Sunday, November 18, 2012

TAIFA BILA YA BABA ...


UBABA waukataa, uchamawanalilia,

Hayo ndiyo majaliwa, mwanangu binti mkiwa,

Babu kakuondokea, na baba hukujaliwa,

Taifa bila ya baba, huwa ukiwa mkubwa !



Baba mwema ni ulua, wana wanajivunia,

Nyumbani akiingia, huwa wamkimbilia,

Na kicheko kuangua, shibe wakajishibia,

Taifa bila ya baba, huwa ukiwa mkubwa !



Na baba asipokuwa, nyumba huwa yatitia,

Ukimya ukajaa, na giza ndani ikawa,

Nuru yote hupotea, na unyevu kuingia,

Taifa bila ya baba, huwa ukiwa mkubwa !



No comments: