Saturday, January 21, 2012

Viongozi na Menejimnti

Viongozi walokuwa, haya kweli wanajua,
Wapi walikojifunzia, na kutia vitendoni,
Ni watu wa nadharia, au kazi watambua,
Si wanaobabia, na ujuzi kujitia,
Ya wengine kuvamia, kuacha wanayojua,
Kisha kuwaharibia, makosa kuwasingizia,
Haya ninayahofia, naamini yatokea,
Na wananchi wasojua, wazidi kuvumilia,
Laiti wangelijua, wangeishawasanzua,
Kwa kuwa si wanaojua, na nchi haitoendelea:

Kwanza kuna majukumu:
Kuna majukumu ya maingiliano na jamii;
Kiaha kuna majukumu ya habari na mawasiliano;
halafu kuna majukumu ya ufanyaji maamuzi bora!

Je, waziri wetu huyu, na katibu wake mkuu,
Mkuu wa mkoa huyu,na watumishi wadau,
Wanafahamu kazi zao ni pamoja na:

Uwakilishi:
Unatakiwa kuwakilisha waliokuchagua,
Na sio kujiwakilisha na kujilimbia,
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !

Kiunganishi:
Watakiwa kuyajua, nchini yanayotokea,
Na eneo lako likawa, moyoni lakaririwa,
Hapana linalotokea, bila wewe kuyajua,
Ndivyo inavyotokea, kwa polisi na raia?
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !

Kuongoza:
Kuongoza twatitia, hufanza tusiyojua
Elimu imepungua, bahati twategemea,
Hana wa kufikiria, jipya lililokuwa,
Nani kuonyesha njia, wakati wengi tunapotea?
Kwa maana hii nawaambia, kiongozi hajatokea:
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !


Msemzaji:
Taasisi yatakiwa, na msemaji kuwa,
Yote anayoelewa, nchini yanayotokea,
Kadhalika na dunia, na hiyo yake tasnia,
Vinginevyo bogasi anakuwa, mapapai ya kuliwa:
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !


Ukusanyaji:
Na habari kuzitoa, lazima kuzipokea,
Meneja anatakiwa, haya kufuatilia,
Habari zote zikawa, anajikusanyia,
Kisha akazitia, kwenye kompyuta kuwa,
Na chochote hunyanyua, akaweza kukupatia:
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !


Utawanyaji:
Na inavyoruhusiwa, watu hujawagtuimia,
Habari za historia, na zinazoendelea,
Hakuna litakalowia, ni gumu kulitambua,
Sayansi yanuia, vidoleni haya kuwa,
Maamuzi ukaamua, sahihi yaliyokuwa:
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !


Kugawa rasilimali:
Kugawa rasilimali, kiongozi atakiwa,
Ulimbikaji ajali, laana hulaaniwa,
Hata ukipata mali, mafunza huja kujilia,
Ukafa wewe bahili, hujui kuyatumia,
Na dhuluma kutumia, wana huwa ni vichaa,
Kizazi kikapotea, na jina kusahauliwa:
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !



Upatania masuala:
Shughuli kupatania, na watu kupatanisha,
Yataka kuvumilia, na watu kuunganisha,
Ubia ukauandaa, kuwafaa kimaisha,
Wao kuja kutambua, ustawi warahisisha:
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !


Mshindania bei nafuu na ubora wa vitu:
Mwenyewe ukijifaa, na hasara watu kutia,
Nuksi zitakufua, na kuzioga balaa,
Umri hujapungua, na neema kusinyaa,
Ikawa usiyefaa, katika pepo na dunia,
Na moto kukungojea, kwa nafuu kutoitoa:
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !


Mfanya maamuzi:
Maamuzi yatakiwa, haraka kujakutolewa,
Kusinzia ni nazaa, na kusahau balaa,
Kiongozi akijua, hili kwake ni dunia,
Na asipokulijua, ajipalia mkaa,
Viumbe hawakuuzaliwa, milele kujakaa,
Hamsini ikitua, wengi budi kujifia:
Na usipoamua, ukawa unachelewa,
Watu wakijifia, lawama wazichukua,
Huwezi mtu kumfaa, kama akishajifia:
Tajiri ukijakua, na sifa kujipatia,
Na unaowatumikia, umasikini wazidia,
Wewe sio kiongozi, bali dhulumati, mbinafsi, njaa kali,
Mhamishaji, mnywaji na mlaji tu !


mwisho/2012.o1.21

No comments: