Wednesday, November 30, 2011

Weza chelewa uishi

Weza chelewa uishi, alowahi ende kufa,
Hii ni yetu aushi,na haya yake maarifa,
Huzua kama mzushi, tena pasipo kashfa,
Weza chelewa uishi, uwahi uende kufa.

Maisha kama nakshi,hupuputika wasifa,
Umri ni kama moshi, humalizika masafa,
Hauna tija ubishi, haujajenga orofa,
Weza chelewa uishi, uwahi uende kufa.

Bahati ni bakshshi, na wala haina ofa,
Huli la mwenzio dishi, hata apate kifafa,
Na wala hapana mzishi, ukiandikiwa mofa,
Weza chelewa uishi, uwahi uende kufa.

Hundi haijawa keshi, ayajua hata lofa,
Njia hauirekebishi, akiichora latifa,
Ukileta ushawishi, hukukuta yaso sifa,
Weza chelewa uishi, uwahi uende kufa.

No comments: