UZIMA uliyepewa, shilingi ya kununua ?
Mtu akakutumia, kama bidhaa ukawa,
Haya kutojionea, na kesho kutohofia ?
Hudanganywa kwa shilingi, watu wajinga wakawa !
Shilingi kweli maua, tena moyo inaua,
Aibu ikaitoa, haya mbali kuulia,
Mtu akaabudiwa, muumba asiyekuwa,
Hudanganywa kwa shilingi, watu wajinga wakawa !
Mushiriki kwenda kuwa, kiumbe akalaniwa,
Akaikosa janaa, na kupoteza dunia,
Na roho akitolewa, abaki kujijutia,
Hudanganywa kwa shilingi, watu wajinga wakawa !
Thursday, November 8, 2012
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment