Tuesday, January 17, 2012

Iktisadi

Ikifika ya ahadi, jaribu iktisadi,
Hili lina ushahidi, ataudai Ahadi,
Nawe ukijalikaidi, vinginevyo kujinadi,
Yatakusibu jadidi, yasiyo nawe mradi,
Huyachelea Wadudi, kwa waje wake abdi,
Ila ijapo kubidi, ndio hutoa ahadi!
Na huyu ndiye Maajidi, Mwenye lengo na kusudi,
Usifanze ilimradi, ukakosa tawhidi,
Komalia zake sudi, uje nawe kufaidi,
Bidii nazo juhudi, acha ziwe yetu jadi!

No comments: