Thursday, January 26, 2012

Yuraniamu Tanzania hapana...


I hate Uranium, marauders spare my people
1.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Nchi inayolaaniwa,
Maajabu huamua,
Wizi wakishaujua,
Lolote watajifanyia,
Huongozwa na tamaa,
na mwisho sote twajua:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

2.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Bungeni ukiangalia,
Watu wengi wasinzia,
Hawa ndio Watanzania,
Dhamana mtawaachia
Mengi wanayoamua,
kichefuchefu yatia:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

3.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Wabunge wa kutegemewa,
Hofu sasa wanatutia,
Si wate wa kufikiria,
Bali ndiyo kuitikia,
Maamuzi yenye udhia,
Rahisi sana kuua:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

4.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Ni wavivu waliokuwa
Vigumu kujisomea
Miswaada kuipitia
Sio linalotarajiwa
Bungeni mbumbumbu wawa:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

5.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Marekani wakataa,
Makwao kuichimbua,
Kondomu na vyandarua
Sisi tukishapatiwa
Hili tunalikubalia?
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

6.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Katazameni dunia,
Kwingineko kulokuwa,
Yuraniamu inaua
Na ulemavu kusia
Viumbe wanazaliwa
Ajabu waliokuwa:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

6.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Ni heri kilema kuwa
Wa mwili unaovia,
Kuliko kilema kuwa
Wa akili kutumiwa
Na wazungu wenye njaa
Uhai wasiotutakia:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

7.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Ubepari wakolea,
Chamani unaenea
Wajamaa walokuwa
Uuaji wanadhamiria
Hakika nitawashangaa,
Yao mkiyasikia:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

8.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Uranium balaa
Tuepuke kukaribia
Vipo tulivyojaliwa
Havifai kuvifukua
Ni mizimu iliyokuwa
Ukishika walipuliwa:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

9.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Bado hatujafikia
Kuwa nayo kali njaa
Kama yao waheshimiwa
Ubinafsi walojaa
Mwenye njaa wasomjua
Mzigo wanaokuwa
Kwa nchi kutokuifaa:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

10.
Laana twawaombea, waidhinishao hili,
kuchimbwa Uranium, hapa kwetu Tanzania,
Wakati haujafikia, na hatujajiandaa,
ha hatunavyo vifaa, tahadhari kuchukua:
Hakimu twamgeukia
Mmiliki wa dunia
Haya tutamuachia
Uamuzi kufikia
Na tishio wanaokuwa
Kuhukumu linalofaa:
Uchu na zenu tamaa, tunawaonya wakubwa,
mauti mwatutakia!

Please Lord protect the ignorasmuses!

No comments: