Tuesday, November 22, 2011

Nilinde

Ulinde ulimi wangu, usidhuru viungo vyangu,
Na linda mkono wangu, usiwadhuru wenzangu,
Ilinde akili yangu, isitamani Uungu,
Naulinde moyo wangu, nisitamani vya wenzangu,
Nahami fikra zangu, nisiige ya wenzangu,
Yalinde mawazo yangu, yasiwe husuda kwangu,
Na kihami chakula changu, kisije kuwa njaa yangu,
Na mlinde mke wangu, asiwe kifo cha utu wangu,
Na waokoe wanangu,wasiwe machungu yangu,
Nilinde jamaa zangu, wasiwe zahama yangu,
Nilinde na wafuasi wangu,wasiwe mashaka yangu,
Na yatunze maji yangu, yasije kuwa sumu kwangu,
Ulinde uongozi wangu. usiwe mauti kwa wenzangu,
Usifanze ukubwa wangu,uwe mwisho wa chama changu,
Ponya ubinafsi wangu,usiwe ndio mauti yangu!

No comments: