Monday, December 26, 2011

Hatatuangamizwa ila tutajiangamiza

Kweli Mwenyezi Mungu alitangaza
Ya kwamba tena hatatuangamiza
Ila katu kwetu vingine hakuvieleza
Kinyume kufanyika kinachoweza
Naye ni bwana wa kujuza na miujiza
Ndio maana nimeanza sasa kuuliza
Ndio kweli Mola tena hatatuangamiza
Lakini hivi aliwahi baadaye kutangaza
Binadamu tena katu 'hawatajiangamiza'
Na sio mikono yetu kazi hii itafanza
Ambayo hata bwana kasema haitampendeza?

Dar es salaam, Tanzania: +255787808539

No comments: