Wednesday, October 31, 2012

Huwa mithili kombora



MEPESI kuyasikia, yasiingie moyoni,
Ila yakishatukia, huupata usononi,
Kugalagala ikawa, dunia huitamani,
Matoni wakiliona, huwa mithili kombora !

Ukweli utafukia, ukawa nayo yakini,
Hawawezi kugundua, yako wasiyoamini,
Njia ukakazania, na kujipamba thamani,
Matoni wakiliona, huwa mithili kombora !

Ila siku hufikia, likaingia machoni,
Na urembo likatiwa, ujikute ulimboni,
Vipi utalikimbia, giza uliloaamini,
Matoni wakiliona, huwa mithili kombora !

Magumu kuyaelewa, yabkiyo kweny mboni,
Kifikra nachelewa, hojaze kuziamini,
Nisije singiziwa, miye sikuwa makini,
Matoni wakiliona, huwa mithili kombora !

No comments: