Wednesday, November 14, 2012
Asiyekuwa na nuru
Haya hawezi elewa, na nuru asiyekuwa,
Ardhi imeshushiwa, wachache sana kufaa,
Adili wanaojua, na tajwidi kutia,
Asiyekuwa na nuru, haya hawezi elewa !
Nia wanaoitia, kazini hawajaingia,
Mola akatangulia, nao nyuma kufatia,
Taa wataichukua, hadi kaburini kwingia,
Asiyekuwa na nuru, haya hawezi elewa !
Kila wanaloamua, misingi wakifatia,
Yumkini kujaliwa, huwa lishakubaliwa,
Vingine haitakuwa, katika hii dunia,
Asiyekuwa na nuru, haya hawezi elewa !
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment