Ninataka nikumbukwe, nilikuwa ni mkweli.

Wanaoumwa na wapone, hata bila kutibiwa,
Uwalii nisigune, jina nikikabidhiwa,
Yafumukayo nishone, nisiachie kuachia,
Ninataka nikumbukwe, nilikuwa ni mkweli.

Kumbikumbi na senene, nyumbani kutumbukia,
Njia wenyewe waone, bila kuwafuatia,
Utukufu niuone, kwa kila ninachopewa,
Ninataka nikumbukwe, nilikuwa ni mkweli.

Wakiwashwa niwakune, utulivu kuwajia,
Wenye vidonda nishone, kwa mate kuyatumia,
Na asali niirine, na watu kuwapatia,
Ninataka nikumbukwe, nilikuwa ni mkweli.

Nilichopanda nivune, zaidi kutochukua,
Kisicho changu nikane, wenyewe kuwaachia,
Nafsi yangu inene, kweli dahari ikawa,
Ninataka nikumbukwe, nilikuwa ni mkweli.


© 2011 Sammy Makilla

Msingi umeshajengwa

Uchina na Malaysia, mamao wanamlea,
Tena wanajivunia, wazidi kuendelea,
Hatua waliyofikia, mama kawasaidia,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Majuha tuliokua, ung'eng;e twang'ang;ania,
Twadhania ni dunia, Kiingereza kujua,
Nchi zinadidimia, tutakujajionea,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Jioni imeshakua, magharibi yaingia,
Mashariki laanza jua, ndio kwanza latokea,
Na kwa wanalojijua, hili wataling'amua,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Mashariki kunafaa, kwenda kujinyanyua,
Magharibi kutembea, wataali kuja kuwa,
Vichache kuokotea, vya kuja kujazilia,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Hivyo tungelianzia, nyumbani kutia paa,
Kiswahili jua kua, havi vyuo kutumia,
Na kisha kufyonzea, maarifa yakakua,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Uchina ninawaambia, elimu zote watia,
Kwenye lugha watumia, kwa kazi na kufundishia,
Hakuna wasilojua, na wengi hawajawajua,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Malaysia nao pia, lugha wameipania,
Kote wanaitumia, toka huko chekechea,
Nini utachowambia, ksiwe kimalaysia?
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Sisi mama twamchezea, kwa rushwa kuzipokea,
Lugha kutoitumia, Kiingereza kubakia,
Hali wote tunajua, wazito kushikilia,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Ilivyo sasa dunia, lugha zao watumia,
Kisha wanazifungua, maabda zikajaa,
Lugha kufundishia, mbalimbali zilokua,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Lugha wana huchagua, ipi ya kuichukua,
Mbili tatu zinakua, zote vyema akajua,
Maabara hutumia, miezi michache waa,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Kizamani twabakia, miaka kuitumia,
Wenzetu fumba fumbua, lugha mpya hujua,
Maabara kutumia, shuleni zinazokaa,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Mkakati hutumia, dunia kuangazia,
Wapi kunakofaa, bidhaa kuzichukua,
Na elimu kuitwaa, enzi inazozifaa,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Ila budi kujaliwa, viongozi wakufaa,
Baraka wanaochukua, na uchaMungu kupewa,
Majina watakapewa, nyuma yawezayo bakia,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Na sio wapita njia, waigizao sanaa,
Wamekuja kutumia, na matumbo kuchumia,
Na sio kutumikia, watu wakawanyanyua,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Bishara ukizijua, Mola hukufunulia,
Za kuzipitia njia, watu uje kuwafaa,
Na lugha yao kukua, ikaikubali dunia,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

Aidhawanaotubia, naye kumgeukia,
Rehema zimemjaa, na huruma kajaliwa,
Wadogo huwasikia, kama wakubwa wakiwa,
Msingi umeshajengwa, nani kuendelea?

© 2011 Sammy Makilla

Kiswahili mama yetu

Uchina na Malaysia, mamao wanamlea,
Tena wanajivunia, wazidi kuendelea,
Hatua waliyofikia, mama kawasaidia,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Majuha tuliokua, ung'eng;e twang'ang;ania,
Twadhania ni dunia, Kiingereza kujua,
Nchi zinadidimia, tutakujajionea,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Jioni imeshakua, magharibi yaingia,
Mashariki laanza jua, ndio kwanza latokea,
Na kwa wanalojijua, hili wataling'amua,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Mashariki kunafaa, kwenda kujinyanyua,
Magharibi kutembea, wataali kuja kuwa,
Vichache kuokotea, vya kuja kujazilia,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Hivyo tungelianzia, nyumbani kutia paa,
Kiswahili jua kua, havi vyuo kutumia,
Na kisha kufyonzea, maarifa yakakua,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Uchina ninawaambia, elimu zote watia,
Kwenye lugha watumia, kwa kazi na kufundishia,
Hakuna wasilojua, na wengi hawajawajua,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Malaysia nao pia, lugha wameipania,
Kote wanaitumia, toka huko chekechea,
Nini utachowambia, ksiwe kimalaysia?
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Sisi mama twamchezea, kwa rushwa kuzipokea,
Lugha kutoitumia, Kiingereza kubakia,
Hali wote tunajua, wazito kushikilia,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Ilivyo sasa dunia, lugha zao watumia,
Kisha wanazifungua, maabda zikajaa,
Lugha kufundishia, mbalimbali zilokua,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Lugha wana huchagua, ipi ya kuichukua,
Mbili tatu zinakua, zote vyema akajua,
Maabara hutumia, miezi michache waa,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Kizamani twabakia, miaka kuitumia,
Wenzetu fumba fumbua, lugha mpya hujua,
Maabara kutumia, shuleni zinazokaa,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Mkakati hutumia, dunia kuangazia,
Wapi kunakofaa, bidhaa kuzichukua,
Na elimu kuitwaa, enzi inazozifaa,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Ila budi kujaliwa, viongozi wakufaa,
Baraka wanaochukua, na uchaMungu kupewa,
Majina watakapewa, nyuma yawezayo bakia,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Na sio wapita njia, waigizao sanaa,
Wamekuja kutumia, na matumbo kuchumia,
Na sio kutumikia, watu wakawanyanyua,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Bishara ukizijua, Mola hukufunulia,
Za kuzipitia njia, watu uje kuwafaa,
Na lugha yao kukua, ikaikubali dunia,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!

Aidhawanaotubia, naye kumgeukia,
Rehema zimemjaa, na huruma kajaliwa,
Wadogo huwasikia, kama wakubwa wakiwa,
Kiswahili wetu mama, wana tumemkimbia!



© 2011 Sammy Makilla

Mwafrika si fukara

Kila ukimchunguza, Mwafrika anaweza,
Kuna kinachomlemaza, maisha yakamkwaza,
Hakuna anayewaza, jambo hilo kutengeza,
Mwafrika si fukara, msaada yatulemaza!

Ukoloni wa kuzoza, watu walishamaliza,
Na tunachokibakiza, wakoloni waongoza,
Si watu wa kutengeza, bali juu kujikweza,
Mwafrika si fukara, msaada yatulemaza!

Kuzalisha si waweza, ila kula na kusaza,
Ni watu wa kumaliza, wala sio wa kuanza,
Kazi ni kubangaiza, wala si nchi kugeuza,
Mwafrika si fukara, msaada yatulemaza!

Sio watu wa kujaza, ila daima kupunguza,
Ni watu wa kupuuza, fanyeni mnayoweza,
Mzawa kimbia giza, mwenyewe kujiendeleza,
Mwafrika si fukara, msaada yatulemaza!

Miaka mtamaliza, mbele hamtajisogeza,
Viongozi wana funza, hawawezi kuongoza,
Ukubwa kwao ni chaza, kuvuna wasichotunza,
Mwafrika si fukara, msaada yatulemaza!

Someni mnaoangaza, na wengine kuwafunza,
Labda ije miujiza, Mzungbu keshawalemaza,
Neema itawaiza, kwa rushwa kuwapumbaza,
Mwafrika si fukara, msaada yatulemaza!

Sifa wanaojijaza, kusonga hawataweza,
Watu wa kufululiza, wenyewe wakajikuza,
Hutuacha tulipoanza,kama si kutudumaza,
Mwafrika si fukara, msaada yatulemaza!

Cha mzawa wanabeza, na Mzungu kumkuza,
Uchina inawabeza, na wengine kuwaiza,
Majuha wa kupumbaza, wengine wanawajuza,
Mwafrika si fukara, msaada yatulemaza!

Azizi unayeweza, tupe wasiolemazwa,
Nchi kuiendeleza, ugumu ukakatiza,
Ya heri kufululiza, hadi juu kutukweza,
Mwafrika si fukara, msaada yatulemaza!


© 2011 Sammy Makilla

Mwafrika anaweza

Kila ukimchunguza, Mwafrika anaweza,
Kuna kinachomlemaza, maisha yakamkwaza,
Hakuna anayewaza, jambo hilo kutengeza,
Mwafrika anaweza, Mzungu kamlemaza!

Ukoloni wa kuzoza, watu walishamaliza,
Na tunachokibakiza, wakoloni waongoza,
Si watu wa kutengeza, bali juu kujikweza,
Mwafrika anaweza, Mzungu kamlemaza!

Kuzalisha si waweza, ila kula na kusaza,
Ni watu wa kumaliza, wala sio wa kuanza,
Kazi ni kubangaiza, wala si nchi kugeuza,
Mwafrika anaweza, Mzungu kamlemaza!

Sio watu wa kujaza, ila daima kupunguza,
Ni watu wa kupuuza, fanyeni mnayoweza,
Mzawa kimbia giza, mwenyewe kujiendeleza,
Mwafrika anaweza, Mzungu kamlemaza!

Miaka mtamaliza, mbele hamtajisogeza,
Viongozi wana funza, hawawezi kuongoza,
Ukubwa kwao ni chaza, kuvuna wasichotunza,
Mwafrika anaweza, Mzungu kamlemaza!

Someni mnaoangaza, na wengine kuwafunza,
Labda ije miujiza, Mzungbu keshawalemaza,
Neema itawaiza, kwa rushwa kuwapumbaza,
Mwafrika anaweza, Mzungu kamlemaza!

Sifa wanaojijaza, kusonga hawataweza,
Watu wa kufululiza, wenyewe wakajikuza,
Hutuacha tulipoanza,kama si kutudumaza,
Mwafrika anaweza, Mzungu kamlemaza!

Cha mzawa wanabeza, na Mzungu kumkuza,
Uchina inawabeza, na wengine kuwaiza,
Majuha wa kupumbaza, wengine wanawajuza,
Mwafrika anaweza, Mzungu kamlemaza!

Azizi unayeweza, tupe wasiolemazwa,
Nchi kuiendeleza, ugumu ukakatiza,
Ya heri kufululiza, hadi juu kutukweza,
Mwafrika anaweza, Mzungu kamlemaza!

© 2011 Sammy Makilla

Mnaanza kudarizi

Mnaanza mashauzi, kuchuma hatujachuma,
Nchi mwageuza mbuzi, kuchuna bila huruma,
Mwajifanya ni wawazi, kumbe yenu yako nyuma,
Mnaanza kudarizi, kufuma hatujafuma?

Yalazimu bumbuwazi, kwa kila mwenye hekima,
Msitufanye viazi, Mbozi wanavyovilima,
Macho yetu yako wazi, na masikio yasema,
Mnaanza kudarizi, kufuma hatujafuma?

Midomo ni mapinduzi, kuikataa dhuluma,
Na sura ni machukizi, mtendayo siyo mema,
Tungelikuwa bazazi, basi nasi tusingesema,
Mnaanza kudarizi, kufuma hatujafuma?

Ucheshi na matanuzi, hayajaleta neema,
Mmetufanya ushuzi, wanuka ila lazima,
Lini nchi yake majenzi, yategemea wagema?
Mnaanza kudarizi, kufuma hatujafuma?

Zinachosha simulizi, kulima tulishalima,
Bidii haina hadhi, faida isipochuma.
Na juhudi ni ushenzi, kama yarudisha nyuma,
Mnaanza kudarizi, kufuma hatujafuma?

Utenzi na uteuzi, mambo yataka hekima,
Udugu hauna enzi, kwenye kazi utazama,
Na kazi bila ujuzi, hugeuka ni ujima,
Mnaanza kudarizi, kufuma hatujafuma?

Mshairi sina kazi, kazi yangu ni kupema,
Na pasipo pema mjuzi, kutangaza ni lazima,
Baa wanaodarizi, na walipo ni kuhama,
Mnaanza kudarizi, kufuma hatujafuma?

Namshukuru Mwenyezi, kuniwezesha kalima,
Pekee ndiye mwenye enzi, napanda akinituma,
Habari ziso ajizi, nimejuza maamuma,
Mnaanza kudarizi, kufuma hatujafuma?


© 2011 Sammy Makilla

Mzungu twampa dhahabu

Pu nguani wadhania, viongozi walokua,
Dhahabu tunaitoa, peremende twachukua,
Kusoma tumefulia, uchumi tunaogea,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!

Mababu hawakujua, sisi mbona tunajua,
Bado tunaendelea, na ileile tabia,
Hakika ninashangaa, viranja sijawajua,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!

Ni njaa yawasumbua, au wajinga majuha,
Mchele watoa gunia, wapokea kitumbua?
Hii laana imekua, mkono wa mtu nahofia,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!

Pamba bure unagawa, mtumba unanunua,
Miwa unaiachia, sukari nyeupe wapewa?
Sumu iliyokwishajaa, kifo hujakihofia,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!

Magurudumu bidhaa, mpira twajiuzia,
Madini twawaachia, wengine kujichimbia,
Wasomi tuliotoa, nje wameshahamia,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!

Wazungu sasa wajaa, tarafu wasiokua,
Amerika na Ulaya, utazoa kwa gunia,
Twabaki twashangaa, badala kuwachukua,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!

Reli kuja kufufua, na ndege zetu nazo pia,
Bandari kujijengea, watu wetu kutumia,
Akili ikilemaa, bofra mwili kulemaa,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!

Wasomi nje wajaa, kazi wanazililia,
Ukienda wachkua, viwanda utainua,
Na nchi juu ikawa, ya pili kwenye dunia,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!

Matatizo wangeondoa, na nchi kujitanua,
Akili wangezinoa, uburu ukajifia,
Tuanze kujichongea, mengi yenye kutufaa,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!

Uongozi twahofia, kulogwa uliokua,
Huna unalolijua, ila siasa kugwaya,
Nchi inadidimia, na wao washindilia,
Mzungu twampa dhahabu, sisi twakubali pipi!


© 2011 Sammy Makilla

Tanzania italia

Kichekesho kitakuwa, miaka ikitimia,
Watakuja elezea, Makilla alitwambia,
Vingine kumdhania, wala hatukumsikia,
Tanzania italia, Makilla aliyasema!

Kaburini nimetiwa, au majivu nishakua,
Wataamka wazawa, na maswali kuyazua,
Wakamaka kuibua, nilikwishawaaambia,
Tanzania italia, Makilla aliyasema!

Wajifanyao wajua, nchi wameshikilia,
Kipi kinachoendelea, ila uwizi wakua,
Utume sijaupewa, ila macho nafungua,
Tanzania italia, Makilla aliyasema!

Mengi nimeshuhudia, nami nikawambia,
Haifai hii njia, wenzangu kuipitia,
Dhihaka mkajitia, na safari kwendelea,
Tanzania italia, Makilla aliyasema!

Na hapa mlipofikia, watu waanza umia,
Kiu kimewazidia na njaa yazidi kua,
Nafuu hawajaijua, umauti walilia,
Tanzania italia, Makilla aliyasema!

Na juu waliokua, ukweli hawajajua,
Kama kama watanua, pepo yao ni dunia,
Siku ikiwashtukia, shinikizo kuwaua,
Tanzania italia, Makilla aliyasema!

Keki wanatangazia, watu wameshagaiwa,
Hali mkate ruia, hakuna anayeujua,
Hii siyo Tanzania, niliyokwisha kuijua,
Tanzania italia, Makilla aliyasema!

Rasilimali zapaa, Ulaya kuelekea,
Wenye mitaa ni njaa, kitu hawakupatiwa,
Madini yachukuliwa, ada kulipa balaa,
Tanzania italia, Makilla aliyasema!

Zahanati zimejaa, dawa chini zafukiwa,
Kila mtu analia, roho mbaya tumekua,
Ni nani asiyekuwa, hata wa juu walokua?
Tanzania italia, Makilla aliyasema!

Mshairi ninatua, mbele sintoendelea,
Mzigo niliochukua, hapa chini naachia,
Si mtu wa kuumia, pale pasipo na nia,
Tanzania italia, Makilla aliyasema!


© 2011 Sammy Makilla

Pasipo televisheni

Redio isipokua, vigumu kuendelea,
Hapatazungumziwa, matatizo yalokua,
Na jinsi ya kutatua, mkoa kuendelea,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Wapi watazungumzia, muhimu yaliyokua,
Hoja wakazisikia, na aula kuchagua,
Kisha kujajipangia, na bajeti kuandaa,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Mikakati kuamua, mkoa unaofaa,
Mbinu wakazichambua, kazi rahisi ikawa,
Miaka ikapungua, afueni kutokea,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Gazeti lisipokua, wajinga wanachanua,
Hoja hawatazijua, ndiyo wataitikia,
Viongozi huchagua, wale wasiowafaa,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Wananchi wataibiwa, kila chao kilokua,
Rasilimali hupaa, na mali asili pia,
Na fedha hukwapuliwa, mchana wajionea,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Tovuti isipokuwa, ni mji uliovia,
Watalii hukimbia, hapo tena hawatakaa,
Kwingine huelekea, mawasiliano yakawa,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Televisheni kupwaya, mji huja kudumaa,
Katu hautaendelea, utazidi kusinyaa,
Na vijana husanzua, jijini kukimbilia,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Simu zisipoenea, mawasiliano huvia,
Vijana hupakimbia, kwingine wakaingia,
Kamwe hawatasalia, hata ukiwafungia,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Wakati tumefikia, maamuzi kuamua,
Redio za umma kua, kila mji Tanzania,
Ya mji kuzungumzia, na yanayotarajiwa,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Magazeti nayo pia, kila mji yatakiwa,
Habari zao kujua, mambo kuchangamkia,
Ya wengine kusikia, kurasa zinazofatia,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Tovuti tunatakiwa, kila kona kuchanua,
Ukienda kutembea, Google wajipatia,
Migawaha maridhawa, huduma ikazitoa,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Televisheni mbia, picha inatupatia,
Ni mengi tunayojua, papo hapo kujionea,
Ziara kujifanzia, hali chumbani twakaa,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Wakale hawakujua, umuhimu ulokua,
Uongo walichelea, gizani tukabakia,
Alamu katujalia, sasa zaangazia,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Ila kinachotokea, uchafu zinachukua,
Bado hatujajitambua, wenyewe twajiumbua,
Viongozi watakiwa, hili kuliangalia,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Zingekuwa za mkoa, vyemja zingedhibitiwa,
Kumoja kutolemea, na kwingine kuonea,
Na wanaosimamia, umiliki kuchukua,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!

Muhimu yangelikuwa, yanayozungumziwa,
Miji ije kuchanua, kama Ulaya ikawa,
Ikang'ara Tanzania, hadi huko Malaysia,
Pasipo televisheni, wazainiwa hujaa!


© 2011 Sammy Makilla

Mji kukosa gazeti

Redio isipokua, vigumu kuendelea,
Hapatazungumziwa, matatizo yalokua,
Na jinsi ya kutatua, mkoa kuendelea,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Wapi watazungumzia, muhimu yaliyokua,
Hoja wakazisikia, na aula kuchagua,
Kisha kujajipangia, na bajeti kuandaa,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Mikakati kuamua, mkoa unaofaa,
Mbinu wakazichambua, kazi rahisi ikawa,
Miaka ikapungua, afueni kutokea,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Gazeti lisipokua, wajinga wanachanua,
Hoja hawatazijua, ndiyo wataitikia,
Viongozi huchagua, wale wasiowafaa,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Wananchi wataibiwa, kila chao kilokua,
Rasilimali hupaa, na mali asili pia,
Na fedha hukwapuliwa, mchana wajionea,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Tovuti isipokuwa, ni mji uliovia,
Watalii hukimbia, hapo tena hawatakaa,
Kwingine huelekea, mawasiliano yakawa,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Televisheni kupwaya, mji huja kudumaa,
Katu hautaendelea, utazidi kusinyaa,
Na vijana husanzua, jijini kukimbilia,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Simu zisipoenea, mawasiliano huvia,
Vijana hupakimbia, kwingine wakaingia,
Kamwe hawatasalia, hata ukiwafungia,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Wakati tumefikia, maamuzi kuamua,
Redio za umma kua, kila mji Tanzania,
Ya mji kuzungumzia, na yanayotarajiwa,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Magazeti nayo pia, kila mji yatakiwa,
Habari zao kujua, mambo kuchangamkia,
Ya wengine kusikia, kurasa zinazofatia,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Tovuti tunatakiwa, kila kona kuchanua,
Ukienda kutembea, Google wajipatia,
Migawaha maridhawa, huduma ikazitoa,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Televisheni mbia, picha inatupatia,
Ni mengi tunayojua, papo hapo kujionea,
Ziara kujifanzia, hali chumbani twakaa,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Wakale hawakujua, umuhimu ulokua,
Uongo walichelea, gizani tukabakia,
Alamu katujalia, sasa zaangazia,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Ila kinachotokea, uchafu zinachukua,
Bado hatujajitambua, wenyewe twajiumbua,
Viongozi watakiwa, hili kuliangalia,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Zingekuwa za mkoa, vyemja zingedhibitiwa,
Kumoja kutolemea, na kwingine kuonea,
Na wanaosimamia, umiliki kuchukua,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

Muhimu yangelikuwa, yanayozungumziwa,
Miji ije kuchanua, kama Ulaya ikawa,
Ikang'ara Tanzania, hadi huko Malaysia,
Mji kukosa gazeti, utatawala ujinga!

© 2011 Sammy Makilla

Mji kukosa tovuti

Redio isipokua, vigumu kuendelea,
Hapatazungumziwa, matatizo yalokua,
Na jinsi ya kutatua, mkoa kuendelea,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Wapi watazungumzia, muhimu yaliyokua,
Hoja wakazisikia, na aula kuchagua,
Kisha kujajipangia, na bajeti kuandaa,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Mikakati kuamua, mkoa unaofaa,
Mbinu wakazichambua, kazi rahisi ikawa,
Miaka ikapungua, afueni kutokea,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Gazeti lisipokua, wajinga wanachanua,
Hoja hawatazijua, ndiyo wataitikia,
Viongozi huchagua, wale wasiowafaa,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Wananchi wataibiwa, kila chao kilokua,
Rasilimali hupaa, na mali asili pia,
Na fedha hukwapuliwa, mchana wajionea,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Tovuti isipokuwa, ni mji uliovia,
Watalii hukimbia, hapo tena hawatakaa,
Kwingine huelekea, mawasiliano yakawa,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Televisheni kupwaya, mji huja kudumaa,
Katu hautaendelea, utazidi kusinyaa,
Na vijana husanzua, jijini kukimbilia,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Simu zisipoenea, mawasiliano huvia,
Vijana hupakimbia, kwingine wakaingia,
Kamwe hawatasalia, hata ukiwafungia,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Wakati tumefikia, maamuzi kuamua,
Redio za umma kua, kila mji Tanzania,
Ya mji kuzungumzia, na yanayotarajiwa,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Magazeti nayo pia, kila mji yatakiwa,
Habari zao kujua, mambo kuchangamkia,
Ya wengine kusikia, kurasa zinazofatia,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Tovuti tunatakiwa, kila kona kuchanua,
Ukienda kutembea, Google wajipatia,
Migawaha maridhawa, huduma ikazitoa,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Televisheni mbia, picha inatupatia,
Ni mengi tunayojua, papo hapo kujionea,
Ziara kujifanzia, hali chumbani twakaa,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Wakale hawakujua, umuhimu ulokua,
Uongo walichelea, gizani tukabakia,
Alamu katujalia, sasa zaangazia,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Ila kinachotokea, uchafu zinachukua,
Bado hatujajitambua, wenyewe twajiumbua,
Viongozi watakiwa, hili kuliangalia,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Zingekuwa za mkoa, vyemja zingedhibitiwa,
Kumoja kutolemea, na kwingine kuonea,
Na wanaosimamia, umiliki kuchukua,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!

Muhimu yangelikuwa, yanayozungumziwa,
Miji ije kuchanua, kama Ulaya ikawa,
Ikang'ara Tanzania, hadi huko Malaysia,
Mji kukosa tovuti, vigumu kuendelea!


© 2011 Sammy Makilla

Mji kukosa gazeti

Redio isipokua, vigumu kuendelea,
Hapatazungumziwa, matatizo yalokua,
Na jinsi ya kutatua, mkoa kuendelea,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Wapi watazungumzia, muhimu yaliyokua,
Hoja wakazisikia, na aula kuchagua,
Kisha kujajipangia, na bajeti kuandaa,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Mikakati kuamua, mkoa unaofaa,
Mbinu wakazichambua, kazi rahisi ikawa,
Miaka ikapungua, afueni kutokea,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Gazeti lisipokua, wajinga wanachanua,
Hoja hawatazijua, ndiyo wataitikia,
Viongozi huchagua, wale wasiowafaa,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Wananchi wataibiwa, kila chao kilokua,
Rasilimali hupaa, na mali asili pia,
Na fedha hukwapuliwa, mchana wajionea,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Tovuti isipokuwa, ni mji uliovia,
Watalii hukimbia, hapo tena hawatakaa,
Kwingine huelekea, mawasiliano yakawa,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Televisheni kupwaya, mji huja kudumaa,
Katu hautaendelea, utazidi kusinyaa,
Na vijana husanzua, jijini kukimbilia,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Simu zisipoenea, mawasiliano huvia,
Vijana hupakimbia, kwingine wakaingia,
Kamwe hawatasalia, hata ukiwafungia,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Wakati tumefikia, maamuzi kuamua,
Redio za umma kua, kila mji Tanzania,
Ya mji kuzungumzia, na yanayotarajiwa,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Magazeti nayo pia, kila mji yatakiwa,
Habari zao kujua, mambo kuchangamkia,
Ya wengine kusikia, kurasa zinazofatia,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Tovuti tunatakiwa, kila kona kuchanua,
Ukienda kutembea, Google wajipatia,
Migawaha maridhawa, huduma ikazitoa,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Televisheni mbia, picha inatupatia,
Ni mengi tunayojua, papo hapo kujionea,
Ziara kujifanzia, hali chumbani twakaa,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Wakale hawakujua, umuhimu ulokua,
Uongo walichelea, gizani tukabakia,
Alamu katujalia, sasa zaangazia,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Ila kinachotokea, uchafu zinachukua,
Bado hatujajitambua, wenyewe twajiumbua,
Viongozi watakiwa, hili kuliangalia,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Zingekuwa za mkoa, vyemja zingedhibitiwa,
Kumoja kutolemea, na kwingine kuonea,
Na wanaosimamia, umiliki kuchukua,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

Muhimu yangelikuwa, yanayozungumziwa,
Miji ije kuchanua, kama Ulaya ikawa,
Ikang'ara Tanzania, hadi huko Malaysia,
Mji kukosa gazeti, vigumu kuendelea!

© 2011 Sammy Makilla

Mji kukosa redio

Redio isipokua, vigumu kuendelea,
Hapatazungumziwa, matatizo yalokua,
Na jinsi ya kutatua, mkoa kuendelea,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Wapi watazungumzia, muhimu yaliyokua,
Hoja wakazisikia, na aula kuchagua,
Kisha kujajipangia, na bajeti kuandaa,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Mikakati kuamua, mkoa unaofaa,
Mbinu wakazichambua, kazi rahisi ikawa,
Miaka ikapungua, afueni kutokea,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Gazeti lisipokua, wajinga wanachanua,
Hoja hawatazijua, ndiyo wataitikia,
Viongozi huchagua, wale wasiowafaa,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Wananchi wataibiwa, kila chao kilokua,
Rasilimali hupaa, na mali asili pia,
Na fedha hukwapuliwa, mchana wajionea,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Tovuti isipokuwa, ni mji uliovia,
Watalii hukimbia, hapo tena hawatakaa,
Kwingine huelekea, mawasiliano yakawa,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Televisheni kupwaya, mji huja kudumaa,
Katu hautaendelea, utazidi kusinyaa,
Na vijana husanzua, jijini kukimbilia,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Simu zisipoenea, mawasiliano huvia,
Vijana hupakimbia, kwingine wakaingia,
Kamwe hawatasalia, hata ukiwafungia,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Wakati tumefikia, maamuzi kuamua,
Redio za umma kua, kila mji Tanzania,
Ya mji kuzungumzia, na yanayotarajiwa,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Magazeti nayo pia, kila mji yatakiwa,
Habari zao kujua, mambo kuchangamkia,
Ya wengine kusikia, kurasa zinazofatia,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Tovuti tunatakiwa, kila kona kuchanua,
Ukienda kutembea, Google wajipatia,
Migawaha maridhawa, huduma ikazitoa,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Televisheni mbia, picha inatupatia,
Ni mengi tunayojua, papo hapo kujionea,
Ziara kujifanzia, hali chumbani twakaa,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Wakale hawakujua, umuhimu ulokua,
Uongo walichelea, gizani tukabakia,
Alamu katujalia, sasa zaangazia,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Ila kinachotokea, uchafu zinachukua,
Bado hatujajitambua, wenyewe twajiumbua,
Viongozi watakiwa, hili kuliangalia,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Zingekuwa za mkoa, vyemja zingedhibitiwa,
Kumoja kutolemea, na kwingine kuonea,
Na wanaosimamia, umiliki kuchukua,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

Muhimu yangelikuwa, yanayozungumziwa,
Miji ije kuchanua, kama Ulaya ikawa,
Ikang'ara Tanzania, hadi huko Malaysia,
Mji kukosa redio, ni ndoto kuendelea!

© 2011 Sammy Makilla

Siri ya maendeleo

Lugha isipotumiwa, yakini kufundishia,
Nchi haitaendelea, wala kuja fanikiwa,
Matatizo yatakua, mikosi pia balaa,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Watawala walokuwa, wanadhania wanajua,
Kumbe mbali wapotea, na kuisahau njia,
Katu hawatatusaidia, ila watajisaidia,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

WATU waliojaliwa, lugha yao kutumia,
Katika hii dunia, ndio wanaendelea,
Watumwa waliokua, nyuma wanafuatia,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Mifano nakutolea, tokea Australia,
Wezi waliotimuliwa, bara wakahamishiwa,
Waingereza wakiwa, lugha wakaichukua,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Wazungu waliojaa, hapo chini Azania,
Kiingereza kufaa, lugha yao ilikuwa,
Afrikaans kuua, ukuu wakauchukua,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Hakuna palipobakia, sasa panaendelea,
Kwa lugha kuitumia, Kiingereza ilokuwa,
Itazame Nigeria, nayo Cameroun pia,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Unaijua Gambia, na vinavyowatokea,
Uganda na Kenya pia, nadhani wajititimua,
Ila kweli kwendelea, hilo sintatarajia,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Ghana wanajikakamua, mila zinawalemea,
Angalia Ethiopia, nao wanachanganyikiwa,
Na hivi sasa Somalia, nani atakujahamia?
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Afrika kulaaniwa, vya watu kung'ang'ania,
Vyake imeshajitupia, yabaki kujiokotea,
Haina lililokuwa, wala ililolijua,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Viongozi wanunuliwa, lugha ngeni kutumia,
Watu wao ukijua, ni ndogo asilimia,
Lugha wanaoijua, vipi wataendelea?
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Mizizi inatakiwa, maarifa nayo kua,
Hayawezi kuotea, chini isipochimbiwa,
Hunyauka na kuvia, nchi ikasinyaa,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Mbegu nimewaachia, kupanda mnatakiwa,
Viongozi mkipewa, macho waliofungua,
Uamuzi wa kufaa, nchi wakaamulia,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!

Miaka hamtakaa, ndege yenu itapaa,
Mtabaki kushangaa, kwanini mlichelewa,
Kumbe lugha kutokua, ni sababu ilokua,
Siri ya maendeleo, Kiswahili kutumia!


© 2011 Sammy Makilla

Siri ya maendeleo

WATU waliojaliwa, lugha yao kutumia,
Katika hii dunia, ndio wanaendelea,
Watumwa waliokua, nyuma wanafuatia,
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Mifano nakutolea, tokea Australia,
Wezi waliotimuliwa, bara wakahamishiwa,
Waingereza wakiwa, lugha wakaichukua,
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Wazungu waliojaa, hapo chini Azania,
Kiingereza kufaa, lugha yao ilikuwa,
Afrikaans kuua, ukuu wakauchukua,
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Hakuna palipobakia, sasa panaendelea,
Kwa lugha kuitumia, Kiingereza ilokuwa,
Itazame Nigeria, nayo Cameroun pia,
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Unaijua Gambia, na vinavyowatokea,
Uganda na Kenya pia, nadhani wajititimua,
Ila kweli kwendelea, hilo sintatarajia,
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Ghana wanajikakamua, mila zinawalemea,
Angalia Ethiopia, nao wanachanganyikiwa,
Na hivi sasa Somalia, nani atakujahamia?
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Afrika kulaaniwa, vya watu kung'ang'ania,
Vyake imeshajitupia, yabaki kujiokotea,
Haina lililokuwa, wala ililolijua,
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Viongozi wanunuliwa, lugha ngeni kutumia,
Watu wao ukijua, ni ndogo asilimia,
Lugha wanaoijua, vipi wataendelea?
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Mizizi inatakiwa, maarifa nayo kua,
Hayawezi kuotea, chini isipochimbiwa,
Hunyauka na kuvia, nchi ikasinyaa,
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Mbegu nimewaachia, kupanda mnatakiwa,
Viongozi mkipewa, macho waliofungua,
Uamuzi wa kufaa, nchi wakaamulia,
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

Miaka hamtakaa, ndege yenu itapaa,
Mtabaki kushangaa, kwanini mlichelewa,
Kumbe lugha kutokua, ni sababu ilokua,
Siri ya maendeleo, lugha yenu kutumia!

© 2011 Sammy Makilla

Uchina na Malaysia

Ukienda kwao jua, hili utafurahia,
Lugha wanajivunia, shuleni kuitumia,
Na vyuo vinachanua, lugha wanairingia,
Uchina na Malaysia, lugha wanajivunia!

Sitini tulianzia, masikini tulikuwa,
Wao walishang'amua, tatizo lililokua,
Wakalishughulikiwa, sawaswa kuliua,
Uchina na Malaysia, lugha wanajivunia!

Lugha walishatambua, si yao kuitumia,
Hivyo wakajaamua, makosa kuyaondoa,
Wakajipanga shujaa, elimu iwe kizawa,
Uchina na Malaysia, lugha wanajivunia!

Wachina wakachanua, vitabu kujitungia,
Kichina vikitumia, ili kuja fundishia,
Miaka hawakuchukua, kila kitu wakajua,
Uchina na Malaysia, lugha wanajivunia!

Wenzetu Malaysia, hayo waliyaamua,
Wakajitafsiria, kila wasichokijua
Kimalysia kuchukua, maarifa ya dunia,
Uchina na Malaysia, lugha wanajivunia!

Sasa lugha watumia, yao wenyewe wazawa,
Kila somo wanajua, kwa kazi na kufunzia,
Nchi yao inakua, dunia ya pili yawa,
Uchina na Malaysia, lugha wanajivunia!

Twadanganywa Tanzania, lugha ngeni kutumia,
Muda wazidi potea, nchi inachechemea,
Laiti tungelitumia, mbali tungelishakua,
Uchina na Malaysia, lugha wanajivunia!

Kujiuliza yafaa, elimu kwani ikawa?
Kama sio kutatua, matatizo yalokua,
Na fursa kutumia, ili watu kwendelea?
Uchina na Malaysia, lugha wanajivunia!


© 2011 Sammy Makilla

Kumbukumbu ya Malenga

Ningekujawachukua, minghairi sikujua,
Akheri kufikiria, ritadi nikahofia,
Nchi mngeikimbia, kwa jinsi ilivyokua,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Sanaa wanyanyapaa, hata serikali pia,
Bajeti waizuia, au inapanguliwa,
Baraza hoi jamaa, budi kuwahurumia,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki uk

Ushairi wachukia, wahariri Tanzania,
Waandishi nao pia, kung'ong'a waamriwa,
Hapajawa Tanzania, mhariri mashairi,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Ushairi wadhaniwa, ni ibada au dua,
Islamu unafaa, sio dini za judea,
Kiswahili nacho pia, ndio kisa chauawa,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Shaaban Robert, kweli nakusimulia,
Kama ungelifufuliwa, kuishi ungekataa,
Lugha ulivyoshikilia, wangekukatisha nia,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Amri Abeid pia, Mnyapala mngelia,
Kandoro mwenye kujua, ngonjera kuhadithia,
Hata nawe ungevia, kuishi kutorishia,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Mbovu metuachia, kwa kuondoka Mochiwa,
Ushairi wateketea, hakuna wa kuokoa,
Maprofesa waduwaa, na walimu nao pia,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Andanenga alijua, amebakia kulia,
UKUTA wabomoa, hapana pa kushikia,
Taasisi zinaliwa, hakuna zinachotoa,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Ugenini chahamia, Kiswahili cha wazawa,
Ksnya wasbangilia, ufalme kuchukua,
Marekani nayo pia, nyuma haijachelewa,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Japani wajivunia, Ujerumani wang'aa,
Uchina wakisikia, na Kusini wafundishia,
Uganda watangulia, nyuma yao twafatia,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Burundi wajenga paa, Rwanda wameshapaua,
Ndiko watakakotokea, mabingwa watakaokuwa,
Kizazi cha kufatia, sisi tukiangalia,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Kiswahili kinafia, hapa kilikozaliwa,
Hii yetu Tanzania, kizuri kisichojua,
Vya watu wang'ang'ania, hata kuzama nao pia,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Majonzi yatabakia, msiba watangulia,
Kaburi kulichimbua, Kiswahili kuzikia,
Nendeni mkifurahia, mimi nimeshajitoa,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!

Laana ninaikimbia, kizazi kitachojia,
Yenu ninawaachia, yangu ninayachukua,
Dunia kushuhudia, neno niliwaambia,
Kumbukumbu ya malenga, kilichobaki ukiwa!


© 2011 Sammy Makilla

Wasema wanisaidia

Uongo unauzua, eti unanigaia,
Hicho unachochukua, na mimi najipatia,
Unaidanganya haya, mwananme usiokua,
Wasema wanisaidia, kama wongo ulaniwe!

Mola ninamuachia, dhahiri kukusikia,
Kisha akajipimia, ukweli uliokua,
Kitu sijashuhudia, ila maneno naambiwa,
Wasema wanisaidia, kama wongo ulaniwe!

Waema wanisaidia, maana nishalemaa,
Tumboni umevimbiwa, vyote umeshavitia,
Aibu ungelijaliwa, haya usingetwambia,
Wasema wanisaidia, kama wongo ulaniwe!

Haywani weza kuwa, ni bora waheshimiwa,
Kuliko uliyekua, uongoa uliyejaa,
Na mimi nakuumbua, chako sijakipokea,
Wasema wanisaidia, kama wongo ulaniwe!

Moto wajipalilia, hujui lakuongea,
Mdomo ukifungua, uongo unaachia,
Mkweli hukuzaliwa, siwezi kutazamia,
Wasema wanisaidia, kama wongo ulaniwe!

Ukubwa twakuombea, na nafsi ije jaa,
Imani hukujaliwa, chukua yako dunia,
Tutakuja kuamua, ukija tuamkia,
Wasema wanisaidia, kama wongo ulaniwe!

Unaipenda dunia, haikupendi dunia,
Wewe waing'ang'ania, yenyewe itakuzoa,
Umejenga mazoea, mengine hutoelewa,
Wasema wanisaidia, kama wongo ulaniwe!

© 2011 Sammy Makilla

Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Ukubwa twakuombea, na nafsi ije jaa,
Imani hukujaliwa, chukua yako dunia,
Tutakuja kuamua, ukija tuamkia,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Unaipenda dunia, haikupendi dunia,
Wewe waing'ang'ania, yenyewe itakuzoa,
Umejenga mazoea, mengine hutoelewa,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

© 2011 Sammy Makilla

Uchi wanaotembea

Dunia inafichua, uchi wanaotembea,
Wenyewe wanashangaa, wanadhani wamevaa,
Kawaida imekua, ni vigumu kutambua,
Uchi wanaotembea, wadhani nguo wavaa!

Kitu wasioambiwa, wenyewe wajionea,
Watoto wameshakua, nage wawachezea,
Tikri waikataa, utani wanadhania,
Uchi wanaotembea, wadhani nguo wavaa!

Ujibari nahofia, hauwezi saidia,
Akili zilotulia, na malengo kuyajua,
Ndicho tunachotakiwa, kuanza kukitumia,
Uchi wanaotembea, wadhani nguo wavaa!

Huwezi ukatugawa, wazuri na wako wabaya,
Mbali hautofikia, kukwama utatitia,
Kazana macho fungua, ukweli utaujua,
Uchi wanaotembea, wadhani nguo wavaa!

Uongozi kuachia, vyenyewe hukurudia,
Kitu uking'ang'ania, mwenyewe utaumia,
Haya nimejionea, wana ninavyowalea,
Uchi wanaotembea, wadhani nguo wavaa!

Ilal ninalolijua, huwa halinayo dawa,
Sikio la kujifia, huwezi kuliokoa,
Wakati ukitimia, lazima kuangamia,
Uchi wanaotembea, wadhani nguo wavaa!

© 2011 Sammy Makilla

Wasema wanigaia

Uongo unauzua, eti unanigaia,
Hicho unachochukua, na mimi najipatia,
Unaidanganya haya, mwananme usiokua,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Mola ninamuachia, dhahiri kukusikia,
Kisha akajipimia, ukweli uliokua,
Kitu sijashuhudia, ila maneno naambiwa,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Waema wanisaidia, maana nishalemaa,
Tumboni umevimbiwa, vyote umeshavitia,
Aibu ungelijaliwa, haya usingetwambia,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Haywani weza kuwa, ni bora waheshimiwa,
Kuliko uliyekua, uongoa uliyejaa,
Na mimi nakuumbua, chako sijakipokea,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Moto wajipalilia, hujui lakuongea,
Mdomo ukifungua, uongo unaachia,
Mkweli hukuzaliwa, siwezi kutazamia,

© 2011 Sammy Makilla

Hayuko uongozini

Ni watoto wa mtaani, waongozao jahazi,
Kutanua yao fani, kelele na mashauzi,
Siamini yumkini, yumo mwenye utambuzi,
Hayuko uongozini, mtoto wa mkulima.

Kungelikuwa tauni, mwana kuwa kiongozi,
Tungeishi vijijini, afya isiwe ajizi,
Wangefurika wageni, kuja kuvuta pumzi,
Hayuko uongozini, mtoto wa mkulima.

Yangetiririka ndani, maji yaso uchafuzi,
Wanawake vijiini, isingelikuwa kazi,
Ngozi ziwe ni laini, wakaongeza mapenzi,
Hayuko uongozini, mtoto wa mkulima.

Kisegerema si shani, kingeliikosa kazi,
Mashine zije auni, mashambani na makazi,
Maisha yasiwe duni, wana wapate hifadhi,
Hayuko uongozini, mtoto wa mkulima.

Sanaa ninaamini, haya ni masimulizi,
Hayumo uongozini, mtoto wake mkwezi,
Ni watotowa mjini, vijiji kwao ushuzi,
Hayuko uongozini, mtoto wa mkulima.

Azuke aliamini, huko afanye makazi,
Apakimbie mjini, hadi watu kuwaenzi,
Kupambike vijijini, kwa kufuma na darizi,
Hayuko uongozini, mtoto wa mkulima.

Huduma ziwe amini, yatokee mapinduzi,
Wapendeze vijinini, mwnzo huu kuuenzi,
Tusifike duniani, kwa kutofanya ajizi,
Hayuko uongozini, mtoto wa mkulima.

© 2011 Sammy Makilla

Shaaban Robert

Laiti ungelizaliwa, nchi isiyolaaniwa,
Ubinafsi iliyojaa, wenyewe wanajifaa,
Wao wanapojifua, wengine wanafulia,
Shaaban Robert, kwenu hauthaminiwi,
Mshairi na mtunzi, dunia itakuenzi!

Hii leo ungekuwa, ni wetu Shakespeare,
Jina lingenyanyuliwa, kwenye minara likawa,
Kumbukumbu kujengewa, na vitabu vikajaa,
Shaaban Robert, kwenu hauthaminiwi,
Mshairi na mtunzi, dunia itakuenzi!

Kubwa lingelikuwa, Kiswahili kuenziwa,
Leo kingelitumiwa, vyuoni kufundishia,
Mbegu tukajipandia, asili zinazofaa,
Shaaban Robert, kwenu hauthaminiwi,
Mshairi na mtunzi, dunia itakuenzi!

Watumwa tusingekuwa, wengine tukawafaa,
Wavune wasichosia, na vyetu kuvichukua,
Vyote tungehifadhia, fasili ikavilea,
Shaaban Robert, kwenu hauthaminiwi,
Mshairi na mtunzi, dunia itakuenzi!

Nchi yazainiwa, ugeni kuutambia,
Rushwa inatumiwa, Kiingereza kukaa,
Na wajinga walokua, wadhania kitakua,
Shaaban Robert, kwenu hauthaminiwi,
Mshairi na mtunzi, dunia itakuenzi!

Giza laanza ingia, magharibi ilokua,
Hakuna anayejua, muda litakalokaa,
Ila kwa wanaojua, matlai wahamia,
Shaaban Robert, kwenu hauthaminiwi,
Mshairi na mtunzi, dunia itakuenzi!

Uchina ungefufuliwa, mwenyewe kujionea,
Lugha wanaitumia, na nchi yazidi kupaa,
Na huko Malaysia, nao wanaendelea,
Shaaban Robert, kwenu hauthaminiwi,
Mshairi na mtunzi, dunia itakuenzi!

Ni sisi tunakosea, njia tunayopitia,
Ujibari twajitia, taabu kukosolewa,
Ni ndoto ninahofia, umaskini kuondoa,
Shaaban Robert, kwenu hauthaminiwi,
Mshairi na mtunzi, dunia itakuenzi!

Usiache omba dua, wenyeji kuwazindua,
Wajifanya wanajua, kumbe wote ni majuha,
Bishara kutuombea, viranja wanaofaa,
Shaaban Robert, kwenu hauthaminiwi,
Mshairi na mtunzi, dunia itakuenzi!


© 2011 Sammy Makilla

Kumekucha

Kumekucha Alinacha, amkeni kunakuchwa,
Hali yazidi kuchacha, wanaongezeka mchwa,
Noeni meno na kucha, au milele mwafichwa,
Kumekucha shika ncha, au nyuma utaachwa!

© 2011 Sammy Makilla

Titi la mzazi tamu

Asili kitu adhimu, kuilea ni muhimu,
Taifa kutakadamu, kiini kutohasimu,
Kamwe kisijidhulumu, kikose ubinadamu,
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Kiswahili lugha tamu, yatia wengi wazimu,
Ila walio dhalimu, lugha wanaihasimu,
Mengine watakadamu, ya kwao wanahujumu,
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Wasahau ukarimu, kwenu kwanza ni muhimu,
Amri wanasalimu, kwa yasiyo ya adhimu,
Wageuzwa maimamu, dini wasioifahamu,
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Ni chemchemi adhamu, kubeba yetu muhimu,
Mizizi kutakadamu, maarifa utakimu,
Vizazi vije kwa zamu, kujifunza yao amu,
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Uchina wanafahamu, lugha sio marehemu,
Hakika wameazimu, masomo kuikirimu,
Maarifa yametimu, ndani yake yatadumu,
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Ya kwetu kama wazimu, hapana wataalamu,
Haya hayagharimu, ila kwao si muhimu,
Wenyewe wajidhulumu, kizazi kitawahukumu,
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Mipango hawaikimu, na mikakati adimu,
Watu hawajirehemu, waendako hawafahamu,
Utumwa waukirimu, udumu daima dawamu,
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Laiti wangefahamu, titi la mzazi litamu,
Lingine halishi hamu, hatga unyonye kwa zamu,
Makusudio adhimu, yangelikuwa azimu,
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Nauliza wahujumu, Kichina sio muhimu ?
Na Kiarabu adhimu, au huu Uislamu?
Kiingereza adimu, kitazidi kutukimu?
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Haijawadia zamu, Kichina kusoma humu,
Na shahada adhimu, waende kutukarimu?
Magharibi yake zamu, haijesha umuhimu?
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

Ninakuomba Rahimu, nchi hii kurehemu,
Yaliyo kwetu adhimu, yawe mambo maalumu,
Yapatiwe umuhimu, hadimu usigharimu,
Titi la mzazi tamu, lingine laisha hamu!

© 2011 Sammy Makilla

Ya wezi kaziye wizi

ZIMEFIKA zama hizi, hadhi wawe nayo wezi,
Na wakubwa majambazi, inshallah viongozi,
Walinzi wawe mijizi, wenye sheria hifadhi,
Mamlaka kama jizi, ya wezi kaziye wizi !

Na wa dini viongozi, kugeuka walanguzi,
Dini ziwe uchuuzi, bidhaa na matanuzi,
Busara iwe masinzi, na hekima kuwa nazi,
Mamlaka kama jizi, ya wezi kaziye wizi !

Malaya wawe wajuzi, wa kazi sio mapenzi,
Vyeo viwe fumanizi, wanone kimaangamizi,
Watajileta mabuzi, kuchinjwa kwenye makazi,
Mamlaka kama jizi, ya wezi kaziye wizi !

Ujaji huwa ni vazi, si utenzi bali hadhi,
Haki wawe wachuuzi, na wa chini dumuzi,
Yakaenea maradhi, pasiwe nayo hifadhi,
Mamlaka kama jizi, ya wezi kaziye wizi !

Wajinga wapewe kazi, na pengine uongozi,
Kazini kupanda ngazi, iwe kama utelezi,
Ufanisi jinamizi, kuzama isiwe kazi,
Mamlaka kma jizi, ya wezi kaziye wizi !

Waandishi na watunzi, wawe kwao waigizi,
Uongo waudarizi, liwe lao kuu vazi,
Keki likawa andazi, fumanizi, ugunduzi,
Mamlaka kama jizi, ya wezi kaziye wizi !

Urongo uwe ujuzi, wautaka viongozi,
Na umma kuwa zoezi, hadaa kuzimaizi,
Nchi isiwe majazi, bali shari na ajizi,
Mamlaka kama jizi, ya wezi kaziye wizi !

Kipendwacho kukabidhi, nusu yake maamuzi,
Ikafanza matanuzi, pato lenye ubaguzi,
Walewe utandawazi, na wa nje majambazi,
Mamlaka kma jizi, ya wezi kaziye wizi !

Huchaguliwa viazi, vikapika maandazi,
Na wasioenda kozi, wakawa ni wakufunzi,
Viatu kuwa kubadhi, wakavaa wanawenzi,
Mamlaka kama jizi, ya wezi kaziye wizi !

Wenye hoja kuwa mbuzi, waheshimiwa kwa ngozi,
Yakakwama mageuzi, uchama kushika uzi,
Tozo hili hatutozi, wajao watamaizi,
Mamlaka kama jizi, ya wezi kaziye wizi !

© 2011 Sammy Makilla

Monday, December 26, 2011

Harusi-2

1.
Msigeuze harusi, zikawa ni kivumbasi,
Isirafu damisi, kwa shehe na makasisi,
Mjukuu Ibilisi, kisirani na nuksi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
2.
Ndoa ibada halisi, walisema waasisi,
Jambo lataka kiasi, si kushibisha nafusi,
Haliafiki Qudusi, mwingi wa kutanafusi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
3.
Nikahi ni fahirisi, utangulizi hukisi,
Lakudumu majilisi, pasiwe na wasiwasi,
Kaskazi au kusi, vyote kupata nemsi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
4.
Ikifanywa kwayo kasi, ya riha na anisi,
Hutia doa jeusi, katika moyo mkwasi,
Na kuleta uyabisi, kila kiungo kuhisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
5.
Harusi kama libasi, wawili ni mahsusi,
Huleta hawa fususi, ya woto na utesi,
Hawapendwi maharusi, kipendwancho ni harusi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
6.
Hili lataka kiasi, hakika si wasiwasi,
Isirafu si nemsi, muulize Abunuwasi,
Na vitabu kadurusi, uone yake nakisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
7.
Harusi si kiharusi, jasho na wingi kamasi,
Lataka bora ususi, mambo yenu kuasisi,
Yasiyoleta nuksi, balaa nayo mikosi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
8.
Harusi kitu halisi, hakichanganywi najisi,
Haumo kwenye kamusi, uchafu nao utesi,
Vinginevyo wasiwasi, na mgeni Ibilisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
9.
Haitaki kandarasi, kuufanya uhandisi,
Huumeza ubinafsi, jumuiya kuasisi,
Ikawa yenye wepesi, umoja na urahisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
10.
Humkataa chunusi, anayezusha mikosi,
Huyakimbia maasi, kwa mbio zake farasi,
Ili kutunza asasi, na kumkana ibilisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
11.
Huchongwa moja libasi, ya kukaa maharusi,
Hawa zikatanafusi, huba ikawa msosi,
Pendo kuwa ni hadithi, simulizi kila mosi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
12.
Ila ikiwa najisi, haitokwisha mikosi,
Yatazidi na maasi, kusambaratika nafusi,
Ndoa ikawa nuksi, na familia kuhasi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.

Wapi Bunge la mkoa ?

Itazame Estonia, angalia Lithuania,
Nako pia Georgia, Urussi iliyokua,
Ilikuwa ni mikoa, sasa nchi zimekua,
Mikoa haitochanua, hadi huru kuja kuwa,
Wakubwa kutembelea, hilo halitasaidia,
Wapi bunge la mkoa, mikoa kuendelea?

Hofu iliyowajaa, chama wanakihofia,
Kwingi kitafagiliwa, hakinayo manufaa,
Waamka Watanzania, vipya watachagua,
Pembeni wakisogea, itaamka mikoa
Na ukubwa kurudia, si rahisi itakua,
Wapi bunge la mkoa, mikoa kuendelea?

Mikoa haitaibiwa, uhuru ikipatiwa,
Waziri Mkuu akiwa, bora atayaamua,
Mikoa haitachezewa, dhahabu wakagawa,
Misitu itaokolewa, na wanyama nao pia,
Vyanzo vya maji kua, salama kwa mamia,
Wapi bunge la mkoa, mikoa kuendelea?

Budi bunge la mkoa, mkoa kuzungumzia,
Sio kwa kututania, bali kwa kuazimia,
Maamzi kuamua, mbele yanayotufaa,
Kisha nasi kusogea, tusiwe wa kusinzia,
Uchumi kuunyanyua, hali bora tukajua
Wapi bunge la mkoa, mikoa kuendelea?

Jamii kusimamia, hadi ikajikomboa,
Nyumba kuasisia, kila mji zikajaa,
Vijiji kuwa vipya, watu wakajahamia,
Maendeleo kuzua, wageni kufurahia,
Wapi bunge la mkoa, mikoa kuendelea?

Nchi jirani zikawa, ni wake mkoa ubia,
Kuuza na kununua, bila ya kuzuiliwa,
Walanguzi kuwangoa, na kodi zenye udhia,
Unyonyaji kukataa, huria sote tukawa,
Wapi bunge la mkoa, mikoa kuendelea?

Wanaochelea tambua, hofu imewaingia,
Walichofanya wajua, vigumu kuvumiliwa,
Ukubwa walipopewa, nchi kama wameuziwa,
Wavuna wasikotia, na haramu kuchukua,
Siku itakapowadia, redioni kuvisikia,
Wapi bunge la mkoa, mikoa kuendelea?

Nchi zote za dunia, ushirika utakua,
Kuunyanyua mkoa, kwa biashara huria,
Na misaada kuingia, mkoa ikasaidia,
Mawaziri wakapewa, shughuli kuzifanyia,
Dar hazitoshia, wala tena kujaliwa,
Wapi bunge la mkoa, mikoa kuendelea?

Mikoa shule itakuwa, viongozi kufunziwa,
Uwaziri watajua, kwenye ngazi ya mkoa,
Miaka watakayokaa, nayo itahesabiwa,
Mazuri watakayotoa, kitaifa kutumiwa,
Nchi ikiwachagua, hawatajifunza jipya,
Wapi bunge la mkoa, mikoa kuendelea?

Daima niko na wewe

Wewe umkataaye
Shetani akikujia
Wahaka nao usiwe
Peke yako hutokua
Niko karibu na wewe
Nuru kukuangazia
Daima niko na wewe
Kama Mola uko naye!

Yetu hayakuwa yenu

Yetu hayakuwa yenu, panono mlidakia,
Ninasikia fununu, mnautaka ubia,
Cheo mmekichukua, si soda ilobakia?
Yetu hayakuwa yenu, na wala hayatakuwa.

Kwetu haikuwa mbinu, kitabu kilitambua,
Yalitetwa mawazinu, watu hawakusikia,
Viongozi wenye tanu, milango wakaachia,
Yetu hayakuwa yenu, na wala hayatakuwa.

Mchi haujawa kinu, na wala haitakuwa,
Pengine ikiwa tunu, kwa waliokwishajaliwa,
Kwani chao sio chenu, ila chenu hutumia,
Yetu hayakuwa yenu, na wala hayatakuwa.

Mkiwaachia yenu, ukwli wataujua,
Kudharau yao nunu, na watawanyanyapaa,
Muishiwe nazo mbinu, yenu mkayachukia,
Yetu hayakuwa yenu, na wala hayatakuwa.

Wenyewe wanazo menu, mambo yao kwa hatua,
Kuingia ndani mwenu, kisha kuwavurugia,
Mkawa hamna lenu, vyema linaloendelea,
Yetu hayakuwa yenu, na wala hayatakuwa.

Wanatumia upenu, kule mnakoegemea,
Wanunua watu wenu, na siri wanawaambia,
Kuna waitwao Manu, au Imma mtawajua,
Yetu hayakuwa yenu, na wala hayatakuwa.

Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

VIPI mtu anakua, kiongozi wa kufaa,
Bila kuchaguliwa, na mila kuzielewa,
Vyeo bure wanapewa, mikoa yadidimia,
Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

Mikoa yadhamiria, mbali kulifagilia,
Tunataka kuchagua, kiongozi wa mkoa,
Waziri mkuu kua, baraza akateua,
Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

Siasa zinatuua, twabeba visivyofaa,
Vyeo sasa tunagawa, pipi sasa imekua,
Wanaokutetemekea, ndio unawachagua,
Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

Wajuao kuzomea, ndio wanaotambuliwa,
Wawezao shangilia, ujinga hata ukiwa,
Na vigelegele pia, kweli watatuongoa?
Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

Mzigo tunanyanyua, usiotusaidia,
Uchafu wa kufagia, hazina tunautia,
Haya ninashangaa, hata mkinichukia,
Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

Uongozi si sanaa, ni ujuzi watakiwa,
Na mkuu wake mkoa, lazima kuchaguliwa,
Gavana ndiye akawa, waziri mkuu mkoa,
Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

Tunawajaza mamia, ofisi zetu mkoa,
Kazi hawakupangiwa, hakuna wanachojua,
Wakanyagana kwa kuwa, hawana cha kuamua,
Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

Vyeo pacha vimekua, mafuu tumeshakua,
Hakuna linaloendelea, fedha ila zinaliwa,
Mbele hatutasogea, hili likiachiliwa,
Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

Wakati wa kuamua, sasa imeshafikia,
Waziri Mkuu kua, si mkuu wa mkoa,
Baraza kusimamia, kma nchi kua mkoa,
Sasa waziri mkuu, si mkuu wa mkoa!

Viongozi kulakula

Uongozi nahofia, wivi waweza ukawa,
Kama wanaojipatia, wakubwa waliokuwa,
Wanyonge kudhulumiwa, na kidogo kuchukuliwa,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kiongozi akipewa, milioni kwa mamia,
Na hawa nao raia, kumi hawajaijua,
Huu sio wizi hua, mchna waendelea?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kumi na nane saa, daktari atumia,
Wagonjwa kuhudumia, bila hata kupumua,
Twashindwa kuwaangalia, wenyewe twajiangalia?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Nesi kote huingia, haishi kujichafua,
Matapishi hufadia, na vinyesi kuchukua,
Bungeni unayekaa, chote hicho wachukua?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Mwalimu choki yaja, machoni na kwenye pua,
Elimu anaitoa, kesho watakaomnyonyoa,
Hili twaliangalia, tunashindwa kuamua,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Sahani mbili mwatwaa, tonge hatujalijua,
Na kisha mwagugumia, hakiwatoshi mwaonewa,
Ibilisi mmekua, binadamu twadhania?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kipimo mnachotumia, mimi bado kukijua,
Kiasi gani mwatwaa, na kiasi gani mwatoa?
Nini mnakichukua, na nini mwatupatia?
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?


Au mwavuna mamia, hata msikopandia,
Kwingine mwakupua, vya wengine vilokua,
Hakika nawashangaa, watu msiojijua,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kwa haya mtachukia, ukweli nawaambia,
Mungu mkimtambua, mtageuka tabia,
Nafsi kuzizuia, wengine kuwatangulia,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Tazameni Malaysia, zamani walipoamua,
Viongozi kukataa, malipo yaliyozidia,
Wananchi kwanza kupewa, mtaji wakaendelea,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Kisha wao kufatia, nchi imeshanyanyuliwa,
Nyie mwanza kutwaa, nchi inadidimia,
Na Mola kawaumbua, mafuriko kutokea,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Sasa tunawashangaa, mwashindwa wajengea,
Hivi mnategemea, muujiza kutokea,
Fisadi walizochukua, kwanini kutotumiwa,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Nyumba ninawaambia, kwa fakiri ndio dawa,
Hili ukishampatia, mengine atajijua,
Ila mkiliachia, dhulumati tatajua,
Viongozi kulakula, hivi sio majambazi?

Uongozi nahofia, wivi waweza ukawa,
Kama wanaojipatia, wakubwa waliokuwa,
Wanyonge kudhulumiwa, na kidogo kuchukuliwa,

Kiongozi akipewa, milioni kwa mamia,
Na hawa nao raia, kumi hawajaijua,
Huu sio wizi hua, mchna waendelea?

Kumi na nane saa, daktari atumia,
Wagonjwa kuhudumia, bila hata kupumua,
Twashindwa kuwaangalia, wenyewe twajiangalia?

Nesi kote huingia, haishi kujichafua,
Matapishi hufadia, na vinyesi kuchukua,
Bungeni unayekaa, chote hicho wachukua?

Mwalimu choki yaja, machoni na kwenye pua,
Elimu anaitoa, kesho watakaomnyonyoa,
Hili twaliangalia, tunashindwa kuamua,

Sahani mbili mwatwaa, tonge hatujalijua,
Na kisha mwagugumia, hakiwatoshi mwaonewa,
Ibilisi mmekua, binadamu twadhania?

Kipimo mnachotumia, mimi bado kukijua,
Kiasi gani mwatwaa, na kiasi gani mwatoa?
Nini mnakichukua, na nini mwatupatia?

Au mwavuna mamia, hata msikopandia,
Kwingine mwakupua, vya wengine vilokua,
Hakika nawashangaa, watu msiojijua,

Kwa haya mtachukia, ukweli nawaambia,
Mungu mkimtambua, mtageuka tabia,
Nafsi kuzizuia, wengine kuwatangulia,

Tazameni Malaysia, zamani walipoamua,
Viongozi kukataa, malipo yaliyozidia,
Wananchi kwanza kupewa, mtaji wakaendelea,

Kisha wao kufatia, nchi imeshanyanyuliwa,
Nyie mwanza kutwaa, nchi inadidimia,
Na Mola kawaumbua, mafuriko kutokea,

Sasa tunawashangaa, mwashindwa wajengea,
Hivi mnategemea, muujiza kutokea,
Fisadi walizochukua, kwanini kutotumiwa,

Nyumba ninawaambia, kwa fakiri ndio dawa,
Hili ukishampatia, mengine atajijua,
Ila mkiliachia, dhulumati tatajua,

Viongozi ni wa nini?

Uongozi nahofia, wivi waweza ukawa,
Kama wanaojipatia, wakubwa waliokuwa,
Wanyonge kudhulumiwa, na kidogo kuchukuliwa,
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Kiongozi akipewa, milioni kwa mamia,
Na hawa nao raia, kumi hawajaijua,
Huu sio wizi hua, mchna waendelea?
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Kumi na nane saa, daktari atumia,
Wagonjwa kuhudumia, bila hata kupumua,
Twashindwa kuwaangalia, wenyewe twajiangalia?
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Nesi kote huingia, haishi kujichafua,
Matapishi hufadia, na vinyesi kuchukua,
Bungeni unayekaa, chote hicho wachukua?
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Mwalimu choki yaja, machoni na kwenye pua,
Elimu anaitoa, kesho watakaomnyonyoa,
Hili twaliangalia, tunashindwa kuamua,
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Sahani mbili mwatwaa, tonge hatujalijua,
Na kisha mwagugumia, hakiwatoshi mwaonewa,
Ibilisi mmekua, binadamu twadhania?
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Kipimo mnachotumia, mimi bado kukijua,
Kiasi gani mwatwaa, na kiasi gani mwatoa?
Nini mnakichukua, na nini mwatupatia?
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Au mwavuna mamia, hata msikopandia,
Kwingine mwakupua, vya wengine vilokua,
Hakika nawashangaa, watu msiojijua,
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Kwa haya mtachukia, ukweli nawaambia,
Mungu mkimtambua, mtageuka tabia,
Nafsi kuzizuia, wengine kuwatangulia,
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Tazameni Malaysia, zamani walipoamua,
Viongozi kukataa, malipo yaliyozidia,
Wananchi kwanza kupewa, mtaji wakaendelea,
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Kisha wao kufatia, nchi imeshanyanyuliwa,
Nyie mwanza kutwaa, nchi inadidimia,
Na Mola kawaumbua, mafuriko kutokea,
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Sasa tunawashangaa, mwashindwa wajengea,
Hivi mnategemea, muujiza kutokea,
Fisadi walizochukua, kwanini kutotumiwa,
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Nyumba ninawaambia, kwa fakiri ndio dawa,
Hili ukishampatia, mengine atajijua,
Ila mkiliachia, dhulumati tatajua,
Viongozi ni wa nini, ustawi kama hamna?

Uongozi ni wa nini?

Uongozi nahofia, wivi waweza ukawa,
Kama wanaojipatia, wakubwa waliokuwa,
Wanyonge kudhulumiwa, na kidogo kuchukuliwa,
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Kiongozi akipewa, milioni kwa mamia,
Na hawa nao raia, kumi hawajaijua,
Huu sio wizi hua, mchna waendelea?
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Kumi na nane saa, daktari atumia,
Wagonjwa kuhudumia, bila hata kupumua,
Twashindwa kuwaangalia, wenyewe twajiangalia?
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Nesi kote huingia, haishi kujichafua,
Matapishi hufadia, na vinyesi kuchukua,
Bungeni unayekaa, chote hicho wachukua?
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Mwalimu choki yaja, machoni na kwenye pua,
Elimu anaitoa, kesho watakaomnyonyoa,
Hili twaliangalia, tunashindwa kuamua,
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Sahani mbili mwatwaa, tonge hatujalijua,
Na kisha mwagugumia, hakiwatoshi mwaonewa,
Ibilisi mmekua, binadamu twadhania?
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Kipimo mnachotumia, mimi bado kukijua,
Kiasi gani mwatwaa, na kiasi gani mwatoa?
Nini mnakichukua, na nini mwatupatia?
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Au mwavuna mamia, hata msikopandia,
Kwingine mwakupua, vya wengine vilokua,
Hakika nawashangaa, watu msiojijua,
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Kwa haya mtachukia, ukweli nawaambia,
Mungu mkimtambua, mtageuka tabia,
Nafsi kuzizuia, wengine kuwatangulia,
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Tazameni Malaysia, zamani walipoamua,
Viongozi kukataa, malipo yaliyozidia,
Wananchi kwanza kupewa, mtaji wakaendelea,
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Kisha wao kufatia, nchi imeshanyanyuliwa,
Nyie mwanza kutwaa, nchi inadidimia,
Na Mola kawaumbua, mafuriko kutokea,
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Sasa tunawashangaa, mwashindwa wajengea,
Hivi mnategemea, muujiza kutokea,
Fisadi walizochukua, kwanini kutotumiwa,
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Nyumba ninawaambia, kwa fakiri ndio dawa,
Hili ukishampatia, mengine atajijua,
Ila mkiliachia, dhulumati tatajua,
Uongozi ni wa nini, kama watu hawapati?

Uongozi sio wizi ?

Uongozi nahofia, wivi waweza ukawa,
Kama wanaojipatia, wakubwa waliokuwa,
Wanyonge kudhulumiwa, na kidogo kuchukuliwa,
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Kiongozi akipewa, milioni kwa mamia,
Na hawa nao raia, kumi hawajaijua,
Huu sio wizi hua, mchna waendelea?
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Kumi na nane saa, daktari atumia,
Wagonjwa kuhudumia, bila hata kupumua,
Twashindwa kuwaangalia, wenyewe twajiangalia?
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Nesi kote huingia, haishi kujichafua,
Matapishi hufadia, na vinyesi kuchukua,
Bungeni unayekaa, chote hicho wachukua?
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Mwalimu choki yaja, machoni na kwenye pua,
Elimu anaitoa, kesho watakaomnyonyoa,
Hili twaliangalia, tunashindwa kuamua,
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Sahani mbili mwatwaa, tonge hatujalijua,
Na kisha mwagugumia, hakiwatoshi mwaonewa,
Ibilisi mmekua, binadamu twadhania?
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Kipimo mnachotumia, mimi bado kukijua,
Kiasi gani mwatwaa, na kiasi gani mwatoa?
Nini mnakichukua, na nini mwatupatia?
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Au mwavuna mamia, hata msikopandia,
Kwingine mwakupua, vya wengine vilokua,
Hakika nawashangaa, watu msiojijua,
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Kwa haya mtachukia, ukweli nawaambia,
Mungu mkimtambua, mtageuka tabia,
Nafsi kuzizuia, wengine kuwatangulia,
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Tazameni Malaysia, zamani walipoamua,
Viongozi kukataa, malipo yaliyozidia,
Wananchi kwanza kupewa, mtaji wakaendelea,
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Kisha wao kufatia, nchi imeshanyanyuliwa,
Nyie mwanza kutwaa, nchi inadidimia,
Na Mola kawaumbua, mafuriko kutokea,
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Sasa tunawashangaa, mwashindwa wajengea,
Hivi mnategemea, muujiza kutokea,
Fisadi walizochukua, kwanini kutotumiwa,
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Nyumba ninawaambia, kwa fakiri ndio dawa,
Hili ukishampatia, mengine atajijua,
Ila mkiliachia, dhulumati tatajua,
Uongozi sio wizi, kama wananchi wanakosa?

Hatatuangamizwa ila tutajiangamiza

Kweli Mwenyezi Mungu alitangaza
Ya kwamba tena hatatuangamiza
Ila katu kwetu vingine hakuvieleza
Kinyume kufanyika kinachoweza
Naye ni bwana wa kujuza na miujiza
Ndio maana nimeanza sasa kuuliza
Ndio kweli Mola tena hatatuangamiza
Lakini hivi aliwahi baadaye kutangaza
Binadamu tena katu 'hawatajiangamiza'
Na sio mikono yetu kazi hii itafanza
Ambayo hata bwana kasema haitampendeza?

Dar es salaam, Tanzania: +255787808539

Mti usio na shina

Shina limeondolewa, ni matawi yabakia,
Hivi mti utakua, na matunda kuyatoa,
Ningali ninahofia, hatima mbaya yajia,
Mti usio na shina, matawi kuuokoa?

Dharuba naisikia, juu inakotgokea,
Gharika nalihofia, chini lajititimua,
Mti umening'inia, vipi utajiokoa?
Mti usio na shina, matawi kuuokoa?

Tumaini sijaona, wasiwasi umejaa,
Hapana pa kujibana, wala pa kushikilia,
Labda nguvu ya Rabana, mti ukauokoa,
Mti usio na shina, matawi kuuokoa?

Wenyewe ulijiona, pekee uliokua,
Na haukushirikiana, na jirani walokua,
Hapakuwa muamana, kila kitu kuchukua,
Mti usio na shina, matawi kuuokoa?

Kimzani ulituna, kama sio kunona,
Ukiritimba hiyana, ukawa wake mwamana,
Na yanaposhindikana, sasa ni kutafutana,
Mti usio na shina, matawi kuuokoa?

Watu wanamalizana, ngawira kuja gawana,
Huku wajifanya wana, na baba hawakumuona,
Na majina wapeana, ukoo kujulikana,
Mti usio na shinda, matawi kuuokoa?

Ila haijajulikana, tufani inavyokazana,
Kama kuna kuokoana, au chini kutupana,
Nani kuangalizana, salamawaje iona,
Mti usio na shinda, matawi kuuokoa?

Siwezi zaidi nena, mimi siye ninayejua
Nahofia mame wana, chakula kutoungua,
Bei kimepanda sana, twaweza lala lna njaa,
Mti usio na shinda, matawi kuuokoa?

Chama chabaki matawi

Matawi yamebakia, mizizi wameing'oa,
Swali linanivamia, kuwepo kitaendelea?
Na wanaoning'inia, ni hao wa kulipiwa,
Chama chabaki matawi, mizizi wamesanzua!

Chama juu chaanzia, kura kujitafutia,
Mizizi haikukua, kwani haikujiotea,
Wajanja walishang'oa, walokuwa haramia,
Chama chabaki matawi, mizizi wamesanzua!

Chama kimechukuliwa, na wasokuwa wazawa,
Kwa malengo fisadia, watu na nchi kuvia,
Wakaneemeka wazoa, na wanaowapigania,
Chama chabaki matawi, mizizi wamesanzua!

Wakubwa wamepokea, hicho walichokipewa,
Pembeni wakasogea, vyao kwao kuanzia,
Mengi wamejijgengea, kama sio kukupua,
Chama chabaki matawi, mizizi wamesanzua!

Chini wameachiwa, vidogo kuvitumia
Hakuna kinachoingia, chama kikakitumia
Vyote watu hujilia, na juu kuongezewa,
Chama chabaki matawi, mizizi wamesanzua!

Kikichwa kinachokua, ni nani anakitoa,
Nini anajipatia, na vipi asaidia,
Au tumeishanunuliwa, jina tu linabakia?
Chama chabaki matawi, mizizi wamesanzua!

Na macho tusipokua, wallahi tutaumia,
Kifo hatutakijia, saa kitakapotokea,
Hugeukwa na wategemewa, tukabaki tunalia,
Chama chabaki matawi, mizizi wamesanzua!

Kiungo chako kibovu

Kiungo hakina kazi, kuwa navyo ni mzozo,
Watakiwa uamuzi, kupunguza shinikizo,
Apatikane mchuuzi, akufanyie mauzo,
Kiungo chako kibovu, wang'ang'ana kisitoke??

Usiifanye ajizi, zitakwisha pumzizo,
Ubakie ni wajuzi, kwenye haya mazungumzo,
Hali ilikuwa wazi, siku ulikuwa nazo,
Kiungo chako kibovu, wang'ang'ana kisitoke??

Halihitaji ujuzi, liwazi tokea mwanzo,
Ukifanya ubazazi, hufanywa ya mawe nguzo,
Ukabaki simulizi, au pengine tangazo,
Kiungo chako kibovu, wang'ang'ana kisitoke?

Yatakiwa mageuzi, na sio mazungumzo,
Maneno ni upuuzi, zama hizi za chetezo,
Moshi haunao kazi, yatakiwa ya mkazo,
Kiungo chako kibovu, wang'ang'ana kisitoke?

Alama zashehenezi, au kwako maigizo,
Hii ngoma ya maswezi, eti kwako ni mchezo?
Isiwe hatuyawezi, pakatokea uozo,
Kiungo chako kibovu, wang'ang'ana kisitoke?

Mengi yataka kimbizo, mwenzetu wazidi pozi,
Hulijui shinikizo, halinalo kizuizi?
Usituseme kikwazo, kumbe wewe kizuizi,
Kiungo chako kibovu, wang'ang'ana kisitoke?

Figo hazifanyi kazi

Figo hazinayo kazi, hustahili kuwa nazo,
Watakiwa uamuzi, kuuongoa mzozo,
Apatikane mchuuzi, akufanyie mauzo,
Figo hazifanyi kazi, wang'ang'ana kuwa nazo?

Usiifanye ajizi, zitakwisha pumzizo,
Ubakie ni wajuzi, kwenye haya mazungumzo,
Hali ilikuwa wazi, siku ulikuwa nazo,
Figo hazifanyi kazi, wang'ang'ana kuwa nazo?

Halihitaji ujuzi, liwazi tokea mwanzo,
Ukifanya ubazazi, hufanywa ya mawe nguzo,
Ukabaki simulizi, au pengine tangazo,
Figo hazifanyi kazi, wang'ang'ana kuwa nazo?

Yatakiwa mageuzi, na sio mazungumzo,
Maneno ni upuuzi, zama hizi za chetezo,
Moshi haunao kazi, yatakiwa ya mkazo,
Figo hazifanyi kazi, wang'ang'ana kuwa nazo?

Alama zashehenezi, au kwako maigizo,
Hii ngoma ya maswezi, eti kwako ni mchezo?
Isiwe hatuyawezi, pakatokea uozo,
Figo hazifanyi kazi, wang'ang'ana kuwa nazo?

Mengi yataka kimbizo, mwenzetu wazidi pozi,
Hulijui shinikizo, halinalo kizuizi?
Usituseme kikwazo, kumbe wewe kizuizi,
Figo hazifanyi kazi, wang'ang'ana kuwa nazo?

Huchelea la wokovu

Binadamu kumjua, bahati tunatumia,
Mgumju kumuelewa, moyoni yanayojaa,
Na unavyomdhania, ndivyo sivyo mara hua,
La wokofu huchelea, kila muogopa kifo!

Na ndivyo wanavyokua, unaotaka wafaa,
Iwe ni kuwaokoa, na dhiki unazojua,
Au balaa kuvaa, watakayoijutia,
La wokofu huchelea, kila muogopa kifo!

Wengi watakuhofia, wataka kuwachezea,
Husikiza ukajua, tayari wamesikia,
Kumbe hawakusikia, bado wanafikiria,
La wokofu huchelea, kila muogopa kifo!

Huchelea ya kufaa, tena ya kuwaongoa,
Mengine kuvamia, yatakayowaumbua,
Wakabaki washangaa, nusura kutoijua,
La wokofu huchelea, kila muogopa kifo!

Roho nimesharidhia, nasaha nitaitoa,
Na watakaosikia, sudi yao kusikia,
Wakiweza kutumia, watu huja kuwafaa,
La wokofu huchelea, kila muogopa kifo!

Waliokwishalaaniwa, jangwa ninawaachia,
Bure watanichukia, mengine wakidhania,
Ukweli wakiujua, watakuja nililia,
La wokofu huchelea, kila muogopa kifo!

Heri ninawatakia, kwa ukweli kuutoa,
Wao wanajihadaa, uongo kuutumia,
Blanketi la baa, maafa linaozua,
La wokofu huchelea, kila muogopa kifo!

Bure nisingejisumbua, ubaya ninaujua,
Nyuma ningeshaingia, na sifakuwasifia,
Na wao wakadhania, haki wanashikilia,
La wokofu huchelea, kila muogopa kifo!

Ila riha nakataa, na uongo kuzua,
Hata akiwa adawa, adili naangalia,
Na hao wasiojua, shetani awachezea,
La wokofu huchelea, kila muogopa kifo!

Hii ni tamu ya ndoa

Mwenzio hutamjua, kila anachofikiria,
Hilo ukilitambua, mengine unaachia,
Hukubali majaliwa, na kile kitakachokua,
Hii ni tamu ya ndoa, vinginevyo haikai.

Haiwi mkawa kimoya, ni viwili vinakua,
Mwenzio anachojua, sicho unachokijua,
Na akli sio sawa, wengine wanazidiwa,
Hii ni tamu ya ndoa, vinginevyo haikai.

Imani waliojaa, Mola kuwatangulia,
Sala wanaozijua, kwa wakati kutimia,
Na dua wanaotoa, muafaka na sawia,
Hii ni tamu ya ndoa, vinginevyo haikai.

Ibada waliojaa, na Mola kumwangukia,
Vitabu kujisomea, vitukufu vilokua,
Nuru huwatangulia, yalo bora kuamua,
Hii ni tamu ya ndoa, vinginevyo haikai.

Wajibu huutambua, na haki hatochagua,
Na mema hukazania, baraka zikaingia,
Huruma huwa wajaa, wengine kusaidia,
Hii ni tamu ya ndoa, vinginevyo haikai.

Na mengi huyagundua, ndoani yasiyofaa,
Wakajifunza radhia, kutenda na kuamua,
Na siku zote mashallah, kweli hawatachelea,
Hii ni tamu ya ndoa, vinginevyo haikai.

Ndipo nikawafunulia:
Akipanda wewe shuka
Akifukua wewe zika
Akifoka wewe toka
Akibweka wewe wika,
Akijifanya mzuka
Wewe kitanda tandika
Na kisha lala na kuamka
Salama utasalimika!

Na tena:
Ulimi silaha mbaya,
Mwenye nayo humuua,
Adawa akabakia,
Ulimi unabomoa,
Juu hautakunyanyua
Ila ukishaamua
Kwa heri kuutumia
Hata nyoka humtoa
Pangoni alimokaa
Na mwenye nia mbaya
Wa kheri mtu kuja kuwa!

Kiongozi mbaya heri

Kwa wasiojitambua, hudhani wamelaniwa,
Mbaya wanapopewa, kiongozi alokua,
Kisirani kikakua, na nia zikawa mbaya,
Kiongozi mbaya heri, mzuri ndipo hutafutwa!

Kiongozi mkipewa, kama Sauli akawa,
Kwa wanaojua biblia, torati kujisomea,
Zaburi haikukawia, maneno nayo yatia,
Kiongozi mbaya heri, mzuri ndipo hutafutwa!

Daudi alipokuwa, ngazi hakupigania,
Moyo ulimtulia, ya bwana akingojea,
Ila ilipofikia, mawili yote kapewa,
Kiongozi mbaya heri, mzuri ndipo hutafutwa!

Sauli alizidia, kwa dhuluma na ubaya,
Mola akamsanzua, Daudi kumchagua,
Ufalme akatwaa, na unabii kupewa,
Kiongozi mbaya heri, mzuri ndipo hutafutwa!

Kiongozi mbaya heri, mzuri ndipo hutafutwa!

Nchi ikatengemaa, na uovu kupungua,
Heri haikumbia, bali kuwakimbilia,
Uyahudi ikakua, na mipaka kupanua,
Kiongozi mbaya heri, mzuri ndipo hutafutwa!

Nchi ikijaliwa, kiongozi asofaa,
Ukubwa nayo tamaa, ikawa ni yake nia,
Asifanye cha kufaa, na watu kudidimia,
Kiongozi mbaya heri, mzuri ndipo hutafutwa!

Watu wakijitambua, na Mola kumgeukia,
Dini zikidhamiria, ibada zikachanua,
Mola atawasikia, na majibu kuyatoa,
Kiongozi mbaya heri, mzuri ndipo hutafutwa!

Yarabi twakulilia, kuangalia wasaa,
Ni wewe unayejua, si wafanzao kujua,
Huruma twaingojea, afu kuonyesha njia,
Kiongozi mbaya heri, mzuri ndipo hutafutwa!

Kila giza likizidi

Hii ni yake tabia, tuijuayo dunia,
Uovu unapochanua, nuru inakaribia,
Wanapojaa wabaya, wema ndio wazaliwa,
Kila giza likizidi, nuru itachungulia.

Giza likipalilia, kila kona kuenea,
Mwanga nyuma hufatia, giza ukaliondoa,
Shari inapozagaa, heri njiani kuingia,
Kila giza likizidi, nuru itachungulia.

Ni ajabu ya dunia, ndivyo hivyo milenia,
Na wasiojielewa, njiani hukata tamaa,
Kumbe nusura hatua, wala haijafikia,
Kila giza likizidi, nuru itachungulia.

Ukweli ukiujua, subira utailea,
Na hatima kukimbia, mbaya iliyolaniwa,
Mustakabali ukawa, pepo kujipalilia,
Kila giza likizidi, nuru itachungulia.

Nchi inapojaa, machungu pia ukiwa,
Uongozi kutanua, na watu kuwasiginia,
Hufika wakati kuwa, afueni wakapewa,
Kila giza likizidi, nuru itachungulia.

Siri anayoijua, Muumba tu nakwambia,
Wengine watabiria, kile kisichotokea,
Na ya kwao kupangia, bahari kutarajia,
Kila giza likizidi, nuru itachungulia.

Nilipo sijapajua, niendapo sijajua,
Ila ninachokijua, wajibu nimenuia,
Macho wote kufungua, dunia mkaijua,
Kila giza likizidi, nuru itachungulia.

Marafiki wa shetani

Marafiki wa shetani, hawakai penye jema,
Kazi yao uzaini, ukweli hawatasema,
Usiku ni mumiani, machana ni watu wema,
Marafiki wa shetani, huogopa malaika.

Ufasidi ni auni, huwasaidia njama,
Mikakati wakibuni, imefurika dhuluma,
Mipango yao uhuni, nchi na watu hukwama,
Marafiki wa shetani, huogopa malaika.

Tasnia wakibuni, himaya hujijengea,
Waishi wakiamini, hawatakutangulia,
Awasgabgaa Manani, ruia haziamini,
Marafiki wa shetani, huogopa malaika.

Nawe usiwaamini, au watakutumia,
Hiyo ndiyo yao dini, wataka kuabudiwa,
Ukimkana shetani, hatia watakutia,
Marafiki wa shetani, huogopa malaika.

Wapo tele waumini, na viongozi wajaa,
Anzia misikitini, hadi kanisani pia,
Wanafiki kwa yakini, Muumba keshawaumbua,
Marafiki wa shetani, huogopa malaika.

Hugeuza duniani, pepo yao ya kukaa,
Wakamdhihaki Bathini, kiyama kukitania,
Na wengi hujiamini, kumbe wameshapotea,
Marafiki wa shetani, huogopa malaika.

Wakiitwa mashakani, kama watoto hulia,
Daima hawaamini, dunia itawakataa,
Mateke wakibaini, mshtuko huwaua,
Marafiki wa shetani, huogopa malaika.

Siku hawaiamini, Ziraili akitua,
Kisha huganda moyoni, na mwilini nako pia,
Mate huisha kinywani, na kauli kupotea,
Marafiki wa shetani, huogopa malaika.

Awe adui shetani, Mola ikubali dua,
Niepushe mitihani, salamani nikakaa,
Mwisho uwe ni auni, daraja linalofaa,
Marafiki wa shetani, huogopa malaika.

Wahariri wanaua

Wahariri Tanzania, mashairi wanaua,
Fani wanyanyapaa, imebakia ukiwa,
Washairi wanalia, wapi wende kuhamia?
Wahariri wanaua, sanaa hya mashairi!

Rai na Mtanzania, kama hivi hamkua,
Uhuru mnazidiwa, hamu inatupungua,
Mwananchi mwasuasua, yakini hatujajua,
Wahariri wanaua, sanaa hya mashairi!

Tanzania daima pia, pembeni twapembuliwa,
Mzalendo lafifia, imebaki kusifia,
Nipashe si tena shua, vingine mnaamua,
Wahariri wanaua, sanaa hya mashairi!

Majira tuliyoijua, ni jina limebakia,
Sanaa ilikoanzia, ndiko sasa inafia,
Laiti wangetambua, yapasa kule kurejea,
Wahariri wanaua, sanaa hya mashairi!

Wadaku wanaodakia, kudokoa wazoea,
Utitiri umejaa, maudhi isofaa,
Nchi bado yawalea, kubaya twaelekea,
Wahariri wanaua, sanaa hya mashairi!

Redio zimesheenea, mashairi wazuia,
Sipati kuyasikia, wala kuzungumziwa,
Lugha wanaoiua, ushairi waanzia,
Wahariri wanaua, sanaa hya mashairi!

Televisheni zajaa, ushairi wafukiwa,
Hakuna historia, wala mfano wa sanaa,
Ya nje twayasikia, ndani yadharauliwa,
Wahariri wanaua, sanaa hya mashairi!

Tovuti naitumia, hifadhi bora ikawa,
Nyuma wakiifungua, sanaa watafukua,
Kimya hatukukaa, wengine tuliyatoa,
Wahariri wanaua, sanaa hya mashairi!

Ushairi ukivia, lugha nayo hudumaa,
KIsha huweza lemaa, isije tena kukua,
Watu wabaki kulia, hakuna cha kuokoa,
Wahariri wanaua, sanaa hya mashairi!