Wednesday, February 29, 2012

Moja uanyoipewa

MWANA unanishtua, kwa unayoniambia,
Iweje ikatokea, moja wewe kupokea,
Kisha ukatoa mia, na mgeni kumwachia:
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Umeshindwa kuelewa, uchumi ulojisomea,
Akilini umekua, mweupe watakatia,
Huu ujinga najua, si vingine kunambia:
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Huwezi kutoa mia, wewe moja wapokea,
Tena ukashangilia, na fahari kufanyia,
Na kisha kumzawadia, moja anayesaidia:
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Utaahira nahofia, nyumbani umeingia,
Kila nikiangalia, si vingine nawambia,
Sasa nataka kujua, hayo misyonambia:
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Wa wapi mwawatumia, wataalamu walokuwa,
Nini wamesomea, na kama haya wanajua,
Au wanawapatia, kwa wenzao kuwanunua ?
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Angefufuka radhia, haya angeyakataa,
Majuha angewaambia, mwakubali nunuliwa?
Mwashidwa kufkiria, katika hii dunia:
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Katika hii dunia, kama mpya imekuwa,
Asia mgeingia, mengi mngeyavua,
Yapo ya kumalizia, na kisha kuendelezea,
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Mapya mngeyazua, ya wengi zaidi kufaa,
Na sio kuzainiwa, wachache yakawafaa,
Wanangu mnapotea, ukweli ninawaambia,
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Wanangu mnapotea, ukweli ninawaambia,
Utandawazi mwavia, na sasa mnaibiwa,
Pupa mmeingilia, wenyewe mpate jifaa?
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Nchi mwaiachia, kama malaya imekua,
Kila mtu mwachukua, hata wezi walokuwa,
Utakarifu wavaa, kumbe masheteani wawa,
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Mwapasa kuangalia, tena sana kuchunua,
Wengine wanaowajia, Ibilisi wanakua,
Na nyie mkizuaa, nchi mwenda iua,
Moja unayoipewa, na wewe mia kutoa:
Aidha una kichaa
Au umelogwa pia
Au njaa wapagawa
Ya shetani ilokuwa
Na mwepesi kuja ua
Na kisha ukafukia
Bila ya watu kujua!

Shabiki si mzalendo

Michezo sio siasa, na siasa si mchezo,
Michezo budi hamasa, mikazo na mashikizo,
Na anasa kuzisusa, pamwe pasiwe mizozo,
Shabiki si mzalendo, mzalendo mshindani:
Asokubali kushindwa,
Kwa kuwa na kilichoundwa,
Wachezaji kuwezeshwa!

Michezo yataka panga, na wala si kupangua,
Michezo yataka anga, tanafusi na kutua,
Michezo yataka twanga, na wala si kutenguliwa,
Shabiki si mzalendo, mzalendo mshindani:
Asokubali kushindwa,
Kwa kuwa na kilichoundwa,
Wachezaji kuwezeshwa!

Ushindani kukimbia, sio kurudi nyuma,
Michezo budi hatua, kujua na kung'amua,
Moyoni wasiokuwa, hawawezi kutufaa:
Shabiki si mzalendo, mzalendo mshindani:
Asokubali kushindwa,
Kwa kuwa na kilichoundwa,
Wachezaji kuwezeshwa!

Michezo ni kukomaa, mazoezi na afya,
Chakula kinatakiwa, na vinywji kujinywea,
Mtiririko ukawa, katu usiopungua:
Shabiki si mzalendo, mzalendo mshindani:
Asokubali kushindwa,
Kwa kuwa na kilichoundwa,
Wachezaji kuwezeshwa!

Ushabiki Tanzania, njaa uliozidiwa,
Watu wanashabikia, vibovu vilivyokuwa,
Huku wamategemea, maajabu kutokea,
Shabiki si mzalendo, mzalendo mshindani:
Asokubali kushindwa,
Kwa kuwa na kilichoundwa,
Wachezaji kuwezeshwa!

Makocha wanatakiwa, hilo hatujakataa,
Na walimu waliokuwa, wajua saikoljia,
Na kisomo kugawia, watu wakajikomboa:
Shabiki si mzalendo, mzalendo mshindani:
Asokubali kushindwa,
Kwa kuwa na kilichoundwa,
Wachezaji kuwezeshwa!

Visiki tunavilea, ni lazima kujikwaa,
Viongozi wachaguliwa, mashaka wananitia,
Kama wanaganga njaa, au kuongoza wajua:
Shabiki si mzalendo, mzalendo mshindani:
Asokubali kushindwa,
Kwa kuwa na kilichoundwa,
Wachezaji kuwezeshwa!

Heri kujinyamazia, kwa macho kuangalia,
kama mbali twafikia, olympiki ikiwa,
Tayari nimeotea, watupu twajirudia:
Shabiki si mzalendo, mzalendo mshindani:
Asokubali kushindwa,
Kwa kuwa na kilichoundwa,
Wachezaji kuwezeshwa!

Midomo na maneno hayashindi !!!!

WATANZANIA shabashi, fundi wa kuzungumza,
Tabasamu na ucheshi, vichache wanaviweza,
Umebaki ushawishi, historia kujuza,
Tunacheza kwa mdomo, na wenzetu kwa mguu:
namna hii tutashinda ?

Usanii twabakia, kimichezo tumekwisha,
Na tuanowachagua, mazishi tunawatwisha,
Ujuaji ukikua, ndio mwisho wa maisha,
Tunacheza magazeti, na wenzetu kiwanjani:
hivi kweli tutashinda?

Mipango twaipangua, na siasa kuzitia,
Wataalamu twaachia, wazawa waliokuwa,
Na kwenda kuwavamia, watalii wa dunia,
Tunacheza kwa tivii, wenzetu kwa mikakati:
hivi kweli tutashinda?

Michezo yataka nia, mipango nazo hatua,
Viwanja ukaanzia, safi vilivyonakshiwa,
Vikatosheleza vifaa, mazoezi kufanzia,
Tunacheza kisiasa, wenzetu kiushindani:
hali hii tutashida ?

Majengo yanatakiwa, kwa michezo ya kulea,
Ndani inayotakiwa, uzio yakajengewa,
Kila kitu ndani kuwa, pasiwe kinachopungua,
Tunacheza kwa mdomo, na wenzetu kwa mguu:
namna hii tutashinda ?

Vifaa vinatakiwa, mbalimbali vilokuwa,
Navyo vya kununua, na kujitengenezea,
Ajira tunazichezea, wakati hakuna vifaa?
Tunacheza magazeti, na wenzetu kiwanjani:
hivi kweli tutashinda?

Walimu wanatakiwa, mizizi waliokuwa,
Mfano wao Zambia, na wa nje kukodiwa,
Ratiba kuiandaa, ya mwaka mzima ikawa,
Tunacheza kwa tivii, wenzetu kwa mikakati:
hivi kweli tutashinda?

Misitu inatakiwa, mazoezi kufanyia,
Ya kupanda na kutua, na wala sio asilia,
Mandhari kunyanyua, bora zilizojaliwa,
Tunacheza kisiasa, wenzetu kiushindani:
hali hii tutashida ?

Huko zana zikatiwa, pamwe na vyote vifaa,
Mtu aweza kukaa, siku nzima katulia,
Mazoezi kufanzia, hadi akajichokea,
Tunacheza kisiasa, wenzetu kiushindani:
hali hii tutashida ?

TFF huu kuwa, na sio kuingiliwa,
Na hao wanaojijua, wajua na wasiojua,
Talanta wakaishapewa, mwisho wa mwaka kuzaa,
Tunacheza kwa mdomo, na wenzetu kwa mguu:
namna hii tutashinda ?

Vijiweni twaingia, na soka kujichezea,
Timu tukajipangia, ushindi kuja chukua,
Uwanjani wakitua, nguo zote wavuliwa,
Tunacheza kwa mdomo, na wenzetu kwa mguu:
namna hii tutashinda ?

Magazeti Tanzania, namba wani yamekuwa,
Yacheza kama Zambia, kwa maneno kuyatoa,
Na kisha kujishangilia, uwanjani bado tua,
Tunacheza kwa mdomo, na wenzetu kwa mguu:
namna hii tutashinda ?

Kucharangwa hufatia, wote kimya wakawa,
Kama wangelijua, ni mbali wangeanzia,
Maandalizi kwingia, wahamasishe kwa nia,
Tunacheza magazeti, na wenzetu kiwanjani:
hivi kweli tutashinda?

Mazoezi kufatia, ndani na nje yakiwa,
Hadi timu kujaliwa, viwango ikafikia,
Na kisha kuhesabia, vile vinavyotakiwa,
Tunacheza kwa tivii, wenzetu kwa mikakati:
hivi kweli tutashinda?

Wazee kuwaondoa, wakati umewadia,
Timu mpya kuzaliwa, vishindo kuhimilia,
Kila siku twawajua, hawa waliojichokea,
Tunacheza kisiasa, wenzetu kiushindani:
hali hii tutashida ?

Mbona kubwa Tanzania, na thelathini mikoa,
Twashinda kujipatia, kumi na moja walokuwa,
Bora na wa kidunia, tuionyeshe dunia?
Tunacheza kisiasa, wenzetu kiushindani:
hali hii tutashida ?


Februari 29, 2012
Sudusia (1/6) ya 2012.
Dar es salaam. Tanzania.

Tuesday, February 28, 2012

Usijisifie kwa mema

VIUMBE wasio haya, si kazi kujisifia,
Ndio wasiojaliwa, hutaka kujinyanyua,
Hata kwa yasiyokuwa, watu hali wawajua,
Usijisifie mema, ukayavua mabaya
!


Kiumbe umelemewa, na wewe unayajua,
Vipi unayachukua, usoweza kuchukua,
Au haujatambua, kwamba ndefu sana yako njia,
Usijisifie mema, ukayavua mabaya!

Kiumbe wapungukiwa, halijajaa gunia,
Vipi unalitoboa, na begani kulitia,
Njiani halitoishia, nawe bila ya kujua?
Usijisifie mema, ukayavua mabaya!

Kiumbe waharibikiwa, wadhani wabarikiwa,
Hali ya hewa wachafua, wadani unaifagia,
Nahofu utapaliwa, ukweli ukijaujua,
Usijisifie mema, ukayavua mabaya!

Mema unajisifia, watu usowatendea,
Mazuri wajivalia, nje ukawavutia,
Hali ndani umejaa, uchafu wa kutitia,
Usijisifie mema, ukayavua mabaya!

Ya watu wachangamkia, yako yanakushushua,
Nje unapalilia, hali ndani hujasia,
Kila nikikuangalia, nashindwa kukuelewa,
Usijisifie mema, ukayavua mabaya!

Ndani nanga budi tia, ndiko kutakakokufaa,
Vinginevyo utapwaya, siku yakikutokea,
Yako usiposhikiliya, wengine ukaachia,
Usijisifie mema, ukayavua mabaya!

Wema ndani hutakiwa, kwako ukajiotea,
Kisha ukapalilia, na daima kuulea,
Nyuma yako hutulia, na Rabi kuwajalia,
Usijisifie mema, ukayavua mabaya!

Wema ukishautoa, soma njema yako dua,
Mlipaji ni mmoya, wa pili hajatokea,
Ahadi keshaitoa, mwongozo ukiangalia,
Usijisifie mema, ukayavua mabaya!

Punje ndogo azijua, na hesabu aitia,
Hapana cha kupotea, hulipwa kitu sawia,
Vingine haijakuwa, amini na zingatia,
Usijisifie mema, ukayavua mabaya!

Miradi ya kuibia raia

WAMEIZUSHA tabia, wananchi kuwaibia,
Wanatakiwa kutoa, hata wasichojaliwa,
Hii shari inakuwa, zahama naihofia:
Miradi ya kuibia, raia mnayozua,
Viongozi nawaonya
Mwatakiwa angalia
Msije zua balaa!

Wema watashingilia, kauli ninayotoa,
Maana wanatambua, mbele yanayowangojea,
Dhuluma waichelea, na haramu kukimbia:
Miradi ya kuibia, raia mnayozua,
Viongozi nawaonya
Mwatakiwa angalia
Msije zua balaa!

Ila wabaya najua, tena sana wachukia,
Makaa ya moto haya, sasa wanayojilia,
Masikini wanajua, ni uhondo uliokuwa:
Miradi ya kuibia, raia mnayozua,
Viongozi nawaonya
Mwatakiwa angalia
Msije zua balaa!

Ila siwezi chelewa, ukweli wangu kutoa,
Sitaki kuwahadaa, uongozi sintogombea,
Kweli tupu ninatoa, na Mola namwangukia:
Miradi ya kuibia, raia mnayozua,
Viongozi nawaonya
Mwatakiwa angalia
Msije zua balaa!

Unafiki umejaa, kwenye zetu manispaa,
Ukweli tunaujua, ila tunauambaa,
Tunaoneana haya, wabaya kuwafichua,
Miradi ya kuibia, raia mnayozua,
Viongozi nawaonya
Mwatakiwa angalia
Msije zua balaa!

Manasara nawajua, haya amri zakataa,
Hata dini wasokuwa, maovu wanajua,
Vipi mliochaguliwa, na walioteuliwa?
Miradi ya kuibia, raia mnayozua,
Viongozi nawaonya
Mwatakiwa angalia
Msije zua balaa!

Vipi mliochaguliwa, na walioteuliwa?
Mnataka kunambia, dhambi hamjaijua,
Wakazi mwawafanyia, hali vipofu mkiwa?
Miradi ya kuibia, raia mnayozua,
Viongozi nawaonya
Mwatakiwa angalia
Msije zua balaa!

Wenyewe mnajiua, na kizazi kujavia,
Kiwe kilicholaaniwa, kwa haramu kutumia,
Hadi wajukuu kuwa, maaluni na vichaa:
Miradi ya kuibia, raia mnayozua,
Viongozi nawaonya
Mwatakiwa angalia
Msije zua balaa!

Mola mkimgeukia, thuma mtasamehewa,
Kwake mkisharejea, miji bora itakuwa,
Ukaondoa udhia, kwa wageni na raia:
Miradi ya kuibia, raia mnayozua,
Viongozi nawaonya
Mwatakiwa angalia
Msije zua balaa!



Februari 28, 2012.
Dar es Salaam. Tanzania.
East Africa.

Minyororo ya migogoro

Tenda zingine kama wizi

WATU wanasumbuliwa, kwa sheria za udhia,
Wakubwa mliyoamua, ni maudhi yamekuwa,
Mwatakiwa angalia, au wote tutalia:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Tenda mnawapatia, hadhi wasiofikia,
Na wanayojifanyia, wizi sasa inakuwa,
Mapema msipwatoa, wakazi watawatoa:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

La magari chukulia, zima linalotembea,
Pembeni ukiegeshea, waja kulifungia,
Minyororo wakatia, brekidauni kuchukua,
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Laki mbili wachukua, haijui manispaa,
Au ni yao sanaa, kwa nyuma wanapokea?
Hili watu waumia, kilio nawalilia:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Mkataba naujua, hamsini ulikuwa,
Dalali anachochukua, thelathini kutimia,
Na jiji huambuliwa, ishirini ya bandia:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Ni nani anayeliwa, hapa ukiangalia,
Mwenyewe unamjua, sitaki kumwongelea,
Taahira asipokuwa, hasira hatoilea?
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Tenda zilishatolewa, takataka kuzizoa,
Na hao waliopewa, leo hoi wamekua,
Fedha bado yaingia, huduma zayoyomea:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Stendi ukiingia,Mwislamu ulokuwa,
Huwezi jisaidia, aibu tupu imejaa,
Kweli tunaendelea, hali kama hii ikiwa:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

GOGORO nawamwagia, facebook mwanijua,
Tulonge kuwaondoa, huduma bora ikawa,
Mkiuchoka udhia, basi leo mtanaambia:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Februari 28, 2012.
Dar es Salaam. Tanzania.
East Africa.

Ya nchi yanatushinda

UKISHAJITEGEMEA, ya wengine angalia,
Sio unategemea, uwezo ukajitia,
Msaada ukipungua, na wengine huumia,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Ndivyo nchi yatakiwa, mambo yake kupangia,
Sio ikajishushua, kuvaa itakayovua,
Bila ya kuendelea, wasanii mnakua,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Moja, mbili, tatu kuwa, hesabu inayotakiwa,
Huwezi ukarukia, kwingine ukavamia,
Huonekana kichaa, au mwehu umekuwa,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Kimbelembele tukiwa, wenyewe tutaumia,
Fashioni haijawa, shoo ya kutoendelea,
Kufanywa yanatakiwa, sio ya kuhadithia,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Nchi ikishaendelea, wengine inavutia,
Kamba hautochukua, kuvuta ukang'ang'ania,
Wenyewe wataingia,ya kwao wakachagua,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Taifa likishakua, heshima huzawadiwa,
Watalii wakapaa, na kuja hapa kutua,
Ndarahma kutwachia, zikawa na manufaa,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Zikitumika sheria, si ubabe kutumiwa,
Wote kushughulikiwa, bila ukubwa kutia,
Wote kujiinamia, katiba kuangukia,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Njiani tukitembea, pasiwe juu wakaa,
Yao wakayaamua, na wao wakatiiwa,
Hata ikiwa kuua, na bado wakachiwa,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Wasafi tukishakua, nchi ikawa yang'aa,
Pasiwe harufu mbaya, katika yetu mitaa,
Watatukimbilia, hata tusiowajua,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Kipaumbele twavia, mambo yanajiendea,
Hata yapaswayo kuwa, kwa sasa yanatukataa,
Kila ukiangalia, maongozi yafifia,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Mlima umepotea, vichuguu vimejaa,
Kwa mchwa sasa valiwa, hakuna linalokuwa,
Watu ni kujisifia, na mali kujilimbikia,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Kalima nimeitoa, na samahani natoa,
Pale nilipokosea, naomba kusamehewa,
Mimi mja nisojua, ajuaye ni Allaa,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Mimi mja nisojua, ajuaye ni Allaa,
Mkubwa aliyekuwa, na juu ameulia,
Apaswaye abudiwa, wengine shiriki huwa,
Mimi mja nisojua, ajuaye ni Allaa,
Ya nchi yanatushinda, twafata ya ulimwengu?

Februari 29, 2012.
Dar es Salaam. Tanzania.
East Africa.

Monday, February 27, 2012

RAIS AWE MWANAMKE!

Mbili ziro moja tano


KWA MIAKA hamsini, wanaume wanapewa,
Waja hadi utosini, hakuna linalokuwa,
Wameshindwa yaniyani, mimi mmoja nikiwa:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!


Nyerere wa kwanza kawa, twamshukuru radhia,
Mazuri katufanyia, na mabaya nayo pia,
Islamu twatambua, ila twajinyamazia:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Mwinyi alipoingia, makubwa tulidhania,
Hivyo katu haikuwa, palepale twabakia,
Ila njaa kupungua, twampa asante hewaa,
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Mkapa kumpokea, kisasi tunakijua,
Lipi lililotufaa, ila yao yalokuwa,
Ila barabara hewaa, sasa tunaitumia:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Wengine watuchagua, maua tumeshakua,
Ila nchi yasogea, nyuma mbele hatujajua
Sasa hali imekuwa, mbaya kwa tusiokuwa:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Vjijini wanalia, ugumu umezidia,
Na maji yamepotea, japo waliahidiwa,
Kuni zinawakimbia, zaenda zinakokua:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Na mjini nako pia, familia zateketea,
Baba wanazikimbia, ugumu ulivyokuwa,
Asema twaendelea, siriye hatujaijua:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Matatizo yalokuwa, wanawake wayajua,
Ndio yanyowavaa,asubuhi kuanzia,
Hadi jioni kwingia,hakuna wa kupumua:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Waume watuzidia, wezi wanavyoujua,
Na uongo wakatoa, kweli ukawakubalia,
Mwanamke akiingia, wizi budi kupungua:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Ufisadi nakwambia, mwanamke hukimbia,
Wengine hufikiria, watakavyokujaumia,
Halali hukimbilia, na haramu kukataa:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Trafiki ukitoa, rushwa wanaikataa,
Labda wanapotumiwa, na wanasiasa wakiwa,
Ila ya fedha baa, hili wanalitambua:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Matanuzi huambaa, na wanaume si sawa,
Ubadhirifu hadaa, vya watu utavitumia,
Hili wanalitambua, na kufanya ni nazaa:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Angalia Liberia, sasa inaendelea,
Wivu tu unawajaa, wanaume wasopewa,
Haweshi kuyazomea, mazuri yaliyokuwa:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Argentina tulia, nao nakuelezea,
Uchumi sasa wakua, mzee kujiondoa,
Na hata alipojifia, nchi yajititimua:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Ukenda Australia, mama anashikilia,
Dume limeondolewa, kwa kuuzusha udhia,
Uchumi wao wapaa, dunia inashangaa:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Nafuu natamania, miaka kumi ikawa,
Nyumbani wakabakia, wanaume mabalaa,
Ili kuiangalia, Tanzania itavyopaa:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Ili kuiangalia, Tanzania itavyopaa,
Mama rais akiwa, na watu kuwanyanyua,
Sijali atatokea, chama gani kilichokuwa:
Mbili ziro moja tano, Rais wa Tanzania:
Budi awe mwanamke!

Mkiongozwa na waongo

Mkiongozwa raia, na waongo walokuwa,
Njia mnaifungua, mabaya zaidi kuwa,
Ibilisi asifiwa, kwa uongo kuuzua:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!


Kwalo atawajalia, pasiwe wa kuwang'amua,
Majoho kuwashonea, ya utukufu kuvaa,
Pasiwe wa kuwadhania, kuutunga wanajua:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Hapa wakishafikia, uovu wote hujua,
Waweza kukukatalia, haikuumbwa dunia,
Na kuwa wameshushiwa, na kiongozi mzawa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Vyombo wakikabidhiwa, vibaya huvitumia,
Akili wakafumua, nyengine kuwapatia,
Wasiwe wa kujijua, kufanya yenye udhia:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Kama mbwa watakuwa, mabwana kutumikia,
Kwa furaha kuwabwkea, na wengine kugugumia,
Ya kheri yakapotea, ikabakia balaa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Waongo huweza ua, waseme hiyo ni dawa,
Mgonjwa aliyopewa, ndiyo iliyomkataa,
Au kuishi kakataa, kwani juu atakiwa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Nchi wataibomoa, kujgenga wakadhania,
Nguzo wanazotumia, uongo zilizojaa,
Vigumu kuyachukua, yote yenye manufaa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Kinachokujakubakia, ubabe na kujikwaa,
Si wa kutegemea, waongo waliokuwa,
Ni ukoma wawavaa, vyema mbali nao kukaa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Si wanaojitambua, mchezo wanadhania,
Majukumu walopewa, rahisi kuyachukua,
Kumbe wanatuchimbia, makaburi hai twawa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Vikao hujifungia, uongo kuupakua,
Wakishakujipikia, uongo kutugawia,
Na sisi tusiojua, kweli tukaitikia:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Hata tusipoujua, au mambo kuyaelewa,
Mola awaangalia, wasanii walokuwa,
Nao awakadiria, adhabu kubwa ikawa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Uwongo autambua, kabla haujatolewa,
Na wizi kaandikia, hesabu iliyokuwa,
Na dhuluma aijua, kabla haujazaliwa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Kumbe wanatuchimbia, makaburi twapumua,
Sio kwamba wakosea, hili vyema walijua,
Ila mbinu imekua, kutokujauliziwa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Ni nchi iliyolaniwa, ya waongo ilokuwa,
Husema wasiyojua, na kutosema wakijua,
Husema wakufufua, kumbe waenda kuua:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Hata wakijititimua, dunia huwaumbua,
Mbegu hazitochipua, na mimea haitomea,
Na kilichochanua, matunda hakitotoa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Kiapo hujiapia, bila aibu wakawa,
Na kisha kuyaingia, yaliyoishakataliwa,
Na katiba kupindua, kwa nia wanazojua:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!


Ninakuomba Jalia, taifa kuangalia,
Warongo kuwaondoa, wakweli tukabakia,
Radhiyo kutushukia,
nchi ikabarikiwa:
Mwongozwapo na waongo, uongo waliosomea,
Mwishowe huwafanyia, wakauzusha uongo,
Wenyewe mmejiua, au ni kifaurongo,
Kufufuka mwatarajiwa:
Budi kuwapa msongo,
Kwa kuanzia usogo,
Pamoja na zao hongo,
Mnyanyue wenu ungo,
Wenyewe mkajirushia!

Waniua taratibu

Taratibu waniua, kila ukiniangalia,
Nyimbo unayoghania, moyoni yaniingia,
Kisha waangalia, kama moyoni watua,
Waniua taratibu, nami naona adha bu:
Kupenda ninaogopa!

Taratibu najifia, sithubutu kuzoea,
Kujaribu nakataa, na kuweza sijajua,
Ila nilichoshudia, mikono imeungua,
Waniua taratibu, nami naona adha bu:
Kupenda ninaogopa!

Sumaku yashabikia, vyuma inajivutia,
Miye ninashupalia, kuondoka haitokuwa,
Hapahapa ninakaa, hadi nguvu kukwishia,
Waniua taratibu, nami naona adha bu:
Kupenda ninaogopa!

Sitaki kukaribia, maafa ninayajua,
Heri mwanzo inapokuwa, mwisho huja kujutia,
Kila alojeruhiwa, hatari huzikimbia,
Waniua taratibu, nami naona adha bu:
Kupenda ninaogopa!

Waniua polepole

Laiti ungelijua, hapa nilipotulia,
Muziki nausikia, laini uliokuwa,
Maneno unayotia, moyoni yanaingia,
Waniua polepole, kwa wimbo unaouimba!


Naona yanielekea, kila nikiyachungua,
Nguo zangu yanivua, na uchi nikabakia,
Na wala sijakujua, nawe haujanijua,
Waniua polepole, kwa wimbo unaouimba!

Waimba kama wajua, kile ninachofikiria,
Mawazo wayachukua, yangu ninayowazia,
Kwenye wimbo ukatia, kama wanizungumzia,
Waniua polepole, kwa wimbo unaouimba!

Nabakia kushangaa, roho moja tumekua,
Na moyo wanipalia, na kwikwi kunikamia,
Natamani kujitoa, siwezi kujinyanyua,
Waniua polepole, kwa wimbo unaouimba!

Masahibu ya dunia, unayoyaelezea,
Yamefinika radhia laiti ungelijua,
Ninazidi kuumia, ninatamani kulia,
Waniua polepole, kwa wimbo unaouimba!

Laiti ungelijua, ungeleta kitambaa,
Machozi nikafutia, na kisha kukurejeshea,
Ungeujua ukiwa, moyoni uliokuwa,
Waniua polepole, kwa wimbo unaouimba!

Laiti ungelijua, mkono ungenigea,
Nipate kukuegemea, wakati ninatembea,
Nyumbani nikarejea, kwenda mwenyewe kulia,
Waniua polepole, kwa wimbo unaouimba!

Laiti ungelijua, wimbo ungelichagua,
Mwingine kujiimbia, kama huu usiokuwa,
Machozi nisingetoa, pasiwe pole kupewa,
Waniua polepole, kwa wimbo unaouimba!

Wanasiasa fuska

MADHAMBI yakiingia, yakazidi kujizaa,
Kwenye safu za dunia, wakubwa walikokaa,
Muumba hatochagua, nani wa kumuumbua:
Taifa hulaaniwa, kati yao kuwa nao:
Wanasiasa fuska
Hupata watu wabaya
Kahaba wakachagua
Na wezi waliokuwa
Uongozi wakatwaa
Mambo yote ovyo kuwa
Mikosi pia balaa!

Hasira humalizia, pale inapoanzia,
Mwenye hurruma akawa, kama mbogo elfu mia,
Sauti akapasua, hadi nyota kukimbia:
Taifa hulaaniwa, kati yao kuwa nao:
Wanasiasa fuska
Hupata watu wabaya
Kahaba wakachagua
Na wezi waliokuwa
Uongozi wakatwaa
Mambo yote ovyo kuwa
Mikosi pia balaa!

Husasan akijua, wanaoharibu ndoa,
Kwa zinaa kuingia, na wengine kutumiwa,
Majonzi makubwa huwa,
viumbe wema wakalia:
Taifa hulaaniwa, kati yao kuwa nao:
Wanasiasa fuska
Hupata watu wabaya
Kahaba wakachagua
Na wezi waliokuwa
Uongozi wakatwaa
Mambo yote ovyo kuwa
Mikosi pia balaa!

Siasa zinachafua, majumba yaliyotulia,
Hakuna salama ndoa, hali tete imekua,
Na baadhi ya mikoa, wanafunzi watumiwa,
Taifa hulaaniwa, kati yao kuwa nao:
Wanasiasa fuska
Hupata watu wabaya
Kahaba wakachagua
Na wezi waliokuwa
Uongozi wakatwaa
Mambo yote ovyo kuwa
Mikosi pia balaa!

Hadithi yasimulia, Tabora kulikokuwa,
Wakubwa kutfutiwa, mabingi wapate poa,
Mutumaina akawa, mkuu awasimamia:
Taifa hulaaniwa, kati yao kuwa nao:
Wanasiasa fuska
Hupata watu wabaya
Kahaba wakachagua
Na wezi waliokuwa
Uongozi wakatwaa
Mambo yote ovyo kuwa
Mikosi pia balaa!

Amri alipopewa, akajua ni unaa,
Masikini watakiwa, thamani hawajapewa,
Hilo akalikataa, na akawabadilishia,
Taifa hulaaniwa, kati yao kuwa nao:
Wanasiasa fuska
Hupata watu wabaya
Kahaba wakachagua
Na wezi waliokuwa
Uongozi wakatwaa
Mambo yote ovyo kuwa
Mikosi pia balaa!

Mabinti kawatwaa, wa wakubwa walokuwa,
Vyumbani walipotomea, wakubwa wakashangaa,
Majina wanayopewa, ubaba uliokuwa:
Taifa hulaaniwa, kati yao kuwa nao:
Wanasiasa fuska
Hupata watu wabaya
Kahaba wakachagua
Na wezi waliokuwa
Uongozi wakatwaa
Mambo yote ovyo kuwa
Mikosi pia balaa!

Ya wenzao waliokuwa, pamoja wanapokaa,
Haya kuyashtukia, adabu ikawajia,
Mama walimtimua, ila pepo yamngojea:
Taifa hulaaniwa, kati yao kuwa nao:
Wanasiasa fuska
Hupata watu wabaya
Kahaba wakachagua
Na wezi waliokuwa
Uongozi wakatwaa
Mambo yote ovyo kuwa
Mikosi pia balaa!

Nchi hivi ikishakuwa, jua kwamba yaalaniwa,
Mitihani kungojea, midogo na mikubwa pia,
Na huruma kutegemea, Mola hatotusikia:
Taifa hulaaniwa, kati yao kuwa nao:
Wanasiasa fuska
Hupata watu wabaya
Kahaba wakachagua
Na wezi waliokuwa
Uongozi wakatwaa
Mambo yote ovyo kuwa
Mikosi pia balaa!

Sunday, February 26, 2012

Walioshindwa mbinu

Mbinu walioishiwa, wepesi kukimbilia,
Fujo kuzichochea, wavune yanayowafaa,
Ukubwa kuutetea, japo waisha raia,
Walioshindwa mbinu, mikakati na fikra:
Mabavu huyatumia!

Ni watu wa kuteua, watu wasiowafaa,
Yao waangalia, si ya wengi yakawa,
Ni laana tumeachiwa, bado tunaing'ang'ania,
Walioshindwa mbinu, mikakati na fikra:
Mabavu huyatumia!

Enzi za kutofikiria, ukingoni zafikia,
Watu wataulizia, hata yale yasokuwa,
Na wajibu kuwatia, wajifanyao wajua,
Walioshindwa mbinu, mikakati na fikra:
Mabavu huyatumia!

Majoho watawavua, yafichyo kuishiwa,
Ujinga wakawaachia, na wengine kuchagua,
Pasiwe wa kubakia, na mtu anayetumiwa,
Walioshindwa mbinu, mikakati na fikra:
Mabavu huyatumia!

Watu wao wapigao

Ni wale tuwajuao, nao ni kawaida yao,
Ukubwa wautakao, wale wao na wakwao,
Walinzi wafugwao, kulinda wakubwa wao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!

Hudhani wao ni wao, na nchi hii ni yao,
Katiba wapinduao, juu kujiweka wao,
Na wananchi walalao, wakawa nalo pumbao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!

Wasijue kuwa wao, ndio wao wafukuzao,
Asibaki mmojawao, zahama ikija kwao,
Uwe ni mwisho wao, na mwanzo wa wajuao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!

Sauti ni nyie mnayo, na mambo muamuoa,
Mkitaka watoke wao, kutoka lazima kwao,
Isiwe ni warudio, juu tena sio yao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!

Ni nyie muwawekao, na muamalizao,
Kwa lenu moja amuo, watoke hapo si kwao,
Wako wengi wenzao, nafasi waitakayo,
Watu wao wapigao, si amani watakao!

Haitoshi wajivuao, gamba liozalo kwao,
Na ngozi yenye kumbao, mwilini wabakiayo,
Uchago hulia wao, waulaliapo mwao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!

Naamba niwaambiao, nyakati hizi si zao,
Mabadiliko ni ngao, huvunjika zao tao,
Yajayo si wazuiayo, watatoka watokao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!

Kivumbasi mwanakwao, heri si wajaliwao,
Shetani ana kikao, mara kwa mara nao,
Na haya waamuayo, mwayaona yazuayo,
Watu wao wapigao, si amani watakao!

Urithi si watakao, wawapa kwanza wanao,
Kuua ni jadi yao, na wala sio wazaao,
Mti hujazaa mbao, si mbao yenye uzao,
Watu wao wapigao, si amani watakao!

Usitende bila fikra

Mnyama ungelikuwa, sawa tungelidhania,
Mambo kutofikiria, na kisha ukayaingia,
Utu yende kukuvua, na uchi ukabakia,
Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!

Fikra ni majaliw,a mja amezawadiwa,
Yafaa kufikiria, kabla haujaamua,
Na utenzi hutanguliwa, kwa mawazo yalokuwa,
Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!

Amri kuzipokea, ukatenda usojua,
Wewe umelaaniwa, na mbingu na ardhi pia,
Na moto wa kungojea, hunalo la kujitetea,
Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!

La haki lililokuwa, kulitenda inafaa,
Na haki lisilokuwa, ni wajibu kukataa,
Muogopeni Jalia, si watu kuwahofia,
Usitende bila fikra, waza kabla kutenda!

Binadamu si mashine

Hukuumbwa mashine, binadamu nakwambia,
Wapaswa kujitambua, akili kuitumia,
Watu wakikutumia, unakuwa ni kifaa,
Binadamu si mashine, apaswa kufikiria!

Itihari kajaliwa, kupima na kuchagua,
Afanye linalofaa, muktadha kuujua,
Na haki kuzingatia, kazini anapokuwa,
Binadamu si mashine, anapaswa kuchagua!

Ubongo kazawadiwa, apaswa kuutumia,
Na akishajipimia, mwenyewe akaamua,
Kwa vigezo vilokuwa, na watu na matukio,
Binadamu si mashine, anapaswa kuamua!

Vinginevyo ni bandia, mwanasesere akawa,
Wawe wamchezea, juu walotangulia,
Dhambi kumuachia, mwenyewe kujibebea,
Binadamu si mashine, apaswa kufikiria!

Wanasiasa balaa, fani yao yalaniwa,
Watu shere watezea, kama taahira wawa,
Ikawa wawakubalia, hata kwa yasiyokuwa,
Binadamu si mashine, anapaswa kuchagua!

Enzi zimeshaingia, watu kujiangalia,
Uhuru wakachagua, na haki kuzingatia,
Pasiwe wa kutumiwa, hadaa na kuzainiwa,
Binadamu si mashine, anapaswa kuamua!

Umeme unapozima

Kwenye nchi ya madoa, rangi tusiyoyajua,
Na amri za kuua, wadhani hawajaua,
Na yatakiwayo kuwa, yasiwe yenye kukua,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!


Ukuu wanaochukua, wasiwe pakuanzia,
Na wanaoyachimbua, wakadhani walimia,
Huwa nchi ya wafukua, kuzikwa kwao haijawa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!


Ndipo saa wazijua, kizani kutususia,
Mengi yananipitia, pembeni nilipokaa,
Wasiojua wajua, ndiyo nchi imekuwa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!


Hakuna wa kutumiwa, wote wataka tumia,
Kuvuna washangilia, kupanda wanakataa,
Wachache hupalilia, nao mimea hung'oa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!


Nchi ya wasiojijua, na kwendako wapotea,
Taifa lisilojifua, kutakata haijawa,
Na uchafu waujua, tena wanautumia,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!


Watu wa kusaidiwa, wasiojisaidia,
Nchi yenye kununua, chake isichokizaa,
Ni nchi ya kulaniwa, mbele haitoendelea,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!


Nchi ya viguu na njia, haiwezi kutulia,
Yao wasiotatua, ya wengine wakavaa,
Ni ya kusikitikiya, na tena kuhurumiwa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!


Ndio ninafurahia, umeme ukisinzia,
Huamka na kuzua, visa vya kuhadithia,
Kizazi kitachokuwa, haya kuja yaambaa,
Umeme unapozima, na giza likaenea:
Mwangaza hunifunua,
Utunzi nikaingia,
Hadi adhana ikawa!

Unajifanya usilokuwa ?

Haukuwa na hatuokuwa
Ijapo nafasi ulishaipewa
Kiumbe jema hukujaliwa
Ila mabaya umeumbiwa
Shetani amekuchukuwa
Kama kifaa unatumiwa
Naye si rahisi ukajaliwa
Minyororoni ukajitowa
Yawa kama umelaniwa
Kwa pako pema kukimbiwa
Ukakimbilia kwenye mabaya!
Wajifanya usilokuwa
Nuksi hapo ndio zaanzia!

Lugha ya watu mizizi

Nimeyaona Asia, Ulaya ni mazoea,
Lugha wanajivunia, hata kidogo wakiwa,
Nyengine kutotumia, ila nje wanapokuwa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!



Chao wanajivunia, bila ya kusimamiwa,
Na kisha waongezea, vya wengine kuvijua,
Ubingwa kujipatia, kwayo na yale ya dunia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Asili waangalia, urithi kutopotea,
Pia rahisi ikawa, watoto kujifunzia,
Lughani wakichipua, mengi sana huyajua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Leo hapa Tanzania, maneno yanapotea,
Ndege wetu kuwajua, wazima utawaumbua,
Sembese watoto kuwa, hawana wanalojua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Wanyama nao pia, wawili watatu wajua,
Samaki waliojaa, bahari nayo maziwa,
Wangapi watakwambia, majina waliyopewa?
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Miti na mingi mimea, hakuna anayejua,
Utacheka nakwambia, mjini ukiulizia,
Afadhali inakuwa, kijijini wanajua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Maumbo yake dunia, wengi utata hukuwa,
Bure utajisumbua, hakuna anayejua,
Na hawa wategemea, kitu kuja kuvumbua?
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Mizizi yake mmea, asili hutegemea,
Ndipo inapokuwa, kwa yote yanayokuwa,
Elimu ikiwa pia, muhimu kuzingatiwa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Watafeli nadharia, kwa lugha kutoijua,
Watoto kuwakandia, ya uongo yalokuwa,
Walimu kuwazulia, hata wasiyofikiria,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kiswahili kutumia, kufundisha nadharia,
Kwa undani kuelewa, yote yanayozungumziwa,
Haya wakishayajua, Kama China tutakuwa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Tuitenge nadharia, na lugha kufundishia,
Maabara kufungua, shuleni na vyuo pia,
Lugha kuzikazania, mbili tatu wakajua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Ndege wengi tutaua,kwa jiwe moja kutumia,
Sayansi wakaijua, na lugha kuzing'amua,
Hata Kiarabu pia, na Kichina kutumia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Mashariki inafaa, tuanze kuangalia,
Isiwe tunachelewa,
Wenzeetu wakatangulia,
Lugha yetu kujitia, lakini kutokutufaa,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Viongozi watakiwa, uzito kuuchukua,
Wafanze kuyaamua, mapema inavyokuwa,
Nami sintoshangaa, wengine kutangulia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kiingereza balaa, ujanja wanatumia,
Lugha yetu kuiua, na yao kuendlea,
Na sisi kamamajuha, mtegoni twaingia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Nyerere alianzia, lugha kasaliti pia,
Mwinyi alipofatia, naye akazainiwa,
Mkapa hakujitambua, wala hatajitambua,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kikwete asipojua, humo humo kufatia,
Kiswahili kukiua, na elimu nayo pia,
Ndicho kilichobakia, na ndiyo yanayotokea,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Ila mtunzi najua, rais wa Tanzania,
Kweli atakayekuwa, Kiswahili ataamua,
Kila ngazi kutumia, na nchi ikaendelea,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kwenye kapu watupiwa, wote waliotangulia,
Takataka watakuwa, kati yetu historia,
Nafasi waliipewa, ila hawakuitumia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kuthubutu hapakua, na kujaribu wapwaya,
Hakuna walilojaliwa, kuliweza na kujua,
Waigaji wabakia, ni wasanii bandia,
Lugha ya watu mizizi, ikikatwa mti hufa:
Au ikifukuliwa
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!

Thursday, February 23, 2012

Za sitini na sabini

Miye nilijiamini, katika hii dunia,
Nilizilishwa hisani, hadi moyo kujaa,
Sikuwa ni msshakani, kila nilipoingia,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Ninakumbuka shambani, na niliyojisomea,
Mimea kuithamini, na viumbe kuwalea,
Najiona majinuni, watoto wasivyojua,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Nakumbuka ya nyumbani, na ugenini pia,
Muziki wenye anwani, moyoni uloingia,
Na maudhui ya undani, kitu uliyochukua,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Nakumbuka vya thamani, vitu vilivyokikaa,
Si vitu kama utani, havikai huchakaa,
Na nyinginezo samani, hata zile za kubembea,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Nakumbuka wanandani, walionikimbilia,
Nikawapoza ubani, na udi kuwapatia,
Na walonipa hisani, hadi hapa kufikia,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Walimu wenye mizani, msingi wliokuwa,
Na sekondari mjini, Mawenzi walopitia,
Moshi na Mbeya mjini, na nilikotumikia,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Maelezo wahisani, mdogo walinichukua,
Kazi kunipa mezani, uandishi kufatia,
Na kutumwa mikoani, habari kuwaletea,
Nawajua njendani, miaka niliyopitia,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Ninakumbuka chuoni, na wapenzi walokuwa,
Tulipozila amini, kutoa sio kutwaa,
Na leo sina imani, wengine wamejifia,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Wanafunzi duniani, wapo wanaonijua,
Niliwafunza imani, na akili kutumia,
Wakaacha ya kughani, mengi wakayafikiria,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Nakumbuka ugenini, nje nilikosomea,
Ubelgiji yamini, Luveni iliyokuwa,
Masta nikaichukua, na pendo kuwaachia,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Kufikia themanini, nilikuwa nimerejea,
Nimeishi ugenini, moyoni nyumbani ukiwa,
Ila sasa mtihani, mengine nayafikiria,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Nakumbuka kwa yakini, nyimbo zilozotulia,
Zikikumbusha zamani, enzi zilizopotea,
Yamebaki maruhani, kichwani yakitembea,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.

Sina lililo thamani, vyote vinshapotea,
Nimebaki upwekeni, wapenzi wamepotea,
Uzeeni siamini, afueni kutokea,
Nazikumbuka mwenzenu, za sitini na sabini.