Uongo unauzua, eti unanigaia,
Hicho unachochukua, na mimi najipatia,
Unaidanganya haya, mwananme usiokua,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!
Mola ninamuachia, dhahiri kukusikia,
Kisha akajipimia, ukweli uliokua,
Kitu sijashuhudia, ila maneno naambiwa,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!
Waema wanisaidia, maana nishalemaa,
Tumboni umevimbiwa, vyote umeshavitia,
Aibu ungelijaliwa, haya usingetwambia,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!
Haywani weza kuwa, ni bora waheshimiwa,
Kuliko uliyekua, uongoa uliyejaa,
Na mimi nakuumbua, chako sijakipokea,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!
Moto wajipalilia, hujui lakuongea,
Mdomo ukifungua, uongo unaachia,
Mkweli hukuzaliwa, siwezi kutazamia,
© 2011 Sammy Makilla
Wednesday, December 28, 2011
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment