Sunday, November 18, 2012

Mwizi wa fikira




Mwizi wa fikira mwizi, kingine hawezi kuwa,

Tabiaye udokozi, ya watu kuyachukua,

Kisha kwenda kuyahodhi, kuwa yake kujitia,

Fikra mwenye kuiba, sikuzote huwa mwizi !



Watazame waenezi, jinsi wanavyodokoa,

Hii ndiyo yao kazi, sasa wanaajiriwa,

Na utundu hawawezi, jema wakalipanua,

Fikra mwenye kuiba, sikuzote huwa mwizi !



Wageuka wachuuzi, wakubwa kuwauzia,

Wakaachia machozi, Baadi kuwaachia,

Mrahaba kuwaizi, ya kwao wakajilia,

Fikra mwenye kuiba, sikuzote huwa mwizi !



Anayaona mwenyezi, sadaka sasa watoa,

Kwake bado wana enzi, siku ya kuahidiwa,

Kisha wote majambazi, huko kwenda kudaiwa,

Fikra mwenye kuiba, sikuzote huwa mwizi !



No comments: