Monday, October 15, 2012

M S I P O K I C H A G U A





Chama mkikiachia, kwenda kujipumzikia,

Haitakuwa nazaa, huenda mkabarikiwa,

Miaka kikaogea, na usafi kujitia,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



JIKI mkaitumia, kuyaondoa madoa,

Mizizi iliyokuwa, ya rushwa inayokomaa,

Halafu mkaondoa, na magugu kuyang'oa,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Kizazi kipya kutwaa, wazee mkawatoa,

Pembeni wakendakaa, wajukuu wakalea,

Sabini waliozaliwa, chama wakakichukua,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Muda huu watakiwa, chama kujajijengea,

Matawi mkafagia, uoza uliojaa,

Mbegu kujipandia, mpya zitakazokuwa,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Ubaya anayedhania, kifo hajakielewa,

Huku sio kujifia, bali upya kuzaliwa,

Wazee kama bidhaa, kwenye chama wamejaa,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Wazee kama bidhaa, na mzigo waliokuwa,

Kwenye chama wamejaa, ovyo wananunuliwa,

Ili hawa kuwaondoa, kushindwa kwenu ni njia,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Taifa kusaidia, nalo upya kujizaa,

safu zikapanguliwa, kilicho bora kwenziwa,

Yaliyovia manufaa, angalau kurejea,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Hakuna cha kusifiwa, kila kitu wameua,

Kwao kilichobakia, ni sadaka kungojea,

Ombaomba wamekuwa, hatuwezi wategemea,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



No comments: