Monday, June 18, 2012

Usanii unakwisha



Ukikoma uigizaji, utaisha usanii,
Mvua ikiwa maji, hewa haifikirii,
Wajinga na wajuaji, ndoa yao haikai,
Uigizaji ukikoma, usanii utaisha !

Mlaji sio mkaji, yake huwa hayakui,
Fundi hamzidi gwiji, ndoo yake haijai,
Hauwezi kunywa uji, ikawa sawa na chai,
Uigizaji ukikoma, usanii utaisha !

Si mtenzi mwigizaji, ndo maana hafulii,
Wa kinywaji na kilaji, tui wala halijui,
Usimpe mfamaji, mkono hauachii,
Uigizaji ukikoma, usanii utaisha !

Kadhalika mshukaji, kwa mkono humsalimii,
Kama wewe mpandaji, awweza kunanihii,
Na daraja sitaraji, siri zangu siachii,
Uigizaji ukikoma, usanii utaisha !


No comments: