Monday, June 18, 2012

Aabuduye Wazungu


Aabuuduye wazungul, hubaki na makamasi,
Akaiona mizungu, na mkubwa wasiwasi,
Asozawa na uchungu, aweje na udamisi ?
Aaabuduye Wazungu, hubaki na makamasi !

Chungu hakiwi mkungu, na nazi  haiwi nasi,
Lake haliwi ni langu, kwa kidogo na kiasi,
Sijaujua mvungu, urefuwe kinamasi,
Aaabuduye Wazungu, hubaki na makamasi !

Ni heri mlaji dengu, choroko sio nuksi,
Watayapanga mafungu, tena pasipo uasi,
Wakaukuza undugu, kwa ndoa nazo harusi,
Aaabuduye Wazungu, hubaki na makamasi !

Wazungu watu wa tangu, yetu hawajayaanisi,
Nchi kwao ni mkungu, ndizi wanatanafusi,
Zinapofunuka mbingu, hata nazo huakisi,
Aaabuduye Wazungu, hubaki na makamasi !

Ukimfanza ni Mungu, kwake huwa ni rahisi,
Hukufanya ni kijungu, akakutia yabisi,
Akakulisha na kungu, uzidi kuwa mwepesi,
Aaabuduye Wazungu, hubaki na makamasi !

Hapa kwetu hana fungu, ila kwao wadamisi,
Wamejitia vifungu, kuifunga kadamasi,
Fungate yenye uchungu, na kuibiwa kwa nafasi,
Aaabuduye Wazungu, hubaki na makamasi !

Siyajui ya wenzangu, siyapendi makamasi,
Na mafua ya uchungu,yatiayo wasiwasi,
Ningekimbia wazungu, Wachina kuwadurusi,
Aaabuduye Wazungu, hubaki na makamasi !

No comments: