Sunday, November 18, 2012
T U S U B I R I
Mimi mtu wa saburi, haraka naiachia,
Lenu lenye ushauri, siwezi kulikataa,
Na kama nikusubiri, hilo nimeliridhia,
Tungojee, tusubiri, nami nasubiri nanyi !
Hamwezi kuomba heri, shari nije wagaia,,
Ninalijua kaburi, na ndani kinachokuwa,
Hilo kwangu sio siri, uhai sijafulia,
Nanyi nami nasubiri, kifuatacho kujua !
Ishara mkidhamiri, siwezi waongopea,
Mimi sio mashuhuri, na utume sijapewa,
Hata huo ubashiri, ni yangu najisemea,
Nanyi nami nasubiri, kifuatacho kujua !
Hakika sina jeuri, ya nuru kukaribia,
Ila kinachodhihiri, huazimu kuwaambia,
Ila pali0o sifuri, duarani hubakia,
Nanyi nami nasubiri, kifuatacho kujua !
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment