Wednesday, December 28, 2011

Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Ukubwa twakuombea, na nafsi ije jaa,
Imani hukujaliwa, chukua yako dunia,
Tutakuja kuamua, ukija tuamkia,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

Unaipenda dunia, haikupendi dunia,
Wewe waing'ang'ania, yenyewe itakuzoa,
Umejenga mazoea, mengine hutoelewa,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!

© 2011 Sammy Makilla

No comments: