Thursday, June 28, 2012

Maji yako mgongoni



Ajabu inatokea, hapa kwetu duniani,
Kifuani waingia, kusaka ya mgongoni,
Na kofia wazivua, na nikahi  kuzitoa ?
Maji yako mgongoni, watafuta kifuani ?

Mgongoni yametua, watafuta kifuani,
Ukweli waukataa, na akili hatiani,
Viroja wanvizua, muhali wakabaini,
Maji yako mgongoni, watafuta kifuani ?

Washindwa angalia, Mbelgiji kafanzani,
Na Aishi nakujua, hoteli ya Machameni,
Mashine imetulia, ibura iwafnzieni,
Maji yako mgongoni, watafuta kifuani ?

Mbowe hili alijua, mashine ni ya zamani,
Maji inayaibua, tokea huko bondeni,
Juu yakayanyua, na kwingia hotelini,
Maji yako mgongoni, watafuta kifuani ?

Maji moa yaufaa, Tabora ni Tanganyikani,
Mengine hayo sanaa, tena mkubwa utani,
Mgongoni kunyanyua, yataingia mtaani,
Maji yako mgongoni, watafuta kifuani ?

No comments: