Monday, June 18, 2012

Ushoga kukaribia


Ni ugonjwa wa tabia, za ukwasi na kinaya,
Wale waliojaliwa, baraka kuichukia,
Na halali kilokuwa, wakawa wakikataa,
Ushoga kukaribia, waweza kukuathiri !

Haramu hutamkia, ndicho huchangamkia,
Nani wa kumsikia, si adhana wa kutia,
Wala mnadi swalaa, na maji wa kuchotea,
Ushoga kukaribia, waweza kukuathiri !

Sikio vigumu dawa, kuweza kuiskia,
Bure utaliumbua, uziwi ukaingia,
Vyema ni kuyaambaa, na mbali sana kukaa,
Ushoga kukaribia, waweza kukuathiri !

Kizazi kikiujua, kitataka kurejea,
Ni mafunzo yatolewa, ole wanayoendea,
Mwana usiyemlea, chochote aweza kuwa,
Ushoga kukaribia, waweza kukuathiri !

Tusiifate dunia, wana wakatupotea,
Vyema kujiangalia, na rafiki kuchagua,
Watu mkiwavamia, mtakuja jijutia,
Ushoga kukaribia, waweza kukuathiri !

Subira inatakiwa, na mwendo kuangalia,
Tusitwae lawalawa, roho tukaziachia,
Na wanaonisikia, ushahidi nimetoa,
Ushoga kukaribia, waweza kukuathiri !

Na wanaoyaachia, wengi wao twawajua,
Madawa walianzia, sasa ushoga watia,
Kesho hatutaijua, pengine waje kuua,
Ushoga kukaribia, waweza kukuathiri !

Ninamuomba Jalia, haya kutuepushia,
Isije kuwa balaa, juu jengine balaa,
Nchi ikalaaniwa, na vizazi kufatia,
Ushoga kukaribia, waweza kukuathiri !


No comments: