Wednesday, November 14, 2012
mwanzo wa kuheshimiwa
UCHAFU ukiingia, nyingine hakuna dawa,
Bali kuzawa upya, ya kwanza ukaanzia,
Na nani atakwambia, ya kwanza yanavyokuwa ?
Ni upya ukizaliwa, mwanzo wa kuheshimiwa !
Na nani atakwambia, ya kwanza yanavyokuwa ?
Kuanzapo yatakiwa, kishake yakachanua,
Na jinsi ya kuyalea, ujana ukarejea?
Ni upya ukizaliwa, mwanzo wa kuheshimiwa !
Huanza kwa kuchungua, walo safi kuwajua,
Kisha ukawaachia, safu wakajipangia,
Wenyewe wanajijua, wengine wasiojua,
Ni upya ukizaliwa, mwanzo wa kuheshimiwa !
Usafi waliojaliwa, nyuso zao zinang'aa,
Unafiki ukitoa, hutoacha kuwajua,
Nao wakikuanglia, macho utayakimbia,
Ni upya ukizaliwa, mwanzo wa kuheshimiwa !
Ni rahisi kuwajua, kama dhambi wakimbia,
Na shetani wamtoa, ashindwe na kulegea,
Hao wanapobakia, malaika huingia,
Ni upya ukizaliwa, mwanzo wa kuheshimiwa !
Mtume hawatojitia, au unabii kuzua,
Dhaifu wanaokuwa, tena kimya wakaa,
Watu wakaangalia, jinsi wakijipitia,
Ni upya ukizaliwa, mwanzo wa kuheshimiwa !
Wametosheka radhia, na Mola awafurahia,
Yao amesharidhia, na milango kfuungua,
Kiburi msipotia, hamuachi watambua,
Ni upya ukizaliwa, mwanzo wa kuheshimiwa !
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment