Sunday, November 18, 2012

Watoto wanaoua




Naiuliza dunia, ukweli ikanambia,

Tofauti sijajua, watoto wanaoua,

Na Hitler mlaniwa, yahudi aliyeua,

Yahudi walioua, na watoto wanaoua:

Wana tofauti gani ?



Kila nikiangalia, tofauti sijajua,

Ninachokiangalia, ni mama waliofiwa,

Watoto wawalilia, nani faraja kutia?

Yahudi walioua, na watoto wanaoua:

Wana tofauti gani ?



Sabbu tena kwa mamia, wanaweza kuzitoa,

Ila hatutaelewa, huruma twajionea,

Kimbari kinatokea, watu wanaangalia ?

Yahudi walioua, na watoto wanaoua:

Wana tofauti gani ?



Rahmani yangu dua, siwachi kukuachia,

Haya umeyaachia, bado yanaendelea,

Sababu unaijua, mimi sijaigundua,

Yahudi walioua, na watoto wanaoua:

Wana tofauti gani ?



No comments: