Wednesday, November 30, 2011

Tarafu

Si watu wa kukinai, huo sio mwendo wao,
Hawa watu bila rai, hulinda nafsi yao,
Wengine hawawajui, ila kwa matamanio,
Tarafu hawaijui, bado wataka kula wao.

Mengine ni goigoi, haraka si mwendo wao,
Haki hawatanabahi, ila iwe ni ya kwao,
Hawadai maslahi, nayo kama siyo yao,
Tarafu hawaijui, bado wataka kula wao.

Hawa ni wetu nabii, wenyewe wajichaguao,
Zama hizi za uhai, haya ndiyo wavunayo,
Si kama ninakebehi, huu ndio ukweli wao,
Tarafu hawaijui, bado wataka kula wao.

Ni rahisi yao bei, gharama waibebayo,
Hutoi9na nishai, utaridhi wasemayo,
Ukiona hayafai, wawa ni mtaji kwao,
Tarafu hawaijui, bado wataka kula wao.

Kandili si karabai, huelewa wajuao,
Nazi haijawa tui, bila lako kamulio,
Na chunusi sio ndui, usimuache mkeo,
Tarafu hawaijui, bado wataka kula wao.

No comments: