Tuesday, January 17, 2012

WAJINGA KUWAACHIA

Mahitaji ya msingi,
Hamsini kutimia,
Watu wetu bado wengi,
Kukosa watahiniwa?
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!


Usanii wazidia,
Iliyo sanaa mbaya,
Vipi ukiangalia,
Akili hutoijua:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Maji yameshapotea,
Miji yote ilokuwa,
Visingizio kadhaa,
Viongozi huvitoa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Nyumba haki yake mtu,
Roho zetu bado kutu,
Twaona kwenye misitu,
Wanafaa kutupiwa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Vijiji vinasinyaa,
Hali mali vingekuwa,
Nchi kuiingizia,
Milioni zilokuwa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Ugumu sijaujua,
Ila usanii wawa,
Wangelijipunguzia,
Haya yangelitokea:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Wakubwa wataka shiba,
Kwa wadogo kuwakaba,
Njaa zinawaziriba,
Muhali kuendelea:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Umeme wanawakaba,
Koo waliokwishakabwa,
Umeme au ubwabwa,
Maamuzi sasa kuwa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!


Hamsini yatimia,
Ni tano asilimia,
Umeme inayopewa,
Tena kwa kusuasua:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!


Kwengine ingelikuwa,
Nchi nzima ingekuwa,
Bei zikajishukia,
Nuru kuwa Tanzania:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Reli ninawaambia,
Ni shule kuifungua,
Profesa wa Ulaya,
Wasokazi kutumia:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Vijana kujitolea,
Posho wakachangiwa,
Huku kisomo wapewa,
Reli tutazifufua:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Ruia wanazootea,
Za kitajiri tambua,
Na hawa nawaambia,
Kwao tutanyong'onyea:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Wao wanafikiria,
Trilioni kumwaa,
Katu hazitoingia,
Njiani zitaishia:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!


Na hata zikiingia,
Wengine zitawafaa,
Na nchi ikalemaa,
Kama si nyuma kuvia:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Barabara nazo pia,
Twaweza kujipatia,
Shule zikiandaliwa,
Elimu kazi ikawa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Hatuwezi endelea,
Wengine kutegemea,
Mweupe wa kumwangalia,
Mweusi haitokuwa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Weupe wamezidiwa,
Ndugu wanawaangalia,
Kwao kinachobakia,
Wenyewe wakitumia:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Kwanza ninawashangaa,
Madini kuyaachia,
Kisha kujakupokea,
Vijisenti vilivyokuwa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Kama babu mmekua,
Mjerumani kumwachia,
Mali kubwa zilokuwa,
Kwa kupewa lawalawa?
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!


Madaraja nayo pia,
Na viwanja vya kufaa,
Michezo iliyokuwa,
Hadi tukajichumia:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Sindano ya Tan zania,
Ingali inatakiwa,
Aibu kuinunua,
Toka nje ya Afrika:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Mbona mnatembea,
Na Ulaya kuingia,
Vipi mnapofuliwa,
Ujanja kutoujua?
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Pampu mwaagizia,
Mbovu ziliziokuwa,
Na hasara kuingia,
Kila mwaka kwa mamia:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Msumbiji wachipua,
Wareno kuwatumia,
Kwao wasioajiriwa,
Sasa wajitengenezea:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!


Hata uzi na samani,
Zijetoka Marekani,
Huu si uhayawani,
Aibu pia fedheha?
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Meli mmeshaazimia,
Makaburi kuchukua,
Paseni kuichukua,
Baharini kuzikiwa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Hadhi mmeshaamua,
Mitumba inatufaa,
Uhai si manufaa,
Wingi mnaukataa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Ndege mmeazimia,
Mitumba kuzichukua,
Mbayuwayu akitua,
Nasi chini tuje tua:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Trekta mwatapeliwa,
Bei mbaya mwanunua,
Badala kujitengezea,
Imara zilizokuwa:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Mabasi tukiamua,
Si kioja yote kuwa,
Yatengenezwa Tanzania,
Mafundi wazidi jaa;
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

Malori nayo pia,
Babu alishaaisisia,
Kutengezwa Scania,
Hapa kwetu Tanzania:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!


Mafundi wazidi jaa,
Ulaya walikozaliwa,
Kazi zimewakimbia,
Riziki wajisakia:
Mashaveli kumjua, hata mimi huchukua,
Rahisi vilivyokuwa, magumu kujitia,
Tukayashughulikia, utata yaliyokuwa,
Hutamani kujitoa, katika hii dunia:
Wajinga kuwaachia!

No comments: