Wednesday, November 14, 2012
Binadamu akishindwa
Nafasi yake masaa, binadamu hajajua,
Na analoliamua, lilikwishaandikiwa,
Yeye tu anatumiwa, kuwa njia kupitia,
Binadamu akishindwa, hivi Ally atashindwa ?
Mola akilikataa, jambo haliwezi kuwa,
Hata ubabe kutumia, nguvu huja kuishiwa,
Likawa linalokuwa, silo unalotarajia,
Binadamu akishindwa, hivi Ally atashindwa ?
Yote tumeandikiwa, na vingine haijawa,
Usijie kujua, eti wewe watufaa,
Mpanda hujushushua, mshuka akaenziwa,
Binadamu akishindwa, hivi Ally atashindwa ?
Utukufu kujitia, uchafu hukuingia,
Tena ukakusambaa, kila mtu kuujua,
Ila dhaifu ukiwa, hutoacha barikiwa,
Binadamu akishindwa, hivi Ally atashindwa ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment