Tuesday, January 17, 2012

Marafiki kutokuwa

Pengine nimejaliwa, marafiki kutokau,
Ingenipata balaa, na mikosi kuingia,
Ningeweza jizuzua, kufa nikatangulia,
Marafiki kutokuwa, baraka yaweza kuwa!

Roho ningeisumbua, na wakati kupotea,
Hasara nikaingia, bila cha kujivunia,
Fakiri ningelikuwa, pasiwe wa kunijua,
Marafiki kutokuwa, baraka yaweza kuwa!

Nje ungeniumbua, na aibu kuivaa,
Mji nikaukimbia, na shamba kujahamia,
Jina nikalikataa, na lingine kulitwaa,
Marafiki kutokuwa, baraka yaweza kuwa!

Maradhi ungenitia, mwili yakanibomoa,
Watu kuninyanyapaa, ugonjwa wasiojua,
Sinema nikabakia, kizazi kunishangaa,
Marafiki kutokuwa, baraka yaweza kuwa!

Twafunza kwetu kutoa, shukrani ni tabia,
Na kisha kuhimidia, allahamdulillahi pia,
Si wenye kujayua, Mola aliyotupangia,
Marafiki kutokuwa, baraka yaweza kuwa!

No comments: