Sunday, November 18, 2012
Watoto wanaoua
Naiuliza dunia, ukweli ikanambia,
Tofauti sijajua, watoto wanaoua,
Na Hitler mlaniwa, yahudi aliyeua,
Yahudi walioua, na watoto wanaoua:
Wana tofauti gani ?
Kila nikiangalia, tofauti sijajua,
Ninachokiangalia, ni mama waliofiwa,
Watoto wawalilia, nani faraja kutia?
Yahudi walioua, na watoto wanaoua:
Wana tofauti gani ?
Sabbu tena kwa mamia, wanaweza kuzitoa,
Ila hatutaelewa, huruma twajionea,
Kimbari kinatokea, watu wanaangalia ?
Yahudi walioua, na watoto wanaoua:
Wana tofauti gani ?
Rahmani yangu dua, siwachi kukuachia,
Haya umeyaachia, bado yanaendelea,
Sababu unaijua, mimi sijaigundua,
Yahudi walioua, na watoto wanaoua:
Wana tofauti gani ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment