Friday, November 2, 2012
Kofi la Mungu lauma
UKIKIZIBWA kibao, hakika hukisikia,
Kofi lisilo na ngao, huwezi kulizuia,
Pigo lake ni chaguo, kwenda likiazimia,
Kofi la Mungu lauma, hasa kama waliona !
Kwa Obama ni mwambado, juzi lilikochagua,
Kuna mayowe na kilio, ijapa wasidiwa,
Na onyo walijuao, mapema waliambia,
Kofi la Mungu lauma, hasa kama waliona !
Nawaza kwa siku hiyo, habari pasipokuwa,
Na watu ni walalao, 'singizini wajifia,
Tsunami si mwenzao, huruma itasikia?
Kofi la Mungu lauma, hasa kama waliona !
Al Gore mtukwao, haya aliwaambia,
Taasisi iko mbio, elimu imeshagawa,
Watu wapiga miayo, hawataki kuyajua,
Kofi la Mungu lauma, hasa kama waliona !
Sio tu wao kwao, hata na sisi pia,
Sio tusikiayo, haya tunayoambiwa,
Mazingira tuchafuao, wenyewe tunajiua,
Kofi la Mungu lauma, hasa kama waliona !
Halinao mwelekeo, kofi la Mungu nazaa,
Mbaki meno msagao, radhi likishawamwagia,
Na hakuna tegemeo, mwenyewe anabakia,
Kofi la Mungu lauma, hasa kama waliona !
Bure tujizuzuao, ya Mola kuyachezea,
Kesha kaa mkao, zawadi kutugawia,
Na sisi si tujuao, hadi yanapotokea,
Kofi la Mungu lauma, hasa kama waliona !
Ya kwetu matamania, kitanzi yaije kuwa,
Jalia uwe ni ngao, ya kufaa kuamua,
Tusitafute kilio, kwa ukubwa kujitia,
Kofi la Mungu lauma, hasa kama waliona !
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment