Sunday, November 18, 2012

NAULIZA TANZANIA ?



Swali najiandikia, na sitaki kujibiwa,

Niacheni kuzubaa, na kisha nikapumbaa,

Ni ligumu ninajua, sio mnavyofikiria,

Itajengwa Tanzania, na wanaonunuliwa ?



Wenyewe wameridhia, na makofi kupigiwa,

Kuuza na kunnua, ni halali imekuwa,

Nini unatarajia, kwa tunakoelekea ?

Itajengwa Tanzania, na wanaonunuliwa ?



Bidhaa tumeshakua, nani wa kulikataa,

Wakubwa wameamua, biashara kuingia,

Wao wajifagilia, wengine ubaya kuwa,

Itajengwa Tanzania, na wanaonunuliwa ?



Rushwa imetunukiwa, nani wa kuikimbia,

Chama kimenakshiwa, rangi zake kuzivaa,

Ukitaka kung'amua, tafsiri kuijua,

Itajengwa Tanzania, na wanaonunuliwa ?



Wahaka umenijaa, anzali nimeshakuwa,

Kila nikifikiria, nashindwa kujitambua,

Watu niliowadhania, wamegeuzwa bidhaa ?

Itajengwa nchi hii, na wanaonunuliwa ?



No comments: