Sunday, September 26, 2010

Kiongozi hamjui mwenye dhiki

Unaishi kwenye nyumba ya fahari,
Ewe kiongozi mwema wa wanadamu,
Wananchi wako ijapo ni hodari,
nyumba bora kwao bado ni kitu adimu,
Stima yakupa kila akheri na bukheri,
watu wako hawaishi kulaumu,
Uhuru zama uliwapa kiasi jeuri,
leo nyuso zakunjika kama ndimu,
Hawasikilizi la kheri wala la shari,
Bei kila leo zinawahasimu,
Husikilizi kabisa wao ushauri,
ila ule tu wa wataalamu,
Wanaotaka aghalabu ughaibu,
na wasiotofautisha sifuri na dhahiri,
Ndio hao sasa wanaotakadamu,
na bora kwako ni wa kwao ushauri,
Wengine wameanza kuwatuhumu,
magari, safari na nyumba ndogo utitiri,
Badala sasa ya nyie kuombewa heri,
watu kulia na kushoto wawaombea shari,
Naomba wakubwa wangu msinilaumu,
Ujumbe huu nimetumwa nami si mtabiri!

No comments: