Thursday, June 28, 2012

Jimbo hili jimbo langu




Mchama kachachamaa, jimbo keshalinunua,
Wengine anakataa, kwake wasije ingia,
Macho wakawafumbua, wale aliowahadaa,
Jimbo hili jimbo langu, mwaja kufuata nini ?

Ni lake kang'ang'ania, hataki kuingiliwa,
Uongo akiuzua, pasiwe wa kumuumbua,
Na wizi akitumia, pasiwe wa kutambua,
Jimbo hili jimbo langu, mwaja kufuata nini ?

Uhuru aulilia, kwa udhaifu kuujua,
Bango anashikilia, la binafsi manufaa,
Na koaja ajivalia, la mfalme juha,
Jimbo hili jimbo langu, mwaja kufuata nini ?

No comments: