Sunday, November 18, 2012
Mambo ni kufatilia
UDHIBITI kipungua, tija nayo hupungua,
Kazi wanaopangiwa, budi kufuatiliwa,
Wafanyacho kukijua, na kinavyoendelea,
Mambo ni kufatilia, sio ovyo kuachia !
Ovyo ukiyaachia, hawezi kufanikiwa,
Lazima utafulia, wengine wakaogea,
Feli zataka hatua, mja zote kuzijua,
Mambo ni kufatilia, sio ovyo kuachia !
Vipimo kuvichukua, mambo ukalingania,
Kujaa ukakujua, pia hata kupungua,
Hasara na manufaa, iwe rahisi kujua,
Mambo ni kufatilia, sio ovyo kuachia !
Ndivyo ilivyo dunia, na maisha yatambua,
Vingine yakiachiwa, huw amkubwa udhia,
Kila mwenye kuyajua, ni akili hutumia,
Mambo ni kufatilia, sio ovyo kuachia !
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment