SUBIRA huvuta kheri, nami ninangojea,
Nitakuwa ni msiri, ndarahima kunuia,
Vyombo kuvishauri, uchumi wapate jua,
Mbona vyanzo viko vingi, mwang'ang'ania vichache ?
Nangoja halmashauri, hodi kunipigia,
Niwape yangu khabari, nipate kuwastua,
Wakazigundua siri, uchumi wameketia,
Haki kwavyo ving'amuzi, mbona hamuwapi wengi?
Tuesday, March 27, 2012
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment