Tuesday, January 17, 2012

Pepo kuwa Jehanamu

Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Na huwezi kukosea,
Ni fisadi walokuwa,
Na waliowasaidia,
Mengineyo ni hadaa!


Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Mamlaka kuibiwa,
Raia walopewa,
Na katiba ilokuwa,
Na wengine kuzomewa!

Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Ni wanaojimegea,
Nchi wanayotakiwa,
Vizuri kuiangalia,
Kama shamba la bibi kuwa!

Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Wanaojilimbikia,
Kushoto pia kulia,
Wanyonge wanaoonea,
Na vya kwao kuchukua!

Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Ni rushwa wanaopokea,
Na matumbo kuwajaa,
Na dola kuwaangalia,
Kama si kuwatetea!

Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Wajenzi wasofatia,
Ubora unaotakiwa,
Hadi wanakabidhiwa,
Kibovu kilichokua!


Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Posho wanaopokea,
Bila ya kujionea,
Bora walichofanyia,
Umma wa Tanzania!


Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Mgeni anayepewa,
Cha wenyeji walokuwa,
Mkubwa akachukua,
Na wenyeji kuibiwa!


Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Polisi anayeua,
Aso hatia raia,
Na vyake kuvichukua,
Na kazi kuendelea!

Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Mwizi anayetumia,
Mbwa wake kumwibia,
Asokuwa na hatia,
Aibiwaye akafungwa!

Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Ni hakimu kupokea,
Amri toka kulikokuwa,
Uamuzi kuutoa,
Haki usiozingatia.


Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Tofauti kuzidia,
Baina yake mikoa,
Wengine juu wapaa,
Wengi chini watambaa!


Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Umeme kuwa hadaa,
Na ahadi ni sanaa,
Kuigiza yote kuwa,
Sadifu ikapotea!


Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Ni maji kuyafukia,
Badala ya kutumia,
Na kiu ikasambaa,
Kila kona Tanzania!

Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Rasilimali kuzoa,
Wasiokuwa wazawa,
Katika wao ubia,
Na wakubwa walokuwa!

Pepo iwezayo kua, nchi ikahujumiwa,
Hatimaye kujakuwa, Jehanamu ya dunia ,
Wapo wa kulaumiwa:
Tofauti ikikua,
Kati ya wetu raia,
Masikini muishiwa,
Na tajiri tumbojaa!

No comments: