Kuna vyama Tanzania,
vya watu vyawaibia,
Ndarahima kunyakua, eti zao kujitia,
Kisha wanatumwaiya, wapate kututumia,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Benki kuu hupakua, mfukoni wakatia,
Watu njaa wakilia, makombo wanagawiwa,
Hazina yapakuliwa, sahani safi zikawa,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Chama kimeingilia, ya serikali kutwaa,
Tumboni wakafukia, vyingi vya kuvibangua,
Nchi mifupa ikawa, yatisha ikitembea,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Ndio wanaviopoa, vya umma vilivyokuwa,
Wao wakajidhania, ndio nchi wamekuwa,
Hofu hawajaijua, umma kuwashtakia,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Ni wizi tunaujua, jingine haliwezi kuwa,
Yafaa kuwaambia, dhuluma wameingia,
Na nchi sasa yalia, wao hawajasikia?
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Na nchi sasa yalia, wao hawajasikia?
Yao
yananyakuliwa, hali wanaangalia,
Na waliowategemea, imani imepotea,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Nchi inabakuliwa, na waliodhaminiwa,
Viongozi wananywea, hawataki kusikia,
Miaka yajiishia, na mengi yanapotea,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Na sasa wametokea, wizi wanaokataa,
Ufakiri waujua, walivyo Watanzania,
Kweli wanawaambia, mfukoni wanapwaya,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Michango wajiombea, wanachama kuitoa,
Na pia wote raia, dhuluma wanaokataa,
Ije demokrasia, iokoke Tanzania,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Watu wawanyenyekea, yao
kutokuwaibia,
Jasho lao wakatoa, halali kukichukua,
Chama kujijengea, kisafi kilichokuwa,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Wengine wanatumia, kuwakusanya jamaa,
Na kisha wakajitia, wanachama waingia,
Vibaka na changudoa, hadi ndani wamejaa,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Hali kimeshazidiwa, kutapatapa kwamea,
Hakiwezi chini kaa, mikakati kuizua,
Nyadhifa waliopewa, giza
mbele imekua,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Miradi wamefulia, upya wafikiria,
Uchama umechachua, hata vipya vyaugua,
Watuwe wameishiwa, mawazo wayadokoa,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Kila mwenye kubagua, vyote akavichukua,
Huja akafilisiwa, akose lilo jipya,
Yake yote huja via, akaanza kulemaa,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Dhulumati walokuwa, laana huwatambaa,
Ikizidi kuingia, huwa wachanganyikiwa,
Ndiyo yanayoteokea, mwisho hatujaujua,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Usiache kuchukua, kitu wakikupatia,
Kisha sadaka kutoa, chama safi kupatia,
Zimwi likawarudia, nje waliloachia,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Kisha kura kuitumia, kwa wasafi walokuwa,
Wachafu wakafulia, kwenye jalala kwingia,
Ndiyo yanayowafaa, kwenye mpya Tanzania,
Huwa wanaviopoa, kisha watu kugawia,
Nasi tumewaelewa, kutuomba kuchangia:
Uadillifu twaujua !
Uadilifu twajua, kumbukumbu yabakia !
No comments:
Post a Comment