Tuesday, October 16, 2012

Bahati haina kwao



Aliyenayo hajui, kuidharau tabia,
Kazoea kama tui, kwenye wali kuitia,
Akawa haiwazii, hadi asiposikia,
Bahati haina kwao, kuhama matarajio!

Huingia pasi hodi, ndani ikakufuatia,
Wala sio kwa mrai, na nai kuipigia,
Wala haina ahadi, mara unaishtukia,
Bahati haina kwao, kupata matazamio!

No comments: