Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!
Ukubwa twakuombea, na nafsi ije jaa,
Imani hukujaliwa, chukua yako dunia,
Tutakuja kuamua, ukija tuamkia,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!
Unaipenda dunia, haikupendi dunia,
Wewe waing'ang'ania, yenyewe itakuzoa,
Umejenga mazoea, mengine hutoelewa,
Wasema wanigaia, kama wongo ulaniwe!
© 2011 Sammy Makilla
Wednesday, December 28, 2011
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment