Sunday, November 18, 2012

Uhuru asiye nao



Hawi mtu wa busara, uhuru asiyekuwa,

Mtu huyo wa hasara, huwezi kumtumia,

Huwa ni simba marara, hata fisi hukimbia,

Uhuru asiye nao, hawi mtu wa busara!



Hawezi nukuu sura, wala aya kufatia,

Maisha yake kuchora, kuandika hatajua,

Duniani husowera, hawezi kutangulia,

Uhuru asiye nao, hawi mtu wa busara!



Uzee huwa madhara, na watu hatowafaa,

Akaingia ujura, viporo kuambulia,

Akillilia nusura, kwa kesho asiyeijua,

Uhuru asiye nao, hawi mtu wa busara!







No comments: