Tuesday, March 27, 2012

Wakimbia ushindani

Mbona mnavuta kamba, hamtaki ushindani,
Hivi sasa mnagomba, kwa kukosa ukinzani,
Nchi nzito kama mimba, hamtaki afueni?
Wakimbia ushindani, wataka ukiritimba ?

Mzigo mmeusomba, tena mwatia kichwani,
Njiani mwatoka shamba, letni niwabebeeni,
Kibaka mnanichamba, ni mwizi na mhuni?
Wakimbia ushindani, wataka ukiritimba ?

Ugonjwa umewakumba, kutokea viwandani,
Na sokoni mwauimba, na feri na mnadani,
Mmeshindwa kuimba, nyimbo ziko mkononi?
Wakimbia ushindani, wataka ukiritimba ?

Mnajipaka mavumba, samaki mwatupa chini ?
Heri mnayoikumba, mwasema si yenu thamani?
Mashavu yanawavimba, ibilisi mtadhani,
Wakimbia ushindani, wataka ukiritimba ?

No comments: