Saturday, December 29, 2012

Maneno tumeshashiba



KUSHIBA hamkuchelewa, ukubwa mlipopewa,
Vipit mwatutarajia, sisi tuwe twangojea ?
Mwenye shibe nimejua, hamjui  mwenye njaa,
Maneno tumeshashiba, tuna njaa ya vitendo.

Watu wamevumilia, sasa wajitapikia,
Nusura wakingojea, miaka ikaishia,
Uzee wakaingia, na wengine kujifia,
Maneno tumeshashiba, tuna njaa ya vitendo.

Wachoka Watanzania, wachche kujishibia,
Kisha wao kuambiwa, watakiwa kungojea,
Kingine kupakuliwa, mwaka ukisharejea,
Maneno tumeshashiba, tuna njaa ya vitendo.

Dhihaka wajionea, mingine kuingojea,
Leo leo vyatakiwa, uhaini kuwafaa,
Sio kuwangojea, maiti wameshakuwa,
Maneno tumeshashiba, tuna njaa ya vitendo.

Kitu hawatasikia, subira kutambuliwa,
Neno wanalingojea, kazi ikishatimia,
Miliki kuichukua, kufaidi manufaa,
Maneno tumeshashiba, tuna njaa ya vitendo.

Tena hawatangojea, kaya kujahadithiwa,
Wanataka kutumiwa, funguo za kufungua,
 Makasha yameshajaa, wenyewe wakachagua,
Maneno tumeshashiba, tuna njaa ya vitendo.

Vingine wataamua, vingine kuviondoa,
Usafi wakajitia, hadi mwaji kujimwagia,
Manukato wakatia, harufu kuziondoa,
Maneno tumeshashiba, tuna njaa ya vitendo.

Ubani kufukuzia, uoza ukafukiwa,
Pale wakijitambua, na dhamana kuitwaa,
Wawe wanajivunia, nchi yao imekuwa,
Maneno tumeshashiba, tuna njaa ya vitendo.




Kweli mwalimu dunia



Ukweli akikwambia, kujali unatakiwa,
Somo ameliandaa, na dunia aijua,
Wewe ukalikataa, mwenyewe utaumia,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!

Uongo akikwambia, fupi huwa yake njia,
Wewe ukauchagua, maisha kukusaidia,
Hatua itafikia, ukweli ukatambua,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!

Wizi akihofia, huja ukakuumbua,
Wewe ukajichekea, na kazi kwendelea,
Siku ya kushtukiwa, moto unaweza tiwa,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!

Haki akikuambia, vibaya kujiuzia,
Wewe ukamtania, na lako kuendelea,
Huja siku kweli kuwa, haya ukajionea,
Kweli mwalimu dunia, kazi yaek anajua!

Zinaaa akihofia, pabaya hukuchukua,
Wewe ukamnunia, na batili kuingia,
Yanapokujatokea, mbali nawe atakuwa,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!

Tamaa akikumbia, hukuingiza pabaya,
Wewe ukajichekea, na kuilea tabia,
Itakuja kuumbua, naye kajiondokea,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!
Uroho akikuambia, waweza kugeukia,
Wewe usiposikia, yanakujakutokea,
Kisha ukajililia, ujinga uliokuwa,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!

Uchu akikuambia, athari kuangamia,
Wewe ukapuuzia, na yako kuendelea,
Siku yakijajizoa, na wewe hutojijua,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!

Watu akikuambia, kuheshimiwa wafaa,
Na thamani kuijua, masihani kiingia,
Wewe ukalikataa, utakuja lijutia,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!

Wazazi wakifulia, itakufunza dunia,
Bila fimbo kuchukua, yakabidi kuingia,
Tena laivu yakawa, mwenyewe wajionea,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!'

Alimu namuachia, njia anayeijua,
Kizazi kuangalia, kisiwe kinapotea,
Njia usiyoijua, haifai kuingia,
Kweli mwalimu dunia, kazi yake anajua!

Mpenda vya ukoloni




Sheria za jalalani, zisibaki vitabuni,
Uhuru tulishawini, twafhifadhi ukoloni ?
Nani ataliami, atokaye Ulayani ?
Mpenda vya ukoloni, na yeye ni mkoloni!

Kama hapana uhuni, basi sisi majinuni,
Au tunayo moyoni, haki yasiyoamini,
Raia twawazaini, hali nasi wakoloni ?
Muenzi vya ukoloni, na yeye ni mkoloni!

Misingi hatuamini, usawa inayowini,
Tunaufanya utani, ustawi kuzaini,
Huu sio uhaini, ukiwemo katibani ?
Mpenda vya ukoloni, na yeye ni mkoloni!

Viongozi duniani, raia wanazaini,
Watwaa ya ukoloni, kuhodhi madarakani,
KIlichokuwa uhuni, sasa chapewa thamani,
Muenzi vya ukoloni, na yeye ni mkoloni!

Kuna mabomu yakini, ya machozi na hewani,
Hayachagui ni nani, atupiwa uwanjani,
Wazee na afkani, wote watiwa kundini,
Mpenda vya ukoloni, na yeye ni mkoloni!

Sheria za uhaini, zawaficha watu ndani,
Dhamana ikawa guni, japo iko katibani,
Ya mtu wayathamini, sio yalo sheriani,
Mpenda vya ukoloni, na yeye ni mkoloni!

Mikutano na maoni, yakatolewa uzani,
Wakaingia vitani, kodi inayoauni,
Mlipa akawa duni, kama damu na mumiani,
Muenzi vya ukoloni, na yeye ni mkoloni!

Kuna nyingi za kihuni, waziachia nchini,
Haki haziithamini, ila kulinda fulani,
Zisizotiwa ubani, wala usawa kuwini,
Mpenda vya ukoloni, na yeye ni mkoloni!

Uhuru wetu ni chini, viwango haujawini,
Katiba zungumzeni, uhuru kuuthamini,
Kisha kutathmini, chapungua kitu gani,
Muenzi vya ukoloni, na yeye ni mkoloni!

Uchochezi ndio nini



Uhaini ndio nini, pakiwepo ushindani,
Wanasheria watani, naomba lizungumzeni,
Latutia matatani, sisi tusiobaini,
Uchochezi ndio nini, dunia ya ushindani?

Niandike kitu gani,  uchochezi kutoghani,
Kama maji siyaoni, niseme yako njiani,
kama twaishi gizani, niige niko nuruni ?
Uchochezi ndio nini, dunia ya ushindani?

Kama shibe siioni, niseme niko makini,
Njaa iko hatarini, kuilaza kaburini,
Nitamdanganya mtu gani, kati ya walioko ndani ?
Uchochezi ndio nini, dunia ya ushindani?

Hata kichanga sidhani, baba kitaniamini,
Kitaniona ni mhuni, kama sio mamluni,
Akishanitathmini, akanitoa hisabuni,
Uchochezi ndio nini, dunia ya ushindani?

Nitakuwa hayawani, wengi wasiniamini,
Au kuwa utumwani, shaka watia moyoni,
Jamani niambieni, uchochezi kitu gani ?
Uchochezi ndio nini, dunia ya ushindani?

Haki zetu kubaini, nisiseme hadharani,
Katiba nisiamini, uhuru kunipa thani ?
Nizungumze kwa yakini, haki hata kwa maskini,
Uchochezi ndio nini, dunia ya ushindani?

Zama zenye ushindani, yote naona ilani,
Yategemea maoni, we, uko upande gani,
Hili ukitathmini, uhaini, uzaini,
Uchochezi ndio nini, dunia ya ushindani?

Mawakili elezeni, mna msimamo gani,
Na sisi tujiamini, pasina kuwa haini,
Itengezeni mizani, pande zote kuauni,
Uchochezi ndio nini, dunia ya ushindani?

SI UKUU HUU



KATIKA hii miaka, ya ujanja na hadaa,
Jambo ninalolijua, uchaguzi watakiwa,
Watu wakamchagua, kiongozi wa mkoa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Kwenye mwaka wa fadhaa, ukweli tutapojua,
Uongo tukifaragua, na ukweli kuenea,
Nchi umoja kulea, lazima huru mikoa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Nchi tuanjionea, vidogo vilivyokuwa,
Guinea Equatorial, milioni hawajawa,
Chumo wanajichumia, mkuu akachezea,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Dubai haijafikia, ya kwetu mingi mikoa,
Mauritius nayo pia, na Seychelles nakwambia,
Ila wanazitungua, hazinani kuingia,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Bahrain angalia, na Brunei nako pia,
Ka-Qatar ukijua, hautoyaridhia,
Ya kati kutawaliwa, watu wasikofikiwa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Ili uchumi kukua, njia ni huru mikoa,
Yao wakayaamua, kupanga na kupangua,
Rasilimali zikawa, zinaufaa mkoa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Wengine wakatambua, umuhimu watakiwa,
Za kwao kuzichumbua, pia nao kuwafaa,
Kubebana sio dawa, pua tutaangukia,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Mtu huru atakiwa, maamuzi kuyatoa,
Kisha akazingatia, utaifa kuufaa,
Mkoa kama nyumba huwa, kwanza kutolala njaa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Yote kuichukulia, kama sawa imekua,
Ni siasa zenye njaa, katu hazitatufaa,
Mikoa kujitambua, hatuwezi likataa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Mikoa kujitambua, fursa zilizokuwa,
Njia wakazichagua, za wao kuendelea,
Sawa haitatokea, tofauti itakuwa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Haya tukiyaelewa, nchi tutaiimua,
Hamira tukaitia, ikaanza jifutua,
Kuoka rahisi kuwa, na vitamu kuzaliwa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Umoja kuendelea, wala lhautajifia,
Ujerumani ni njia, hii waliyopitia,
Mtai anaijua, huko tulitembelea,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

UJimbo sio balaa, bali sasa ndio njia,
Kenya wameshaamua, kwa ukabila twajua,
Sisi tumeendelea, bado tunalihofia ?
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Ninaona ni hadaa, uchama kuendelea,
Wanachohofia, kuipoteza mikoa,
Upinzani kuitwaa, haraka ikajapaa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Naanika si kuanua, wenyewe mtalijua,
Uchama kwetu tanzia, kifo unatuletea,
Ustawi unavia, hali wanajisifia,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Njaa yazidi kolea, shibe wanasimulia,
Kisha wanatushangaa, njaa kuitangazia,
Kwao sasa ni sanaa, mchezo wa kugiziwa,
Si ukuu wa mkoa, nchi utakaojenga!

Kila kitu kina hadhi



Hakuna asiyejua, thamani kapungukiwa,
Mzawa adharauliwa, hadhi amefilisiwa,
Wakuu washindania, tena chini kumtia,
Kila kitu kina hadhi, ila mzawa nchini!

Uwizi anahofia, vya watu kuvikwapua,
Na wanaosingizia, ushahidi waishiwa,
Maneno yanabakia, huku wana waugua,
Kila kitu kina hadhi, ila mzawa nchini!

Uvivu asingiziwa, na ruksa kulilia,
Wakubwa wayasikia, wawekezaji kwmbia,
Yao wakayaridhia, la mzawa kukataa,
Kila kitu kina hadhi, ila mzawa nchini!

Elimu wanfulia, na ujuzi una njaa,
Hivyo wanatenguliwa, uboi ndio wafaa,
Na usafi kuutia, vyumba vikapendezea,
Kila kitu kina hadhi, ila mzawa nchini!

Umeneja wachagua, nje wanaotokea,
Haramu wakaingia, na bado waajiriwa,
Udhibiti wafulia, nini wanalolijua ?
Kila kitu kina hadhi, ila mzawa nchini!

Au wameshachukua, mapema walichong'oa,
Macho wakajifumbia, ujingani kujitia,
Mchezo kwako wachezewa, wachezaji kutojua?
Kila kitu kina hadhi, ila mzawa nchini!

Mwka huu natulia, yangu nimeelezea,
Kazi hayajafanyiwa, majibu nayangojea,
Kitu sikuambulia, bali macho kufungua,
Kila kitu kina hadhi, 'sipokuwa Mtanzania!

Huimbi lala mtoto



Mtoto sijasikia, lala mtoto kuimbiwa,
Hali sasa afungua, macho ili kuangalia,
Ataka changamkia, utoto kufurahia,
Huimbi lala mtoto, mwana akishaamka!

Kulala ukimwimbia, hilo haliwezi kuwa,
Lepe limemuishia, hawezi tena rudia,
Ila akijichokea, na njaa kutosikia,
Huimbi lala mtoto, mwana akishaamka!

Wakubwa mngelijua, wimbo huu udhia,
Mwana anapoimbiwa, aweza kukukwatua,
Au meno kukutia, pale usipotegemea,
Huimbi lala mtoto, mwana akishaamka!

Usingizi maridhia, kama alijipatia,
kwa miaka katulia, sasa ajiamkia,
Kukuru zake balaa, zaweza kuwaumbua,
Huimbi lala mtoto, mwana akishaamka!

Mkubwa akishakuwa, ni bora kumsikia,
Yake kuwaelezea, mkapata muelewa,
Elimu mngelitoa, hapa msingefikia,
Huimbi lala mtoto, mwana akishaamka!

Siasa kuzikimbia, kando mkajiwekea,
Kisha mkazungumzia, matumbo kujishibia,
Lugha hiyo waelewa, muafka hufikiwa,
Huimbi lala mtoto, mwana akishaamka!

Pamoja tungelikuwa, haya ningewaambia,
Mali yenu tunajua, kwa hapo ilipokaa,
Kwanza mnatakiwa, nyie mkajivunia,
Huimbi lala mtoto, mwana akishaamka!

Ila kwa wetu Utanzania,  sote budi kutufaa,
Mgao tutaangalia, mtakaokubalia,
Huo tutautumia, hadi neema kuenea,
Huimbi lala mtoto, mwana akishaamka!

Ujanja mkitumia, watu kuanza kugawa,
Mbali hamtafikia, kingoni mtatulia,
Mapya kuja zuliwa, hali mbaya kurejea,
Huimbi lala mtoto, mwana akishaamka!

Billa upya kuzaliwa



Mahala tumefikia, budi upya kuzaliwa,
Hilo lisipotokea, janga latunyemelea,
Viraka tukivitia, njiani vitatuumbua,
Bila upya kuzaliwa, naliota jinamizi!

Katiba tumeanzia, na mengine kuingia,
Mali asili kujua, vipi tunajigawia,
Haiwezi kuwa sawa, ilipo na isipokuwa,
Bila upya kuzaliwa, naliota jinamizi!

Tathmini zatakiwa, thamani kuzitambua,
Hesabu kukokotoa, mgawo tukaujua,
Haki ikiangaliwa, salama tutabakia,
Bila upya kuzaliwa, naliota jinamizi!

Uongozi watakiwa, kwanza watu kukomboa,
Kisha ukajinyanyua, hali bora ishakuwa,
Kwanza wanapojilia, tabaka zinashupaa,
Bila upya kuzaliwa, naliota jinamizi!

Usawa huanzia, kwa wanyonge kugawiwa,
Katikati wakikaa, nchi yaweza tulia,
Ila mbali kuachiwa, watakujatuumbua,
Bila upya kuzaliwa, naliota jinamizi!

Muhimu demokrasia, kote ikawakolea,
Ujanja tukiutia, twatafuta majeraha,
Tukitumia hadaa, zitakuja tenguliwa,
Bila upya kuzaliwa, naliota jinamizi!

Yangu ninayawazia, silazimishi yakwa,
Ila ninachokijua, watu wajiamkia,
Kulala wanakataa,  sasa macho wamekuwa,
Bila upya kuzaliwa, naliota jinamizi!

Hili asiyesikia, heri hajatutakia,
Ni kiziwi kuhofiwa, kweli kutoitambua,
Yeye akajiendea, shimoni kwenda tutia,
Bila upya kuzaliwa, naliota jinamizi!


KWANZA ULAJI, KISHA SIASA

Thamaniye huwa chini, miguu ikafutiwa,
Na popote duniani, nafasi haitapewa,
Mengine huwa utani, tumbo likichaguliwa,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Hata wenye kampuni, hili wanaliewa,
Fayageti huwa duni, watu wakajipitia,
Kwani upo ushindani,  njia wajitafutia,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Huondoka mashakani, mageti wakiyatia,
Ninajua yumkini, wapo rushwa wapokea,
Wataniachia ndani, kazi nikajifanzia,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Mla kala leo kwani, hili hawajalijua,
Na msomi wa mizani, huwa ametangulia,
Anayetamba nyikani, na mjini akujua,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Hutamba kwayo hisani, walaji wanayotoa,
Hali zetu bado guni, daawa haijatua,
Na ndarahima sineni, wingiwe sijaujua,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Ila sio yumkini, wote watazimwagiwa,
Hizo zina matawini, pamo namo mwa mitaa,
Kiasi chake mizani, imeishakutulia,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Hapa nilikuwa ndani, yangu nishajifanyia,
Ninawaaga watani, mwakani nitarejea,
Kwa leo pumzikeni, inshallah tukirejea,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Nilitoka bustani, maua kujipandia,
Kuingia kilingeni, mikwara nikaivaa,
Karibu sikubaini,  nje ninazuiliwa,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Nikakusanya watani, kazi wakaigombea,
Muda sikuubaini, saa gani ilikuwa,
Sikuona ubishani, dau nikajipangia,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Nikafungua vipini, na funguo kuzitoa,
Kisha nikawa makini, njia yangu kuchagua,
Pale kwenye upinzani, kupita nikakataa,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Pasipo na upinzani, nikazishusha silaha,
Sikupanda ukutani, mlangoni mepitia,
Nilipojitoma ndani, sera nikazipangua,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Kumbe hivi umaskini, kwa wngine ni silaha,
Hili wanalithamini, wataka kuendelea,
Ukifikia mwishoni, wapo wengi kufulia,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Na kisha abauitani, utajiri ndiyo njia,
Huna watalokuhini, fukara walia njaa,
Yako watayaamini, na njia kukuachia,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Yaoneni ya kusini, nako mashariki pia,
Uongozi wa imani, wafa kama ujamaa,
Sasa twabaki manyani, kuiga waliokuwa,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Watu hawana thamani, kitu wasipojaliw,a
Daima wakawa chini, watu wa kuitikia,
Ukubwa ni wa mizani, uzito ukachukua,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Vyama viko mashakani, yaoza demokrasia,
Imetiwa mitihani, migumu kujivukia,
Pasina ya mabilioni, ona vinavyougua,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Wafuasi wa imani, wote wameshazolewa,
Wanabaki mumiani, senti kuzifuatilia,
Walojaa mfukoni, miungu wameshakuwa,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Chama chao maskini, matajiri wachukua,
Wabakie mitaani, hadithi kusimulia,
Hawanao ushindani, wenye fedha watambia,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Nazo hizi kampuni, za simu zilizokuwa,
Se zetu tulio duni, wenye nacho wametwaa,
Yao kama ni shakani, rahisi kukuzuia,
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

Wafanza kama hisani, huku wanakupakua,
Wakakukata mapeni, muda wakakukatia,
Mnyonge ufanye nini, kwa waua demokrasia?
Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

NANI MWENYE KATIBA


KATIBA naiusia, mmiliki kutajiwa,
Tupate kumtambua, watu wote Tanzania,
Asije akatokea, tapeli kutuzingua,
Mmiliki wa katiba, lazima atambuliwe!

Ninavyojua raia, mmiliki atakuwa,
Pawa zote akapewa, kuamua, kutengua,
Kura akiitumia, au njia ya kufaa,
Mkubwa wa serikali, lazima tumtambue !

Afrika watibua, katiba kuzichezea,
Watumishi kuchukua, na haki wasichokuwa,
Ukuu kujipalia, mkaa usiokuwa,
Mkubwa wa kila kitu, lazima ajulikane!

Kisha kung'ang'ania, pale wasipotakiwa,
Ni vigumu kuachia, madhambi tukayajua,
Wanapenda kujifia, ikulu wanakokaa,
Mmiliki wa katiba, lazima atambuliwe!

Muundo unatakiwa, hili likaamuliwa,
Nami ninawausia, mabunge yanatufaa,
Juu yakishakua, na uchama kujifia,
Mkubwa wa serikali, lazima tumtambue !

Mawili yanatakiwa, taifa  kutumikia,
La kawaida likawa, la wanaochaguliwa,
La upili kuzaliwa, kwa fani na tasnia,
Mkubwa wa kila kitu, lazima ajulikane!

Hisabu ikatimia, kwa makundi kuingia,
Watu yakiwatetea, na wapweke kutokuwa,
Haya yatapokuwa, hukaa juu raia,
Mmiliki wa katiba, lazima atambuliwe!

Nadiriki kuongea, kuhusu pia  mikoa,
Mkuu anatakiwa, naye akachaguliwa,
Kisha akasaidiwa, na bunge la wake mkoa,
Mkubwa wa serikali, lazima tumtambue !

Thelathini yatakuwa, Mtwara ndani ikiwa,
Haki zao kutetea, kama gesi kuwafaa,
Katu wasingechezewa, kama wanayotezewa,
Mkubwa wa kila kitu, lazima ajulikane!

MMILIKI WA KATIBA NANI ?

 
 
KATIBA naiusia, mmiliki kutajiwa,
Tupate kumtambua, watu wote Tanzania,
Asije akatokea, tapeli kutuzingua,
Mmiliki wa katiba, lazima atambuliwe!
 
Ninavyojua raia, mmiliki atakuwa,
Pawa zote akapewa, kuamua, kutengua,
Kura akiitumia, au njia ya kufaa,
Mkubwa wa serikali, lazima tumtambue !
 
Afrika watibua, katiba kuzichezea,
Watumishi kuchukua, na haki wasichokuwa,
Ukuu kujipalia, mkaa usiokuwa,
Mkubwa wa kila kitu, lazima ajulikane!
 
Kisha kung'ang'ania, pale wasipotakiwa,
Ni vigumu kuachia, madhambi tukayajua,
Wanapenda kujifia, ikulu wanakokaa,
Mmiliki wa katiba, lazima atambuliwe!
 
Muundo unatakiwa, hili likaamuliwa,
Nami ninawausia, mabunge yanatufaa,
Juu yakishakua, na uchama kujifia,
Mkubwa wa serikali, lazima tumtambue !
 
Mawili yanatakiwa, taifa  kutumikia,
La kawaida likawa, la wanaochaguliwa,
La upili kuzaliwa, kwa fani na tasnia,
Mkubwa wa kila kitu, lazima ajulikane!
 
Hisabu ikatimia, kwa makundi kuingia,
Watu yakiwatetea, na wapweke kutokuwa,
Haya yatapokuwa, hukaa juu raia,
Mmiliki wa katiba, lazima atambuliwe!
 
Nadiriki kuongea, kuhusu pia  mikoa,
Mkuu anatakiwa, naye akachaguliwa,
Kisha akasaidiwa, na bunge la wake mkoa,
Mkubwa wa serikali, lazima tumtambue !
 
Thelathini yatakuwa, Mtwara ndani ikiwa,
Haki zao kutetea, kama gesi kuwafaa,
Katu wasingechezewa, kama wanayotezewa,
Mkubwa wa kila kitu, lazima ajulikane!

Siasa kwenye ulaji


 

Thamaniye huwa chini, miguu ikafutiwa,

Na popote duniani, nafasi haitapewa,

Mengine huwa utani, tumbo likichaguliwa,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Hata wenye kampuni, hili wanaliewa,

Fayageti huwa duni, watu wakajipitia,

Kwani upo ushindani,  njia wajitafutia,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Huondoka mashakani, mageti wakiyatia,

Ninajua yumkini, wapo rushwa wapokea,

Wataniachia ndani, kazi nikajifanzia,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Mla kala leo kwani, hili hawajalijua,

Na msomi wa mizani, huwa ametangulia,

Anayetamba nyikani, na mjini akujua,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Hutamba kwayo hisani, walaji wanayotoa,

Hali zetu bado guni, daawa haijatua,

Na ndarahima sineni, wingiwe sijaujua,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Ila sio yumkini, wote watazimwagiwa,

Hizo zina matawini, pamo namo mwa mitaa,

Kiasi chake mizani, imeishakutulia,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Hapa nilikuwa ndani, yangu nishajifanyia,

Ninawaaga watani, mwakani nitarejea,

Kwa leo pumzikeni, inshallah tukirejea,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Nilitoka bustani, maua kujipandia,

Kuingia kilingeni, mikwara nikaivaa,

Karibu sikubaini,  nje ninazuiliwa,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Nikakusanya watani, kazi wakaigombea,

Muda sikuubaini, saa gani ilikuwa,

Sikuona ubishani, dau nikajipangia,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Nikafungua vipini, na funguo kuzitoa,

Kisha nikawa makini, njia yangu kuchagua,

Pale kwenye upinzani, kupita nikakataa,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Pasipo na upinzani, nikazishusha silaha,

Sikupanda ukutani, mlangoni mepitia,

Nilipojitoma ndani, sera nikazipangua,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Kumbe hivi umaskini, kwa wngine ni silaha,

Hili wanalithamini, wataka kuendelea,

Ukifikia mwishoni, wapo wengi kufulia,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Na kisha abauitani, utajiri ndiyo njia,

Huna watalokuhini, fukara walia njaa,

Yako watayaamini, na njia kukuachia,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Yaoneni ya kusini, nako mashariki pia,

Uongozi wa imani, wafa kama ujamaa,

Sasa twabaki manyani, kuiga waliokuwa,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Watu hawana thamani, kitu wasipojaliw,a

Daima wakawa chini, watu wa kuitikia,

Ukubwa ni wa mizani, uzito ukachukua,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Vyama viko mashakani, yaoza demokrasia,

Imetiwa mitihani, migumu kujivukia,

Pasina ya mabilioni, ona vinavyougua,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Wafuasi wa imani, wote wameshazolewa,

Wanabaki mumiani, senti kuzifuatilia,

Walojaa mfukoni, miungu wameshakuwa,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Chama chao maskini, matajiri wachukua,

Wabakie mitaani, hadithi kusimulia,

Hawanao ushindani, wenye fedha watambia,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Nazo hizi kampuni, za simu zilizokuwa,

Se zetu tulio duni, wenye nacho wametwaa,

Yao kama ni shakani, rahisi kukuzuia,

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

 

Wafanza kama hisani, huku wanakupakua,

Wakakukata mapeni, muda wakakukatia,

Mnyonge ufanye nini, kwa waua demokrasia?

Siasa kwenye ulaji, miguu itafutiwa!

ASIYEJUA SHABAHA


Huhangaika mkiwa, na hii kubwa dunia,

Shabaha aliyepwaya, hawezi akapatia,

Kila akifikiria, pengine atatungua,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Wengi nimeshuhudia, ujanja walijitia,

Kwa kiburi kujitia, kulenga wamesomea,

Ila kilichofatia, washinda kushuhudia,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Karibu waliyaachia, mbali wakayazuikia,

Kuja kutahamakia, mkenge wameingia,

Na walilolidhania, kama kweli halikuwa,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Kwa pembeni wafulia, ukutani  kuingia,

Kulalama wabakia, pengine wamechezewa,

Au wamehujumiwa, wala haki haikuwa,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Kilio watakizua, machozi wakayatoa,

Macho yaliathiriwa, uchafu ukaingia,

Au homa kuingia, ghafla mwili kulewa,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Yote ukiangalia, mwee, wanasingizia,

Ziliwazidi tamaa, huku na huku kwingia,

Saa ilipofikia, wkadhindwa kuamua,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Ndiyo yanayotokea, kwa wengi wa Tanzania,

Kwa walilojitakia, kuwa limewakataa,

Na walilolichukia, ndio sasa lawafaa,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Wapo walioolewa, hali ni bahati mbaya,

Mme mpenzi hajawa, na mkewe aidha pia,

Wanauzusha ubia, subira na kuvumilia,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Hawezi kushangaa, DNA yachukiwa,

Kwa kuizua balaa, na kweli ikazagaa,

Walio na maridhia, mkono hawajajaa,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Bwanangu mwenye kujua, neno ninakuachia,

Siri yangu waijua, na vyangu vilivyokuwa,

Asante kwa kuridhia, haki yangu kuipewa,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

 

Wivu sitajionea, wenye vyao visokuwa,

Kidogo nilichopewa, kinaweza kunivua,

Subira nitailewa, pasina kulewa dunia,

Asiyejua shabaha, halengi  mpaka kufa!

MCHAGUA SANA


 

Kuna muda na wasaa, na kitambo kupitia,

Majira usipojua, dakika zitapotea,

Ukija kuhesabiwa, masaa yemetimia,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Dahari hatukupewa, ni sekunde twaachiwa,

KIla zinapochepua, ngozi zetu zikavia,

Na pumzi huchelewa, mengi tukajichokea,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Bahati ikiwajia, bado wataichambua,

Kisha hujiinukia, mbele ikaendelea,

Halafu huangukia, pua zao kuumia,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Wa msimu huingia, upepo wa kulowea,

UKiisha wapepea, heri wakategemea,

Ukiwawageukia, kama ukichaa huwa,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Wastani huachia, zaidi kukimbilia,

Huko akishaingia, nakisi huigundua,

Nyuma akigeukia, tayari kimetwaliwa,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Uzuri atachagua, akakuta walemaa,

Rijali akivizia, akakuta una waa,

Na mme mke huwa, katika hii dunia,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Akili akifatia, huingia ukichaa,

Bora alichochagua, kikawa kinamchachia,

Werevu akaezua,  mvi akajipambia,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Mali hukimbilia, uzani ukatitia,

Mbio hapo husanzua, kwingine kuelekea,

Hali akatarajia, atakuta iko sawa,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Huko akafumania, nayo yamejichachia,

Katikati hubakia, kama amenatishiwa,

Akiweza kujitoa, nusura huwa kulia,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Kikaango hukimbia, motoni akaingia,

Huruma hatoijua, hadi majivu akawa,

Huo mwisho wake kuwa, akaiga dunia,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Ndivyo ilivyo dunia, ya mchezo na sanaa,

Saburi inaijua, kisha mkubwa wasaa,

Haraka haijaijua, ila inapojifungua,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Hchounachojionea, lenga hapo na kutua,

Kibakaika radhia, hatua utapotea,

Mwanangu binti kukaya, huu ni wangu wasia,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

Sijisumbue na kung'aa, huja kuwa ni balaa,

Mtake wako Jalia, ombilo kukuridhia,

Ibada mkiijua, yeye atawaangalia,

Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !

 

AMANI KAMA TUNDA



WAOVU ukiachia, mabichi wanaaangua,

Wende kuvundukia, wewe usipopajua,

Juu kwa juu ikawa, bei wanapatania,

Amani yetu ni tunda, nani anatunza shamba  ?

 

Miti msipoangalia, magugu hujiotea,

Ikawa shida kuzaa, mti unapohujumiwa,

Matatizo huzushiwa, hadi shamba kukimbia,

Amani yetu ni tunda, hivi mti twautunza ?

 

Na maji pasipokuwa, mti waweza sinyaa,

Mchwa wakafurahia, chakula chao kikawa,

Wakua ukidhania, kumbe wenda kujifia,

Amani yetu ni tunda, mti twastawishaje  ?

 

La bibi linapokuwa, watu wakajichumia,

Hasara mtaingia, mwizi pasi kumjua,

Haki wamejigawia, nini utaambulia ?

Amani yetu ni tunda, shamba amiliki nani ?

 

Miti inapochakaa, mipya huwa yatakiwa,

Mbegu usipojaliwa, hutoweza jipandia,

Vya kale vikiendelea, huja kuvuna udhia,

Amani yetu ni tunda, mbegu twazipata wapi ?

 

Mti wataka mbolea, pia maji kumwagia,

Hasa katika dunia, mvua ilikopotea,

Bila hivyo kikawia, waweza jinyaukia,

Amani yetu ni tunda, mti twastawishaje  ?

 

Jasho mwaweza kutoa, pasiwe cha kuambulia,

Sababu mia kutoa, kwanini mmefulia,

Ikawa kusingizia, tatizo kisichozua,

Amani yetu ni tunda, shamba amiliki nani ?

 

Sayansi inatakiwa, pia kwenda kutumia,

Sasa ni kunyunyizia, tone kwa kila hatua,

Kwayo mti ukakua, na maua kuchanua,

Amani yetu ni tunda, mbegu twazipata wapi ?

 

Maji katika dunia, sasa yanakopotea,

Mikakati yatakiwa, kidogo kutoshelea,

Watu wakaajabia, kuwa wasilodhania,

Amani yetu ni tunda, mti twastawishaje  ?

 

Yajapo yakatokea, umiliki kuvamiwa,

Na wanaoyasimamia, wao pembeni kukaa,

Wakateza na sheria, kukunja na kukunjua,

Amani yetu ni tunda, shamba amiliki nani ?

 

Hasira huziibua, kwa wanaofatilia,

Kuwatuliza huvia, mishipa wakatanua,

Mhemuko ukikua, huja kuzuka balaa,

Amani yetu ni tunda, mbegu twazipata wapi ?

 

Mti ukijaugawa, pande moja kumwagia,

Ajabu haitakuwa, nusu kufa, nusu zaa,

Bali wote utavia, na mwisho kuteketea,

Amani yetu ni tunda, mti twastawishaje  ?

 

Chanzo msipokijua, dalili mkaagua,

Huja kushtuliwa, maradhi yakizidia,

Hujivunga wakujua, kupata pa kupenyea,

Amani yetu ni tunda, shamba amiliki nani ?

 

Mbegu wakizifukua, wakaanza kujilia,

Pasiwe kurudishia, uhai kuendelea,

Watajazuka vichaa,  mapanga yakatembea,

Amani yetu ni tunda, mbegu twazipata wapi ?

 

Wanaoiba mbolea, na vipando kuvitwaa,

Vyao wakajifanyia, kwanza wanakimbilia,

Wengine wakafulia, huja wakaambuliwa,

Amani yetu ni tunda, mti twastawishaje  ?

 

Juu waliokalia, budi macho kufungua,

Kwa sawa kuangalia, hali hasa wakajua,

Vingine ni kutania, na kuchezea dunia,

Amani yetu ni tunda, shamba amiliki nani ?

 

Nani anatuhadaa, mti tunaufatia,

Kisha tukajipandia,  huko tusikoruhusiwa,

Tunga linaning'inia, twataka kujichumia ?

Amani yetu ni tunda, shamba amiliki nani ?

 

Kila nikiangalia, haki na usawa bandia,

Mwivi namgundua, ndiye ananyemelea,

Macho tunawafumbia, vingine kusingizia,

Amani yetu ni tunda, shamba amiliki nani ?

Pazia lafunguliwa



Lakunjuliwa pazia, tuone yanayotokea,

Mwaka unakaribia, Januari kuingia,

Nangojea potezea,  jinsi zitakavyokuwa,

Pazia lafunguliwa, la sanaa na viroja !

 

Nazingojea sanaa, zitakavyonistua,

Akili zilizolemaa, wenda zikashtuliwa,

Hali yangu kurejea, uhakika nikajua,

Pazia lafunguliwa, la aibu na fedheha !

 

Pazia la madini gawa, na hisabu kupotea,

Akili kuzilalia, mfukoni kuzitia,

Na hongo kuinunua, uwezayo kununua,

Pazia lafunguliwa, la sanaa na viroja !

 

Pazia mafuta haya, na nani ayanunua,

Na mchezo kuchezewa, uwanja usiokuwa,

Bei ikapotezewa, na uchumi kuchafua,

Pazia lafunguliwa, la aibu na fedheha !

 

Pazia umeme njaa, njiani unaoishia,

Hamsini kutimia, robo haijafikia,

Visababu kwa gunia, haviachwi kutolewa,

Pazia lafunguliwa, la sanaa na viroja !

 

Pazia la maji mwaa, watu wasiyojionea,

Na ahadi zajifia, bila ugonjwa kujua,

Kilio kutosikia, ila mazishi yakawa,

Pazia lafunguliwa, la aibu na fedheha !

 

Pazia la ng'ombe waya, na vijosho vya kwogea,

Nasaba ikanukia, na ujanja wa kijuha,

Heri inakopepewa, hadi moto kuuzua,

Pazia lafunguliwa, la aibu na fedheha !

 

Pazia la Swizi gea, na vigia vya kutia,

Waliojikusanyia, na vilango kupitia,

Uchama ukawatoa, kama wanavyoutoa,

Pazia lafunguliwa, la sanaa na viroja !

 

Pazia la kufunikia, daktari kutegewa,

Kisa haki kulilia, ubaya akazuliwa,

Mwee, ninajichukia, kama nisiyezaliwa,

Pazia lafunguliwa, la aibu na fedheha !

 

Pazia la kufukia, wala si kufundishia,

Walimu walilolivaa, na kushindwa kuwafaa,

Vitumbua kugawiwa, vya kuokewa sheria,

Pazia lafunguliwa, la sanaa na viroja !

 

Batili yaendelea, na haramu yanadiwa,

Haki wameifungua, dhuluma waifungua,

Tarakimu kutimia, maajabu nangojea,

Pazia lafunguliwa, la aibu na fedheha !

Imani sio kelele

 
Imani wasiokuwa, kwa kelele huwajua,
Itarindima  mitaa, eti wanafurahia,
Na kundini kujitia, Mola wanamhofia,
Imani sio kelele, wengine kuwapigia !
 
Kumbe kwao ni mzaha, usanii wajitia,
Yao wamejilengea, kutimu wakusudia,
Nao wasiotambua, mkengeni huingia,
Imani sio kelele, wengine kuwapigia !
 
Miziki huifungua, masikio kuvamiwa,
Ugaidi kufanyia, ushindwe jipumzikia,
Ni furaha ya hadaa, masaa haitachukua,
Imani sio kelele, wengine kuwapigia !
 
Udamisi hujitia, marafiki  kununua,
Pilau kuwapikia, kula pamoja kwa furaha,
Nje wakichekelea, ndani uovu wajaa,
Imani sio kelele, wengine kuwapigia !
 
Si heri hapo hutua, ila bad na majaa,
Watu wakijiondoa, wengine wakaugua,
Na mikosi kufatia, kila wanakopitia,
Imani sio kelele, wengine kuwapigia !
 
Mwaka hawataujua, ndondocha  watazaliwa,
Yao hapo kuishia, wao wakaendelea,
Nyumba usiyoijua, ogopa kwenda kukaa,
Imani sio kelele, wengine kuwapigia !
 
Kuna nyumba za nazaa, uovu zinazolea,
Mchana utadhania, walokole wamekua,
Usiku ukiingia, mashetani wanakuwa,
Imani sio kelele, wengine kuwapigia !
 
Roho wanazojaliwa, nyeusi zanyaukia,
Hata weupe wakiwa, dalili huzihofia,
Wewe hawatakwambia, kwingine huzungukia,
Imani sio kelele, wengine kuwapigia !
 
Furqani maridhia, kinga ninakutumia,
Enenda kuwaumbua, popote wanapokaa,
Na usiku wakitua, kaziyo kuwanyanyua,
Imani sio kelele, wengine kuwapigia !
 

Toka lini mshirikina



Mshirikina amini, amekuwa ni kuhani,
Kaingia hekaluni, joho li  kisiginoni,
Ameremeta yakini, kama taa ya imani,
Toka lini mshirikina, akawa ni mcha mungu ?

Molawe yuko nyumbani, kabakia kabatini,
Kamchonga kwa makini, ndiye humpa imani,
Akienda hekaluni, huwa ni uchi mwilini,
Toka lini mshirikina, akawa ni mcha mungu ?

Ibada yake shetani, kamjengea moyoni,
Majini wamdhamini, na maruhani kuwini,
Na mikoye ni ghalani, kaihifadhi darini,
Toka lini mshirikina, akawa ni mcha mungu ?

Akiranda mtaani, mitumewe mfukoni,
Hao anawaamini, humlinda majiani,
Kwa talasimu kifani, shingoni na kiunoni,
Toka lini mshirikina, akawa ni mcha mungu ?

Atadamka manani, kumsikiza shetani,
Kisha akatathmini, muda wa kuwa kundini,
Mkaona ibadani, naye yumo miongoni,
Toka lini mshirikina, akawa ni mcha mungu ?

Asubuhi na jioni, kutabana ni hisani,
Kaitwa majaribuni, na vibwete vya majini,
Hakosi mkutanoni, kuyapata madhumuni,
Toka lini mshirikina, akawa ni mcha mungu ?

Mizimu ataamini, kuliko wana nyumbani,
Shari wakishaazini, asipotii haini,
Kuua yake husuni, na ngome ushirikinani,
Toka lini mshirikina, akawa ni mcha mungu ?

Kapewa akili dunia, ahera na duniani,
Jema hatolibaini, ila akirizaini,
Akaijenga imani, ahame toka uthani,
Toka lini mshirikina, akawa ni mcha mungu ?

Raia ni kama wana



ZAMA hizo tukijua, ungozi ni kulea;
Dhamana wakiitwaa; wao wazazi wakawa,
Leo tunawashangaa, wapitaji wamekuwa,
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukichukia:
Mwana humtakia mabaya;
Kisha akamsingizia;
Na kumtia  hatia ?

Wana wachanganyikiwa, njaa kuwashambulia,
Baba anakazania, shibe inawasumbua ?
Barazani amekaa, kiko anajivutia,
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukionea:
Akawalaza na njaa;
Na maji kuwamwagia;
Usiku wajilalia ?

Makombo awapatia, huko alikoyatoa,
Mashaka yanawatia, usalama kutokuwa,
Kuleni mkikataa, mtalala na njaa:
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Chakula huwaokotea,
Jalalani kwenye baa;
Sio kuwa kaishiwa;
Ila thamani kawatoa ?

Nje wakijitokea, ipate jua dunia,
Kuandamana balaa, mawe anawatupia,
Kisha kuwasingizia, ni wevi waliokuwa;
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukichukia:
Ulemavu kuwatia;
Kwa mabomu kurushia;
Na sumu kuwamwagia ?

Nje wakienda lia, ipate jua dunia,
Mkusanyiko huzua, maji moto kumwagiwa;
Kisha kuwasimbulia, sheria wanachezea;
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukichukia:
Ulemavu kuwatia;
Kwa mabomu kurushia;
Na sumu kuwamwagia ?

Mikataba aingia, urithi kujiuzia,
Wana wakiulizia, waambiwa kujijua;
Lao kujitafutia, malaika walokuwa ?
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Urithi ajinadia;
Bila wana kuwambia;
Mashimo yakabakia;
Kaburi kujichimbia!

Watu baki kaachia, mashamba wajivunia,
Senti anazoletewa, kila siku zinapwaya;
Mifuko imemjaa, hataki kujisumbua:
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Tathminiye hadaa;
Penye ukwasi pakiwa;
Mgeni hujichumia;
Wanawe  wakafulia ?

Akiambiwa hukataa, uongo akaridhia,
Hujifanzia sanaa, kwa akili kumjaa;
Kisha huwadithia, kile kisichowafaa,
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukichukia:
Ulezi akaondoa;
Hatari kuwatakia;
Wawapo katika njia  ?

Kwake kaifunga taa, gizani wana wakaa,
Vifaa ndani vyajaa, nishati ndio udhia,
Kila wakiililia, ni mchezo wachezewa,
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Gizani huwaachia:
Wakajihangaikia:
Yeye nuruni kakaa:
Vyake anavitumbua ?

Bomba kwake yaishia, maji kunywa ni ukiwa,
Wote wanahitajiwa, magoti kumpigia,
Jeuri ukijitia, kwa kiu utajifia;
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Maji kawadanganyia;
Na kiu kinawaua;
Wa nje awajazia;
Hadi wanayachezea ?

Asili yahukumiwa, sasa kusahauliwa,
Vijiji vinaumia, kwa kiu pia na njaa,
Nani wa kuangalia, wa mjini  wazidiwa ?
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kijiji hukikimbia;
Mjini akaingia;
Kwake kupachukia;
Ustawi ukavia ?

Raia ni kama wana



ZAMA hizo tukijua, ungozi ni kulea;
Dhamana wakiitwaa; wao wazazi wakawa,
Leo tunawashangaa, wapitaji wamekuwa,
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukichukia:
Mwana humtakia mabaya;
Kisha akamsingizia;
Na kumtia  hatia ?

Wana wachanganyikiwa, njaa kuwashambulia,
Baba anakazania, shibe inawasumbua ?
Barazani amekaa, kiko anajivutia,
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukionea:
Akawalaza na njaa;
Na maji kuwamwagia;
Usiku wajilalia ?

Makombo awapatia, huko alikoyatoa,
Mashaka yanawatia, usalama kutokuwa,
Kuleni mkikataa, mtalala na njaa:
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Chakula huwaokotea,
Jalalani kwenye baa;
Sio kuwa kaishiwa;
Ila thamani kawatoa ?

Nje wakijitokea, ipate jua dunia,
Kuandamana balaa, mawe anawatupia,
Kisha kuwasingizia, ni wevi waliokuwa;
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukichukia:
Ulemavu kuwatia;
Kwa mabomu kurushia;
Na sumu kuwamwagia ?

Nje wakienda lia, ipate jua dunia,
Mkusanyiko huzua, maji moto kumwagiwa;
Kisha kuwasimbulia, sheria wanachezea;
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukichukia:
Ulemavu kuwatia;
Kwa mabomu kurushia;
Na sumu kuwamwagia ?

Mikataba aingia, urithi kujiuzia,
Wana wakiulizia, waambiwa kujijua;
Lao kujitafutia, malaika walokuwa ?
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Urithi ajinadia;
Bila wana kuwambia;
Mashimo yakabakia;
Kaburi kujichimbia!

Watu baki kaachia, mashamba wajivunia,
Senti anazoletewa, kila siku zinapwaya;
Mifuko imemjaa, hataki kujisumbua:
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Tathminiye hadaa;
Penye ukwasi pakiwa;
Mgeni hujichumia;
Wanawe  wakafulia ?

Akiambiwa hukataa, uongo akaridhia,
Hujifanzia sanaa, kwa akili kumjaa;
Kisha huwadithia, kile kisichowafaa,
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kizazi hukichukia:
Ulezi akaondoa;
Hatari kuwatakia;
Wawapo katika njia  ?

Kwake kaifunga taa, gizani wana wakaa,
Vifaa ndani vyajaa, nishati ndio udhia,
Kila wakiililia, ni mchezo wachezewa,
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Gizani huwaachia:
Wakajihangaikia:
Yeye nuruni kakaa:
Vyake anavitumbua ?

Bomba kwake yaishia, maji kunywa ni ukiwa,
Wote wanahitajiwa, magoti kumpigia,
Jeuri ukijitia, kwa kiu utajifia;
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Maji kawadanganyia;
Na kiu kinawaua;
Wa nje awajazia;
Hadi wanayachezea ?

Asili yahukumiwa, sasa kusahauliwa,
Vijiji vinaumia, kwa kiu pia na njaa,
Nani wa kuangalia, wa mjini  wazidiwa ?
Raia ni kama wana, hivi ni mzazi gani:
Kijiji hukikimbia;
Mjini akaingia;
Kwake kupachukia;
Ustawi ukavia ?

Atakiwaye king'ora

Matumizi sijajua, king'ora kukitumia,
Laiti mkinambia, usahihi nitajua,
Wapi pa kukitumia, kugota nikaachia,
Atakiwaye king'ora, mgonjwa au mzima ?

Ni hoi aliyekuwa, kwa dhiki pia na njaa,
Au aliyejaliwa, tumbo limejifutua,
Shibe imemlevyea, hadi chakari akawa ?
Atakiwaye king'ora, hoi au alojaliwa

Kichanga aliyekuwa, njiani ameumia,
Au mkubwa kajaa, twatakiwa kumjua ?
Kwanza akajipitia, wengine tukafatia ?
Atakiwaye king'ora, mkubwa au mtogo ?

Nani wa mbele akawa, uchumi kuuinua,
Juu waliokalia, au chini walokuwa,
Wao wakinyanyuliwa, ngazi kwao kujakuwa ?
Atakiwaye king'ora, rais au raia?

Kibibi kashambuliwa, uchawi kutuhumiwa,
Au mzazi tarajiwa, zahanati kuwahia,
Aende kujifungua, kitumbe tusichojua?
Atakiwaye king'ora, mzazi au ajuza ?

Maiti zachukuliwa, mijifedha zashonewa,
Ipi tutakayojua, ni ujanja wa kuzuwa,
Njia tukawaachia, salama kujipitia ?
Atakiwaye king'ora, aliye hai au mfu ?

Akili zikizidia, hakika ujinga huwa,
Yapo ya kujirithia, twafaa kuyakataa,
Nendeni Scandinavia, haya mtajionea,
Atakiwaye king'ora, ni fedha au kiumbe ?

Hatuwezi kulingana



Sifa sijaitafuta, na wala sintoitaka,
Sijipakai mafuta, ngozi yangu yatakata,
Hapa kinachonileta, haki isiwe wahaka,
Hatuwezi kufanana, nyie mnataka sifa:
Mie ninataka dawa !

Majibu ninatafuta, majawabu sijashika,
Kukariri sijadata, ila fikra nazitaka,
Na uongo kuuteta, kwangu huwa ni dhihaka,
Hatuwezi kufanana, nyie mnataka sifa:
Mie ninataka dawa !

Mna ndoto za kuota, nalitaka la hakika,
Mwajijengea ukuta, ila wangu wabomoka,
Kila muweka matuta, usalama autaka,
Hatuwezi kufanana, nyie mnataka sifa:
Mie ninataka dawa !

Ya kwenu ni kupepeta, mimi ni kuhangaika,
Kazi yangu si kusuta, ila bayana kuweka,
Kama nyie chuma-leta, mimi yangu kulimika,
Hatuwezi kufanana, nyie mnataka sifa:
Mie ninataka dawa !

Ya kwenu ni ya kung'ata, vigumu kutafunika,
Meno yenu ya kukata, hali yetu yapangika,
Mkiyachota kwa kata, yetu yaja kwa birika,
Hatuwezi kufanana, nyie mnataka sifa:
Mie ninataka dawa !

Nyie mnapojiokota, sisi kwanza tunashuka,
Mikono mkipepeta, siye twaanza kuvuka,
Twaogelea ukata, nyie mmetajirika,
Hatuwezi kufanana, nyie mnataka sifa:
Mie ninataka dawa !

Mkata kaziye kusota, shoga hakubahatika,
Zama pakiwepo kota, leo ghorofa zazuka,
Kumbe maisha huchota, wengine wakamwagika?
Hatuwezi kufanana, nyie mnataka sifa:
Mie ninataka dawa !

Uziwi wanajitia



ZAMA zimetufikia, ngoma zetu kutoboa,
Ukadhani wajijua, na kuwakoga jamaa,
Anga ukazipasua, riha ipate enea,
Uziwi wanajitia, kwa wengine kusumbua!

Kumbe unajishaua, ubaya kukurudia,
Masikio kutoboa, uziwi ukaingia,
Siku inapofikia, muziki hutoujua,
Uziwi wanajitia, kwa wengine kusumbua!

Kelele lhutoijua, tofauti ilokuwa,
Muziki kilingania, sawa ukajionea,
Midadi uloringia, ikawa yakuumbua,
Uziwi wanajitia, kwa wengine kusumbua!

Hali sawa kujitia, njiani ukitembea,
Ila kwa wanaokujua, vidole kukunyoshea,
Watu wakahadithia, kisa kilichotokea,
Uziwi wanajitia, kwa wengine kusumbua!

Ulikuwa wa kujua, ngoma unajijazia,
Za uzito kadiria, disco unaoingia,
Ndani ukajichimbia, ili watu kustua,
Uziwi wanajitia, kwa wengine kusumbua!

Lakini haukujua, mzizi unachimbua,
Vifaa kuvipasua, visije kesho kufaa,
Wakati ukafikia, si tena wa kusikia,
Uziwi wanajitia, kwa wengine kusumbua!

Dhihaka uliyogawa, iwe inakurudia,
Furaha uliyojua, ikaja kuwa ni ukiwa,
Dhiki kutojitambua, ukiishi na jamaa,
Uziwi wanajitia, kwa wengine kusumbua!

Wakwasi waliopewa, wazazi wajivunia,
Wana wakawaachia, wakaitesa jamaa,
Nayo kama hayo pia, ndiyo yanayowafikia,
Uziwi wanajitia, kwa wengine kusumbua!

Ukijifanya bendera



IKIWA umeamua, ya bendera kuyazua,
Upepo hukuchukua, kushoto hata kulia,
Juu ukakunyanyua, hadi chini kukutia,
Ukijifanya bendera, mwenyewe utajipepea !

Waweza kujisikia, umeikwea dunia,
Hadhi utakayopewa, isiache kukuzua,
Hadi jioni 'kindia,uwe chini washushiwa,
Ukijifanya bendera, mwenyewe utajipepea !

Hali inapotulia, kweli utaheshimiwa,
Na saluti kupigiwa, na watu usiowajua,
Ila wakikuzoea, kitambaa utakuwa,
Ukijifanya bendera, mwenyewe utajipepea !

Nyumayo pasipokuwa, na dola ya kuheshimiwa,
Ila unajitokea, miguu kujiburuzia,
Watu maji hukutia, ukaitwa changudoa,
Ukijifanya bendera, mwenyewe utajipepea !

Hadhari usipotia, mnarani hunyofolewa,
Ukachanwachanwa pia, jalalani kutupiwa,
Sio kitu ulikuwa, ndipo unapojitambua,
Ukijifanya bendera, mwenyewe utajipepea !

Waweza moto kutiwa, pasiwe wa kukuokoa,
Motoni kuteketea, rangi hadi kupotea,
Wasifa uliokuwa, mara sio kitu kuwa,
Ukijifanya bendera, mwenyewe utajipepea !

Waweza kufafiliwa, ufagio mara kuwa,
Vumbi ukalitimua, na buibui kutoa,
Kazi mpya kujaliwa, kazini kujifunzia,
Ukijifanya bendera, mwenyewe utajipepea !

Waweza kunyakuliwa, na mwendambio kichaa,
Shuka akakutumia, usiku kujifunikia,
Maji hautayajua, hadi kuaga dunia,
Ukijifanya bendera, mwenyewe utajipepea !

Wachawi waende wapi ?


Wana vingi wahofia, nje hawatatokea,
Wana uzi wa ubaya, wenzao wawafumia,
Wana deni wadaiwa, kuwiwa wanahofia,
Wachawi waende wapi, sikukuu hula kwao!

Mila zao za kuvia, hawawezi kuchanua,
Popote wnapokaa, hali huwa zasinyaa,
Sikukuu huchukia, nguvu zao zafifia,
Wachawi waende wapi, sikukuu hula kwao!

Kutabana waishia, bure hawajaijua,
Wakati wautumia, ovyo kwenda jisemea,
Kazi yao kutokuwa, sauti wasipotoa,
Wachawi waende wapi, sikukuu hula kwao!

Si wa kufikiria, jipya wakalizua,
Lao wanalotumia, ukale  limeanzia,
Halina teknolojia, vipi litaendela ?
Wachawi waende wapi, sikukuu hula kwao!

Yao ni ya kusumbua, wala si kusaidia,
Vipi kusherehekea, na misaba wanazaa,
Wanaupenda ukiwa, yalazimu kuulea,
Wachawi waende wapi, sikukuu hula kwao!

Jirani wanapokuwa, yao wanaazimia,
Kuudhi na kusumbua, na furaha kuondoa,
Ukabakia ukiwa, wao wende furahia,
Wachawi waende wapi, sikukuu hula kwao!

Asali hii si tamu



ASALI hii bandia, tayari nimeijua,
Utamu haijaliwa, ila mate yautia,
Kwa hili kuling'amua, debe ninalikataa,
Asali hii si tamu, mate yanakuchezea!

Gairo naelekea, yangu kwenda kununua,
Singida nikapitia, viwango kujipimia,
Halisi nikiijua, ndio pochi kuachia,
Asali hii si tamu, mate yanakuchezea!

Asili inapokuwa, dawa kweli inakuwa,
Maradhi kujitibia, elfu yaliyokuwa,
Si uongo nawambia, kwa kila mwenye kujua,
Asali hii si tamu, mate yanakuchezea!

Yatakiwa ya maua, nyuki  kutochakachua,
Mizingani kulelewa, na kisha ikapepewa,
Kwa ufundi kutolewa, panna kitu kutiwa,
Asali hii si tamu, mate yanakuchezea!

Sukari inayotiwa, hauachi kuijua,
Guru ikiongezewa, rangiye utaijua,
Ya kweli isiyokuwa, wala dawa haitakuwa,
Asali hii si tamu, mate yanakuchezea!

Shamaba  nimelinuia, kwenda kujianzishia,
Mizinga nikaitia, na nyuki kuangalia,
Umri ukishaingia, ya kweli kujipatia,
Asali hii si tamu, mate yanakuchezea!