Monday, October 15, 2012

Mganga kajigangua






Qulu lany yuksibuna, lahuu laana huwa,

Aya iliyo bayana, tamko imeshatoa,

Sikuchelewa kuvuna, kupanda nawaachia,

Mganga kajigangua, alipoikuta dua!



Na dua alipokutana, mganga kajiumbua,

Kwa jicho twatazamana, mkubwa kanitajia,

Mwanaizaya mtwana, nikamhurumia,

Mganga kajigangua, alipoikuta dua!



Aliye na Maulana, malaika huwa'chia,

Vidole wakivikuna, udhia ukapotea,

Mie hofu kwangu sina, walinzi nawaachia,

Mganga kajigangua, alipoikuta dua!



Bure mnapotezana, katika hii dunia,

Moto mwaupuliza sana, wa kwenda kuungulia,

Kama haya mwayakana, afu nadra kupewa,

Mganga kajigangua, alipoikuta dua!





No comments: