Sunday, November 18, 2012

Yako yaweje aghali


Raia ukiachia, ovyo ya kwao yakawa,

Yako ukaangalia, ya ndugu nao jamaa,

Ninashindwa kutambua, vipi bora utakuwa,

Yako yaweje ni ghali, ya kwetu kama rahisi ?



Rahisi yao yakiwa, hivi ghali yako kuwa,

Dharau ukiitia, utakuwa mheshimiwa,

Fakiri wakijikwaa, ukwasi utafurahia,

Yako yaweje ni ghali, ya kwetu kama rahisi ?



Bado najiulizia, na jibu sijapatiwa,

Juu anayeingia, zaidi ataendelea,

Au hapo kafikia, mwisho palipoishakuwa,

Yako yaweje ni ghali, ya kwetu kama rahisi ?



No comments: