Saturday, June 2, 2012
Mwalimu mwenye ajenda
Wanafunzi hatufai, mwenye ajenda binafsi,
Mwalimu mwenye nishai, elimuye wasiwasi,
Hata kama ni digrii, pengine ni kinamasi,
Mwalimu mwenye ajenda, binafsi hatufai !
Ni mtu wa kukinai, kama vile makamasi,
Si kwa nazi wala tui, yalo yake wasiwasi,
Na hata ukimrai, haitambui nafusi,
Mwalimu mwenye ajenda, binafsi hatufai !
Mtu wa namna hii , ualimu anahasi,
Kumchagua jinai, ndani ana ibilisi,
Kitu chema hakizai, bali dhiki na maasi,
Mwalimu mwenye ajenda, binafsi hatufai !
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment