Sunday, November 18, 2012

Mambo ni kufatilia




UDHIBITI kipungua, tija nayo hupungua,

Kazi wanaopangiwa, budi kufuatiliwa,

Wafanyacho kukijua, na kinavyoendelea,

Mambo ni kufatilia, sio ovyo kuachia !



Ovyo ukiyaachia, hawezi kufanikiwa,

Lazima utafulia, wengine wakaogea,

Feli zataka hatua, mja zote kuzijua,

Mambo ni kufatilia, sio ovyo kuachia !



Vipimo kuvichukua, mambo ukalingania,

Kujaa ukakujua, pia hata kupungua,

Hasara na manufaa, iwe rahisi kujua,

Mambo ni kufatilia, sio ovyo kuachia !



Ndivyo ilivyo dunia, na maisha yatambua,

Vingine yakiachiwa, huw amkubwa udhia,

Kila mwenye kuyajua, ni akili hutumia,

Mambo ni kufatilia, sio ovyo kuachia !

No comments: