Thursday, June 28, 2012

Haki yet u kudanganya



Chama chetu ni ruhusa, kuiba na kubakua,
Leseni tumeshapewa, nani ataka zuia,
Nchi nzima tumejaa, makaburi kuchimbua,
Haki yetu kudanganya, wengine hawana haki !

Makaburi kuchimbua, haki za kuizikia,
Na usawa kukataa, sisi pekee tukawa,
Wajinga wawe waliwa, pasiwe wa kuulizia,
Haki yetu kudanganya, wengine hawana haki !

Kibali tumeamua, wenyewe tunakitoa,
Nani atayekataa, na mpini twajishikia,
Makali tukiachia, wote nyie mtaumia,
Haki yetu kudanganya, wengine hawana haki !

Kuiba tukiamua, saa yote twachukua,
Ni yetu yanshakuwa, serikali jina yawa,
Chama kimeshikilia, nani wa kukikosoa,
Haki yetu kudanganya, wengine hawana haki !

Kudanganya ni tabia, yabidi kuendelea,
Wajinga Watanzania,c hama chetu kinajua,
Kijani ikiingia, na njano inafuatia,
Haki yetu kudanganya, wengine hawana haki !

Kijani ikiingia, na njano hufuatia,
Wao basi hupagawa, yote wakatuachia,
Dawa yetu yawafaa, hawana wanalojua,
Haki yetu kudanganya, wengine hawana haki !

Kuwapiga ni tabia, na maji kuwamwagiwa,
Pilipili yalojaa, nao wanafurahia,
Aklili zimewalegea, kitu gani wanajua ?
Haki yetu kudanganya, wengine hawana haki !

No comments: