Sunday, November 18, 2012

T U S U B I R I


Mimi mtu wa saburi, haraka naiachia,

Lenu lenye ushauri, siwezi kulikataa,

Na kama nikusubiri, hilo nimeliridhia,

Tungojee, tusubiri, nami nasubiri nanyi !



Hamwezi kuomba heri, shari nije wagaia,,

Ninalijua kaburi, na ndani kinachokuwa,

Hilo kwangu sio siri, uhai sijafulia,

Nanyi nami nasubiri, kifuatacho kujua !



Ishara mkidhamiri, siwezi waongopea,

Mimi sio mashuhuri, na utume sijapewa,

Hata huo ubashiri, ni yangu najisemea,

Nanyi nami nasubiri, kifuatacho kujua !



Hakika sina jeuri, ya nuru kukaribia,

Ila kinachodhihiri, huazimu kuwaambia,

Ila pali0o sifuri, duarani hubakia,

Nanyi nami nasubiri, kifuatacho kujua !



No comments: