Sunday, November 18, 2012

VIJIJI



Vijiji mkipuuza, mijini kutakalika ?

Si watu mwawakimbiza, mijini kuja furika ?

Ajizi mnayofanza, vigumu kueleweka,

Mkipuuza vijiji, kutakalika mijini ?



Jambo hili lashangaza, mipango 'kiangalia,

Ghafla tulijaikwaza, katikati kuachia,

Hivi leo tunaiza, hata kwenda tembelea ?

Mkipuuza vijiji, kutakalika mijini ?



Twashindwa kujieleza, upacha uliokuwa,

Vijiji Kulwa mpuuzwa, na Doto muweza njia ?

Usawa tusiposambaza, udugu utaachia,

Mkipuuza vijiji, kutakalika mijini ?



Tukajazua ya viza, uhuni na mabalaaa,

Wakashtuka ajuza, na shaibu kujikwaa,

Wataraji miujiza, uovu ukazuia,

Mkipuuza vijiji, kutakalika mijini ?





No comments: