Kuna muda na wasaa, na kitambo kupitia,
Majira usipojua, dakika zitapotea,
Ukija kuhesabiwa, masaa yemetimia,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Dahari hatukupewa, ni sekunde twaachiwa,
KIla zinapochepua, ngozi zetu zikavia,
Na pumzi huchelewa, mengi tukajichokea,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Bahati ikiwajia, bado wataichambua,
Kisha hujiinukia, mbele ikaendelea,
Halafu huangukia, pua zao kuumia,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Wa msimu huingia, upepo wa kulowea,
UKiisha wapepea, heri wakategemea,
Ukiwawageukia, kama ukichaa huwa,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Wastani huachia, zaidi kukimbilia,
Huko akishaingia, nakisi huigundua,
Nyuma akigeukia, tayari kimetwaliwa,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Uzuri atachagua, akakuta walemaa,
Rijali akivizia, akakuta una waa,
Na mme mke huwa, katika hii dunia,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Akili akifatia, huingia ukichaa,
Bora alichochagua, kikawa kinamchachia,
Werevu akaezua, mvi
akajipambia,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Mali hukimbilia, uzani ukatitia,
Mbio hapo husanzua, kwingine kuelekea,
Hali akatarajia, atakuta iko sawa,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Huko akafumania, nayo yamejichachia,
Katikati hubakia, kama amenatishiwa,
Akiweza kujitoa, nusura huwa kulia,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Kikaango hukimbia, motoni akaingia,
Huruma hatoijua, hadi majivu akawa,
Huo mwisho wake kuwa, akaiga dunia,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Ndivyo ilivyo dunia, ya mchezo na sanaa,
Saburi inaijua, kisha mkubwa wasaa,
Haraka haijaijua, ila inapojifungua,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Hchounachojionea, lenga hapo na kutua,
Kibakaika radhia, hatua utapotea,
Mwanangu binti kukaya, huu ni wangu wasia,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
Sijisumbue na kung'aa, huja kuwa ni balaa,
Mtake wako Jalia, ombilo kukuridhia,
Ibada mkiijua, yeye atawaangalia,
Kila mchagua sana, hubaki kuhangaika !
No comments:
Post a Comment