Saturday, January 14, 2012

Viongozi bangaiza

Historia huua, ya kwao kuyafichiza,
Viogozi walokua, kazi wanabangaiza,
Hawarithi mapokeo, kila kitu hutekeza,
Viongozi bangaiza, historia huua !

Wizara wakichukua, kazi upya huanza,
Na idara kufatia, kumbukumbu hupoteza,
Kisa kilichosanzuliwa, wengine kutofatiza,
Viongozi bangaiza, historia huua !

Hizi zama za balaa, uovu watu wawaza,
Vyama vilivyofulia, au laana kuapizwa,
Huwa navyo vyaingia, na kisha vikateleza,
Viongozi bangaiza, historia huua !

Uongozi si sanaa, wala ploti kuigiza,
Huwaza na kuwazua, watu kukusikiliza,
Vinginevyo huwa ndoo, na maji kuyamwagiza,
Viongozi bangaiza, historia huua !

Hii ngoma ya majaa, sio uganga wa pweza,
Na tambo wanaozua, ni vigumu kuicheza,
Huishia kutitia, wawe kwa wengi kikwazo,
Viongozi bangaiza, historia huua !

No comments: