Sunday, November 18, 2012
TAIFA BILA YA BABA ...
UBABA waukataa, uchamawanalilia,
Hayo ndiyo majaliwa, mwanangu binti mkiwa,
Babu kakuondokea, na baba hukujaliwa,
Taifa bila ya baba, huwa ukiwa mkubwa !
Baba mwema ni ulua, wana wanajivunia,
Nyumbani akiingia, huwa wamkimbilia,
Na kicheko kuangua, shibe wakajishibia,
Taifa bila ya baba, huwa ukiwa mkubwa !
Na baba asipokuwa, nyumba huwa yatitia,
Ukimya ukajaa, na giza ndani ikawa,
Nuru yote hupotea, na unyevu kuingia,
Taifa bila ya baba, huwa ukiwa mkubwa !
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment