Wednesday, November 30, 2011

Makalio kuwa nje

Mshairi nashagaa, katakei walokua,
Majina sijatambua, kuitwa nini wafaa,
Kila nikiwaangalia, naona kama bidhaa?
Makalio kuwa nje, ni shoga au ni mende?

Wanawake naelewa, wateja wanavutia,
Kina blaza sijajua, nini wanafukuzia,
Chupi ikitokezea, na makalio bwabwajaa,
Makalio kuwa nje, ni shoga au ni mende?

Kama shoga sijajua, au mende wamendea?
Wazazi mwawaangalia, au mmechanganyikiwa,
Kama dini msojua, na vitabu mwasomea?
Makalio kuwa nje, ni shoga au ni mende?

Huu si Utanzania, yakini naukataa,
Kuiga kulikokua, taahira walokua,
Huku wanajidhania, ni wazima walokua,
Makalio kuwa nje, ni shoga au ni mende?

No comments: