Tuesday, March 27, 2012

Mbona vyanzo viko vingi ?

SUBIRA huvuta kheri, nami ninangojea,
Nitakuwa ni msiri, ndarahima kunuia,
Vyombo kuvishauri, uchumi wapate jua,
Mbona vyanzo viko vingi, mwang'ang'ania vichache ?

Nangoja halmashauri, hodi kunipigia,
Niwape yangu khabari, nipate kuwastua,
Wakazigundua siri, uchumi wameketia,
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?

No comments: